Baada ya Baraza Kuu la Chadema kutupilia mbali Rufaa zao na kuthibitisha kuwafukuza uanachama wa Chadema, Halima Mdee na wenzake hawatathubutu kwenda Mahakamani Kwa sababu zifuatazo;
1. Watakuwa na maswali mengi ya kumjibu Kuhusu walivyoupata huo Ubunge wao, Nani alisaini nyaraka zao, Nani alijaza fomu Kwa Niaba ya Katibu Mkuu wa Chadema na ili kujitetea watalazimika kuwasilisha nyaraka hizo.
2. NEC Itaingizwa kwenye kashfa ya Karne, kwani wataitwa Mahakamani kama mashahidi juu ya Nani aliwapa barua za uteuzi na fomu namba 12C ambazo zinatakiwa kusainiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha siasa.
3. Nusrat Hanje, alitolewa Gerezani usiku na kwenda kuapishwa kuwa Mbunge, atatakiwa kujibu alitolewa Kwa utaratibu upi na aliwezaje kujaza fomu za kugombea Ubunge akiwa Gerezani? Ataliingiza Jeshi la Magereza katika kashifa kubwa ya jinsi wasivyofuata sheria za Magereza.
4. Nyaraka za kugushi, watakuwa na mzigo wa kujieleza kuhusu nyaraka walizogushi Kwa kushirikiana na NEC ili wateuliwe kuwa wabunge, Jambo hili litaivua nguo tume na Serikali nzima.
5. Hawa Mwaifunga,Kunti Yusuph na Grace Tendega watakuwa na kazi ya kuieleza Mahakama ushiriki wa Katibu wa wabunge wa CCM Rweikiza katika kuandaa orodha ya majina ya wabunge hao! Kazi hii itaivua nguo CCM na jinsi walivyoweza kushiriki kwenye kashfa hii!
6 . Spika Job Ndugai , atatakiwa kuitwa na kuwa Shahidi kueleza alikopata orodha ya wabunge hao,na baada ya Chadema kuwafukuza ni Kwa nini aliendelea kuwakumbatia Kinyume na Katiba ya JMT ibara ya 71(1)(e), ambayo imetamka wazi kuwa Mbunge atapoteza sifa za kuwa Mbunge kama atafukuzwa uanachama na Chama chake cha siasa! Hapo patakuwa patamu Sana ! Ndugai ndio itakuwa fursa kwake kulipiza kisasi Kwa Dola?
Hizi ni baadhi ya sababu ambazo zinawafanya wajiulize kama wakifika Mahakamani watapona au ndio itakuwa kilio na kusaga Meno!
1. Watakuwa na maswali mengi ya kumjibu Kuhusu walivyoupata huo Ubunge wao, Nani alisaini nyaraka zao, Nani alijaza fomu Kwa Niaba ya Katibu Mkuu wa Chadema na ili kujitetea watalazimika kuwasilisha nyaraka hizo.
2. NEC Itaingizwa kwenye kashfa ya Karne, kwani wataitwa Mahakamani kama mashahidi juu ya Nani aliwapa barua za uteuzi na fomu namba 12C ambazo zinatakiwa kusainiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha siasa.
3. Nusrat Hanje, alitolewa Gerezani usiku na kwenda kuapishwa kuwa Mbunge, atatakiwa kujibu alitolewa Kwa utaratibu upi na aliwezaje kujaza fomu za kugombea Ubunge akiwa Gerezani? Ataliingiza Jeshi la Magereza katika kashifa kubwa ya jinsi wasivyofuata sheria za Magereza.
4. Nyaraka za kugushi, watakuwa na mzigo wa kujieleza kuhusu nyaraka walizogushi Kwa kushirikiana na NEC ili wateuliwe kuwa wabunge, Jambo hili litaivua nguo tume na Serikali nzima.
5. Hawa Mwaifunga,Kunti Yusuph na Grace Tendega watakuwa na kazi ya kuieleza Mahakama ushiriki wa Katibu wa wabunge wa CCM Rweikiza katika kuandaa orodha ya majina ya wabunge hao! Kazi hii itaivua nguo CCM na jinsi walivyoweza kushiriki kwenye kashfa hii!
6 . Spika Job Ndugai , atatakiwa kuitwa na kuwa Shahidi kueleza alikopata orodha ya wabunge hao,na baada ya Chadema kuwafukuza ni Kwa nini aliendelea kuwakumbatia Kinyume na Katiba ya JMT ibara ya 71(1)(e), ambayo imetamka wazi kuwa Mbunge atapoteza sifa za kuwa Mbunge kama atafukuzwa uanachama na Chama chake cha siasa! Hapo patakuwa patamu Sana ! Ndugai ndio itakuwa fursa kwake kulipiza kisasi Kwa Dola?
Hizi ni baadhi ya sababu ambazo zinawafanya wajiulize kama wakifika Mahakamani watapona au ndio itakuwa kilio na kusaga Meno!