Ben Zen Tarot
JF-Expert Member
- Dec 13, 2014
- 3,910
- 6,704
Sababu kubwa kuliko zote mganga anajua madhara ya hela za masharti, kwahiyo hawezi kuhatarisha maisha yake na familia yake!!¡
Ukienda kwa mganga unataka utajiri cha kushangaza yeye hana hata mbuni!
Anachofanya mganga anakuwa kama dalali wa kukuitia majini watakaokupa huo utajiri kwa masharti watakaopanga wao!!!
Kama unavyojua dalali lazima umlipe kwa kazi anayokufanyia ya kukurahisishia unachokitaka mganga naye utamlipa kulingana na mtakavyokubaliana.
Jini naye atahitaji malipo kumbuka yeye hahitaji pesa anazo za kutosha malipo yake anaweza dalali (mganga) asikuambia lakini utajua tu. (hakuna cha bure).
Kwahiyo mganga atawasiliana na majini popote walipo na kuwaambia kuna mtu anataka hela zenu, atajitokeza jini ambaye atatoa hela maelekezo yote yatàpitia kwa mganga yaje kwako na wewe utatekeleza maagizo yote ambayo huyo jini atayasema.
Baada ya kukubaliana na matakwa ya jini na kuyafanyia kazi, utaanza kupata mihela na baada ya hapo utaona mabadiliko makubwa katika maisha yako, mara umefiwa na mama mara umefiwa na mtoto mara unatakiwa kuua ndugu mmoja kila mwaka na mengineyo!!!
Kuna watu wanalala kwenye majeneza na vitimbi vya kila aina, hata ukirudi kwa mganga kuomba avunje mkataba huwa ngumu sana!!!
Ukienda kwa mganga unataka utajiri cha kushangaza yeye hana hata mbuni!
Anachofanya mganga anakuwa kama dalali wa kukuitia majini watakaokupa huo utajiri kwa masharti watakaopanga wao!!!
Kama unavyojua dalali lazima umlipe kwa kazi anayokufanyia ya kukurahisishia unachokitaka mganga naye utamlipa kulingana na mtakavyokubaliana.
Jini naye atahitaji malipo kumbuka yeye hahitaji pesa anazo za kutosha malipo yake anaweza dalali (mganga) asikuambia lakini utajua tu. (hakuna cha bure).
Kwahiyo mganga atawasiliana na majini popote walipo na kuwaambia kuna mtu anataka hela zenu, atajitokeza jini ambaye atatoa hela maelekezo yote yatàpitia kwa mganga yaje kwako na wewe utatekeleza maagizo yote ambayo huyo jini atayasema.
Baada ya kukubaliana na matakwa ya jini na kuyafanyia kazi, utaanza kupata mihela na baada ya hapo utaona mabadiliko makubwa katika maisha yako, mara umefiwa na mama mara umefiwa na mtoto mara unatakiwa kuua ndugu mmoja kila mwaka na mengineyo!!!
Kuna watu wanalala kwenye majeneza na vitimbi vya kila aina, hata ukirudi kwa mganga kuomba avunje mkataba huwa ngumu sana!!!