Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Wandau wa JF, mara nyingi huwa tunasisitizana kutanguliza uzalendo mbele katika mambo mbalimbali tunayoyatenda. Mojawapo ya vitambulisho vya uzalendo na utaifa wa mtu ni wimbo wa Taifa lake. Hoja yangu kwa wadau, kwa nini sisi Watanzania wimbo wetu wa Taifa uendelee kuanza na Mungu Ibariki Afrika badala ya Mungu Ibariki Tanzania. Wengine watasema kwamba, ni namna moja wapo ya kumuenzi Mwalimu JK ambaye wakati ule, pamoja na wenzake akina kwame Nkuruma, walikuwa na fikra za kuwa na Afrika moja. Imeshapita zaidi ya miaka arobaini sasa tangu nchi za Kiafrika zianze kujipatia uhuru, na Afrika moja imekuwa ni njozi, badala yake kuna Taasisi ambazo zinaundwa na kutuongezea gharama zisizo za lazima, kama hili Bunge la Afrika, au Afrika Mashariki.
Nadhani kuna haja ya kubadili mpangilio wa wimbo wetu wa Taifa ili uanze na Mungu Ibariki Tanzania halafu ndo ifuate Mungu Ibariki Afrika.
Natoa hoja kwa Mjadala
Nadhani kuna haja ya kubadili mpangilio wa wimbo wetu wa Taifa ili uanze na Mungu Ibariki Tanzania halafu ndo ifuate Mungu Ibariki Afrika.
Natoa hoja kwa Mjadala