Kwanini Panya road isishughulikiwe?

Kwanini Panya road isishughulikiwe?

Askari Muoga

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
6,112
Reaction score
4,663
Hivi hawa Panya road wameshindikana? Imekosekana dawa ya kuwazuia makundi kama aya ya uhalifu? Ni hatari tukiendelea kuyaacha na kushabikia bila kuangalia kiini au chimbuko la panya road.

Nakumbuka zamani miaka ya 2006 nilikuwa nawasikia mbwa mwitu ila sasa panya road. Kwanini wasiwafuatilie na kujua chanzo cha hawa panya road wanaotupelekea kuwa na wasiwasi na kufunga maduka mapema?
 
Hakuna panya road Bali vigenge vya vijana ukienda kigogo kuna camps vijana hawana kazi wanavuta bangi na wakazi wa huko hujihusisha kupora,ukienda goms hvy hvy vijana wengi wanamaliza form4 wamefeli hawana kazi wanaishia kukaa maskani na kuvuta bangi ukienda mbagala ,manzese nk nk

Huku mtaani kwetu wapo lkn baadhi wamepungua wanamiliki bodaboda lkn camps hz za vijana kitaani wanavuta bangi kazi hawana nk

Kiini vijana wengi wanaishia o level wanakaa kitaani tu maskani na wengi under 25 hawana kazi
 
Hivi hawa Panya road wameshindikana? Imekosekana dawa ya kuwazuia makundi kama aya ya uhalifu? Ni hatari tukiendelea kuyaacha na kushabikia bila kuangalia kiini au chimbuko la panya road.

Nakumbuka zamani miaka ya 2006 nilikuwa nawasikia mbwa mwitu ila sasa panya road. Kwanini wasiwafuatilie na kujua chanzo cha hawa panya road wanaotupelekea kuwa na wasiwasi na kufunga maduka mapema?
Duka liko chimbo gani, nauliza tu
 
Hivi hawa Panya road wameshindikana? Imekosekana dawa ya kuwazuia makundi kama aya ya uhalifu? Ni hatari tukiendelea kuyaacha na kushabikia bila kuangalia kiini au chimbuko la panya road.

Nakumbuka zamani miaka ya 2006 nilikuwa nawasikia mbwa mwitu ila sasa panya road. Kwanini wasiwafuatilie na kujua chanzo cha hawa panya road wanaotupelekea kuwa na wasiwasi na kufunga maduka mapema?


Hili swala linatakiwa kudhibitiwa kuanzia mbali sana,
  • Wazazi majumbani kuhakikisha wanawalea watoto wao katika maadili mema na kushirikiana na wanajamii wengine kuhakikisha watoto katika mtaa wao wanazingatia maadili
  • Walimu mashuleni wapewe ushirikiano na wazazi katika kutatua changamoto zinazohusu mwenendo mbaya wa watoto wao na hasa pale wanapoambiwa wafike shuleni kwa ajili ya mashauriano
  • Serikali itazame namna mtaala wetu wa elimu unavyoweza kuwa na tija kwa watoto wetu na hasa katika kuweka mazingira ya watoto wetu kupata mafunzo ya namna ya kupata mtaji na kujiajiri wamalizapo masomo yao
  • Vyombo vya usalama vijenge mahusiano mema yenye tija na kushirikiana kwa karibu na raia wema wanaotoa taarifa za kihalifu, ikiwezekana kuwapa raia hao motisha (chonde vyombo vya usalama sina nia mbaya nasema kwa nia njema tu,)
Bila kuyatama mambo kadha wa kadha tutabaki kuwa watu wa kushangaa matukio kila kunapokucha
 
Back
Top Bottom