Kwanini Physics na Chemistry hazifundishwi makanisani na misikitini??

Kwanini Physics na Chemistry hazifundishwi makanisani na misikitini??

Retired Analyst

Senior Member
Joined
Apr 7, 2025
Posts
138
Reaction score
244
Kwanini taasisi za elimu (shule za Primary na Secondary) zinajipa majukumu ya kidini?? Mbona taasisi za kidini (makanisa na misikiti) hazijipi majukumu ya kitaaluma (academia)

Watoto wanatoka majumbani mwao wakijua wao ni wamoja. Wanaongozana pamoja on their way to school.

Watoto wanafika shule na kukaa assembly point wakijua wao ni wamoja.

Watoto wanaenda mapumziko wakijua wao ni wamoja na kwa pamoja wanachangishana pesa na kununua chipsi dume (Mihogo)

Watoto wanacheza wote soccer, netboll na rede wakijua wote ni wamoja.

Watoto wanafagia uwanja wakiwa wote ni wamoja.

Alafu inafika saa sita mchana igongwa kengele ya kuwaambia kuwa licha ya kushirikiana katika yote kuanzia kitembea pamoja kuja shule na kula wote Mihogo mapumziko, nyie sio wamoja bali nyie ni waislamu na wakristo.

Guys, this is nonsense ujue.

Hivi ni kitu gani huwa kinafujdishwa katika hizo so-called vipindi vya dini katika taasisi za elimu ambavyo havitafundishwa ama havikufundishwa katika misikiti Ijumaa iliyopita au Jumapili ijayo.

Hii nchi ina Policy and dicisions makers wa hovyo sana.
 
DIni ni kiwanda cha kuzalisha binadamu wasiweza kufikiri nje ya box, na njia rahisi ya kutawala watu ni kuwafumba wasiweze kufikiri nje ya box kwa kuwakaririsha stori za akina abunuani muhammad na yesu, hii huwajengea watoto hofu hata ya kuhoji vitu vidogo vidogo
 
Maana yake mambo ya ushirikina hayana ukweli ndio maana yanafichwa gizani... Yakiletwa nuruni/ kwenye hisabati na sayansi ikili itayatambua kuwa ya hovyo.

Sayansi, hisabati na kemia vinaruhusu uchunguzi ila huku kwenye imani unapaswa kwenda bila milango ya fahamu
Ndio maana ninakereka sana nikiona dini zinafundishwa katika taasisi za elimu
 
Elezea vizuri, Kuna ubaya gani watu wakijifunza hizo dini. Maana almost kila mtu ana dini yake na anaruhusiwa kuhudhuria kulingana na imani yake.
Imani ni jambo binafsi
Halikuhitaji kufundishwa kwa gharama ya Kodi zetu.
 
Kutokana na masaa waliyonayo,
Shuleni wanasoma siku tano kila siku anasoma masaa yasiyopungua nane ila kwenye dini anaenda jumamosi na jumapili anasoma masaa manne mpaka tano, na basic teaching ya mafunzo ya dini ni moral code, ethics na historia ya main figure kwenye dini husika, sasa unategemea hayo masaa manne waanze kuwafundisha electrolysis wakati anaweza kufundishwa shule
 
Elezea vizuri, Kuna ubaya gani watu wakijifunza hizo dini. Maana almost kila mtu ana dini yake na anaruhusiwa kuhudhuria kulingana na imani yake.
Kwani ikifundishwa katika taasisi za dini haitoshi?? Kuwafundisha watoto dini mashuleni ni sawa na kuwakumbusha tofauti zao ambazo walikwishaziacha majumbani mwao.
 
Kutokana na masaa waliyonayo,
Shuleni wanasoma siku tano kila siku anasoma masaa yasiyopungua nane ila kwenye dini anaenda jumamosi na jumapili anasoma masaa manne mpaka tano, na basic teaching ya mafunzo ya dini ni moral code, ethics na historia ya main figure kwenye dini husika, sasa unategemea hayo masaa manne waanze kuwafundisha electrolysis wakati anaweza kufundishwa shule
Hiyo title ya mada hii ina maana kila taasisi ibaki na jukumu lake la msingi.

Taasisi za elimu zina lengo la kuleta watoto pamoja na sio tena kuwagawa katika misingi ya dini zao.
 
Kwanini taasisi za elimu (shule za Primary na Secondary) zinajipa majukumu ya kidini?? Mbona taasisi za kidini (makanisa na misikiti) hazijipi majukumu ya kitaaluma (academia)
L
Toa shule za Katoliki hapo hawana mchezo kwenye masomo ya Sayansi

Shule zao zote za katoliki sekondari kusoma masomo ya sayansi O level sio hiari ni lazims utake usitake
 
Kwanini taasisi za elimu (shule za Primary na Secondary) zinajipa majukumu ya kidini?? Mbona taasisi za kidini (makanisa na misikiti) hazijipi majukumu ya kitaaluma (academia)

Watoto wanatoka majumbani mwao walijua wao ni wamoja.

Watoto wanafika shule na kukaa assembly point wakijua wao ni wamoja.

Watoto wanaenda mapumziko wakijua wao ni wamoja na kwa pamoja wanachangishana pesa na kununua chipsi dume (Mihogo)

Watoto wanacheza wote soccer, netboll na rede wakijua wote ni wamoja.

Watoto wanafagia uwanja wakiwa wote ni wamoja.

Alafu inafika saa sita mchana igongwa kengele ya kuwaambia kuwa licha ya kushirikiana katika yote kuanzia kitembea pamoja kuja shule na kula wote Mihogo mapumziko, nyie sio wamoja bali nyie ni waislamu na wakristo.

Guys, this is nonsense ujue.

Hivi ni kitu gani huwa kinafujdishwa katika hizo so-called vipindi vya dini katika taasisi za elimu ambavyo havijafundishwa ama havijafundishwa katika misikiti Ijumaa iliyopita au Jumapili/Jumamosi ijayo.

Hii nchi Ina Policy and dicisions makers wa hovyo sana.
Hamia nchi isiyo na vipindi vya dini mashuleni. Ficha upumbavu wako
 
Toa shule za Katoliki hapo hawana mchezo kwenye masomo ya Sayansi

Shule zao zote za katoliki sekondari kusoma masomo ya sayansi O level sio hiari ni lazims utake usitake
Ni wapi nimetaja shule ya katoliki??
 
Imani ni jambo binafsi
Halikuhitaji kufundishwa kwa gharama ya Kodi zetu.
Kina nani wanaolipa hizo kodi? Asilimia kubwa ya walipa kodi nchi hii ni hao wenye dini, so hao walipa kodi waliwahi sema wapi hawataki watoto wao wasifundishwe dini? Ama sasa hivi umeijua twitter na fb ghafla na wewe umekua Metl na Bakhresa?
 
Naunga hoja. Ni heri kungekuwa na kipindi cha maadili kwa watoto wote. Watoto wakafundishwa wizi sio mzuri pamoja na matendo yote mabaya. Wakafundishwa maadili mazuri katika jamii. Mambo ya dini yakafundishwa kwenye taasisi za dini.
 
Physics na chemistry ingekuwa inafundishwa misikitini waislam wangekuwa mbali sana. Hayo ni mambo ya imani hayachanganyiki na sayansi. Kule kwetu unaambiwa ya kaisari apewe kaisari na ya Mungu apewe Mungu
 
Kwanini taasisi za elimu (shule za Primary na Secondary) zinajipa majukumu ya kidini?? Mbona taasisi za kidini (makanisa na misikiti) hazijipi majukumu ya kitaaluma (academia)

Watoto wanatoka majumbani mwao walijua wao ni wamoja.

Watoto wanafika shule na kukaa assembly point wakijua wao ni wamoja.

Watoto wanaenda mapumziko wakijua wao ni wamoja na kwa pamoja wanachangishana pesa na kununua chipsi dume (Mihogo)

Watoto wanacheza wote soccer, netboll na rede wakijua wote ni wamoja.

Watoto wanafagia uwanja wakiwa wote ni wamoja.

Alafu inafika saa sita mchana igongwa kengele ya kuwaambia kuwa licha ya kushirikiana katika yote kuanzia kitembea pamoja kuja shule na kula wote Mihogo mapumziko, nyie sio wamoja bali nyie ni waislamu na wakristo.

Guys, this is nonsense ujue.

Hivi ni kitu gani huwa kinafujdishwa katika hizo so-called vipindi vya dini katika taasisi za elimu ambavyo havijafundishwa ama havijafundishwa katika misikiti Ijumaa iliyopita au Jumapili/Jumamosi ijayo.

Hii nchi Ina Policy and dicisions makers wa hovyo sana.
Jenga shule yako binafsi toa vipi Di vya dini, Shule za Serikali zinahudumia watanzania na watanzania ndio wanaochangia serikali, na serikali inapaswa kutimiza matakwa ya Watanzania, Watanzania wana dini na wanataka Watoto wao wawe na maadili.
 
Back
Top Bottom