Kwanini mke haelewani na wifi?

Ila inakera sana. Bora mtu kutokuoa. Kama wewe hujaoa, mpe exam mkeo ya kuwazoea dada zako.

Mkuu Kama alivyosema Kaunga hii kitu ni ya pande mbili. Na mara nyingi huanzishwa na dada wa kaka kwa kutaka mkeo aishi kutokana na matakwa yao wao. na wakati mwingine huanzishwa na Mkeo asipokuwa na uelewa wa kutosha kwa namna ya kuishi na jamii ya watu wengine tofauti na familia alioizoea.


Mkuu kwa habari ya hii mambo huwa ni ngumu sana kuamua au kusuluhisha usipojitahidi kuwa ''independent'' nikimaanisha usichukue maneno ya upande mmoja na kuyafanyia kazi, jipe muda, chunguza na atakayekuwa ameenda kinyume na mwingine umuonye mbele ya wengine kwa HAKI, Kama ni dada zako unawakemee kwa haki na kama ni mkeo unamkemea kwa haki, hapo utaanza kujenga uhusiano na heshima kwa kila mmoja.

Mwisho jitahidi sana kuwa na msimamo wako kama Mwanaume na kama kichwa cha nyumba yako.
usiache dada zako na mama yako wamue namna ya wewe na nyumba yako muishi. You are the head so they under your terms.

Maneno ya hekima yanasema katika kitabu cha mwanzo kuwa ''Mtu mume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na Mkewe nao watakuwa mwili mmoja'' so kuna matatizo mengine inaweza pia kuwa wewe mwanaume ni chanzo pasipo kujua. so jitahidi kuangalia kama role yako kama mwanume una-play fairly

''nani alikuambia wanawake wanapendana kiasi hicho hata waishi pamoja kwa amani na uelewano? ni wachache sana kaka wa namna hiyo''
 
Samahani kwa kutumia neno hilo la "mjinga". Ila nilimaanisha mke anayeendekeza ugomvi pasipo na sababu. Mazingira niliyochukulia ni yale yenye "all people are ignorant under a corporate veil" Kwamba hujawahi kujua kama wifi zako ni wakorofi, ila wewe unaanzisha kuwachukia tu wifi zako bila kuangalia mazingira yao.
kwahiyo umethibitisha kwamba mawifi sio wakorofi ila mkeo ndio mkorofi sio?? je hatak kukaa nao kwenye nyumba moja ama hatak kushirikiana nao?? ama ana maneno ya uchonganish na umbea??
 
Hapo naelewa concern
yako, ila mi nilichotaka kuongelea je pakiwa na wifi zako wadogo (form
one au hawajaanza shule) au wengine wapo wapo tu, na wao hawana ugomvi
(chukulia wale ambao hawajakulia mijini--yaani siyo wambea mbea). Je
chuki ya nini kwa watu ambao hawajakuchokoza?

Tena hao ndio wabaya maana wanaendeshwa kwa remote! Ana shida anampigia mama yake mkoa,mama anampigia mumeo amsaidie mtoto wewe huna habari! Mwe!
 
Mkuu Kama alivyosema Kaunga hii kitu ni ya pande mbili. Na mara nyingi huanzishwa na dada wa kaka kwa kutaka mkeo aishi kutokana na matakwa yao wao. na wakati mwingine huanzishwa na Mkeo asipokuwa na uelewa wa kutosha kwa namna ya kuishi na jamii ya watu wengine tofauti na familia alioizoea.


Mkuu kwa habari ya hii mambo huwa ni ngumu sana kuamua au kusuluhisha usipojitahidi kuwa ''independent'' nikimaanisha usichue maneno ya upande mmoja na kuyafanyia kazi, jipe muda, chunguza na atakayekuwa ameenda kinyume na mwingine umuonye mbele ya wengine kwa HAKI, Kama ni dada zako unawakemea kwa haki na kama ni mkeo unamkemea kwa haki, hapo utaanza kujenga uhusiano na heshima kwa kila mmoja.

Mwisho jitahidi sana kuwa na msimamo wako kama Mwanaume na kama kichwa cha nyumba yako, '

Maneno ya hekima yanasema katika kitabu cha mwanzo kuwa ''Mtu mume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na Mkewe nao watakuwa mwili mmoja'' so kuna matatizo mengine inaweza pia kuwa wewe mwanaume ni chanzo pasipo kujua. ''nani alikuambia wanawake wanapendana kiasi hicho hata waishi pamoja kwa uelewano? ni wachache sana kaka wa namna hiyo''



Bold na Blue, hizo point nazikubali. Ila sasa kwa nini hata mwanamke ambaye ni msomi anashindwa kuelewa jinsi ya kuishi na watu ambao hawajaenda shule, tena ambao ni humble to the ground? Ila ulivyosema pande mbili ni kweli ila nadhani pia mke kama msaidizi wa mume she need to be bold and speak out of anywrong doing za wifi, wakati mwingine mke anaweza kausha, haswa wifi wanapoboronga anasubiria waharibu zaidi halafu anakuja kusema eti siku nyingi alikuwa anafanya hivyo, then unamuuliza why hukusema, anabaki kimya, je huyu utamuhesabu ni mke??
 
Tena hao ndio wabaya maana wanaendeshwa kwa remote! Ana shida anampigia mama yake mkoa,mama anampigia mumeo amsaidie mtoto wewe huna habari! Mwe!
Sasa hapo shida ni uwazi wa wanandoa. Nadhani kama hakuna dhamira ya kuwa wawazi kwa wanafamilia nalo ni tatizo.
 
Bold na Blue, hizo point nazikubali. Ila sasa kwa nini hata mwanamke ambaye ni msomi anashindwa kuelewa jinsi ya kuishi na watu ambao hawajaenda shule, tena ambao ni humble to the ground? Ila ulivyosema pande mbili ni kweli ila nadhani pia mke kama msaidizi wa mume she need to be bold and speak out of anywrong doing za wifi, wakati mwingine mke anaweza kausha, haswa wifi wanapoboronga anasubiria waharibu zaidi halafu anakuja kusema eti siku nyingi alikuwa anafanya hivyo, then unamuuliza why hukusema, anabaki kimya, je huyu utamuhesabu ni mke??

Nakubaliana na wewe Mkuu, kuwa tulitegemea mtu msomi aweze kukabiliana na changamoto kiusomi zaidi. lakini imekuwa kinyume chake. japo kuna ishu ya hekima na busara ya mtu lakini elimu nayo ni nguzo muhimu kwa mtu.


Kwa bahati mbaya usomi mwingi wa kwetu (sijajua bado kama ni mfumo wa elimu au ni sis wasomi au ni wakufunzi) Kuna tatizo kubwa sana. Usomi kwa wengi umekua kuvuka vidato lakini kwa akili/fikra zile zile, busara zilezile tabia zile zile na hulka zile zile. wakati tulitegemea kadiri mtu anavyoendelea kielimu, ile elimu ionekane ikimsaidia yeye kwanza katika nyanja zote za ujinga na upumbavu. Bahati mbaya kuna watu usipowauliza wana level gani ya elimu, ukimsikiliza tu kidogo unakadiria ni form four failure kumbe kamaliza chuo. kwa hiyo wakati mwingine tusipime usomi wamtu kwa level ya madarasa aliopitia.

Kuna vitu vingine (vingi vizuri na vya kutusaidia sana) havifundishwi madarasani jamani, tuamke, tujifunze kusoma maadishi mbalimbali na tujifunze kwa bidii kutoka kwa watu wanaotuzunguka. Hata kwenye ujinga kuna kitu cha kujifunza.
 
Wadau ni suala ambalo
mie limenisumbua kidogo. Kwa nini wake huwa hawaelewani na wifi zao? Je
ni ujinga wa wake? au? Yaani wakati mwingine unaweza kuta mke ni msomi
anashindwa kuelewana na wifi zake ambao either ni wadogo au wakubwa
hawajaenda shule, why? mwenye experience.

Ni vile kila mtu anataka akae kwenye mstar wa mwenzake,wifi ataka aplay role za dada mtu na dada mtu nae hvo hvo,hapo ugonvi hauepukiki
 
roho ya kwa nin!! ikitokea kwammoja wapo either wifi or mke lazma wagombane!!! but all in all!! ujinga na roho mbaya!!
 
uchoyo, ubinafsi, na poor mentality ya wakezetu, pia hudanganywa vijiwen wanaposukana yakuwa ndugu wa mwanaume wanafitna, ukweli hili nitatizo tena wanawake wengine hufika mbali hadi kwa wakwe zao.upande mwingine mawifu nao huwa na chokochoko kwa wakezetu ila kama wanajua msimamo wako hutulia.elimu inahitajika pande zote ili kunusuru ndoa zetu.
 
nashukuru Mungu mie na mawifi zangu tunapatana sana, hata mama mkwe pia tunaelewana.

hongera sana kwa hilo,ila jindae kwa lolote mbeleni ili usijekujuta wao kukufaham kiundani,chezea wawifi wewe!!
 
neggirl, nimekuelewa. Ila sasa chanzo cha chuki ndiyo mi nashindwa kuelewa. Mimi kama mwanaume unaweza kukuta nawapenda sana wadogo za mke wangu, wawe wa kike au mkiume. Ila kwa wanawake hii inakuwa tabu. Mfano, kama mke akijua unawasaidia wadogo zako haswa wa kike roho inamuuma sana, tena anakuwa anaona eti hatuwezi wasaidia wote, anakuwa na ile roho mbaya ile mbaya ya kutu kabisa. Sasa mi kinachonitatiza, kwa nini wawe vile?
Wanaume mnashindwa kuelewa nafasi yenu kwenye ndoa wewe ni kichwa unatakiwa kutawala kwa akili sio kwa upendeleo kama mkeo hapatani na dada yako oongea na mkeo kwa upendo nini unataka na atakuelewa ila ukitaka kujifanya unampotezea akikulalamikia ndo unawasha moto pili punguza kuongelea mabaya ya ndugu zako kwa mkeo hiyo inampa nafasi ya kuwachukia ndugu zako
 
Back
Top Bottom