Ikiwa dunia inavuta vitu mbalimbali kuelekea chini kupitia nguvu ijulikanayo kama "gravitational force".
Je kwanini nguvu hiyo ya "gravitional force" haivuti moshi kuelekea down badala yake moshi huo huelekea tu angani?je ni nguvu ipi inayopelekea moshi kuvutika kuelekea tu angani?
Mwenye uelewa wa kutosha naomba anisaidie juu ya swali hilo
Mawazo yangu;-
1. Moshi sio massless kama walivyosema baadhi ya wachangiaji. Ukweli ni kwamba moshi una mass.
2. Kwa sababu namba moja hapo juu (moshi una mass) ina maana moshi una experience the effect of gravitational force (unavutwa kuelekea katikati ya dunia).
Je, kwanini unaenda juu wakati centre ya dunia ni chini na katika kwenda juu huko unaenda freely (haitumiki nguvu yoyote) tofauti na bombardier (ndege) za Magufuli zinavyopaa angani (hizi huwa zinatumia nguvu fulani kufanya hivyo nadhani forces na pressure).
Maelezo mafupi;-
Tuna hali tatu za mada (three states of matter) yaani yabisi (solid), kimiminika (liquid) na gesi (gas). Kitu kikiwa katika hali ya kimiminika na gesi kuna mpangilio maalumu nani awe chini nani awe juu pale VINAPOCHAMGANYWA na kutengeneza MCHANGANYIKO USIO MWANANA (Heterogeneous mixture) yaani vinapochanganywa na kila kitu kukaa pekeyake. Mfano maji na mafuta.
Nani akae juu nani akae chini hutegemea ni yupi mwenye density kubwa (atakaa chini) na yupi mwenye density ndogo (atakaa juu ya mwenzake) katika mpangilio huo.
Hali ni tofauti kwenye solid state kwa sababu unaweza kuweka kipande cha tofali juu ya kipande cha keki na pia kwenye homogeneous mixture (mchanganyiko mwanana) mfano maji na maziwa (hauwezi kusema nani atakaa juu nani chini).
Jibu:-
Kwa sababu moshi ni less denser than air (una density ndogo kuliko hewa) unaenda "kujipanga juu" then unakua attracted towards the centre of the earth from there. Hii ndio sababu kwanini moshi unakwenda juu licha ya kwamba kuna hiyo nguvu ya uvutano kuelekea katikati ya dunia.
Asante.