Kwanini Mbeya ni jiji?

Kwanini Mbeya ni jiji?

Mtoa post namfananisha na mkuu mmoja iv alisema tz inapiga hatua yaani maendeleo kutokana na uwepo wa foleni, du! it is shameful
 
Tanzania majiji ni mawili tu
Dar na Mwanza...Mbeya ni 'big village'
Arusha nayo ni 'big village'.....

Uliza watu wa arusha kuna barabara ngapi za lami....za kuingia na kutoka Arusha..
jibu utakalopewa ndo utajiuliza ni jiji au big village
 
Nimeshangazwa na nilichokisikia asubuhi, taarifa za barabarani (radio one).

Arusha wamesema barabara zina msongamano wa magari sehemu za kuingilia jijini,
Mwanza the same, Dar magari yamejaa na kuna foleni...

Kutoka Mbeya magari ni machache ila waendesha mikokoteni ndiyo wengi madereva wawe makini...
Mbeya jiji na uwingi wa waendesha mikokoteni inakuwaje? hadi traffic kutoa taarifa za uwingi wa mikokoteni!!

Halafu wewe ni JF senior expert member. Aibu...
 
Nimeshangazwa na nilichokisikia asubuhi, taarifa za barabarani (radio one).

Arusha wamesema barabara zina msongamano wa magari sehemu za kuingilia jijini,
Mwanza the same, Dar magari yamejaa na kuna foleni...

Kutoka Mbeya magari ni machache ila waendesha mikokoteni ndiyo wengi madereva wawe makini...
Mbeya jiji na uwingi wa waendesha mikokoteni inakuwaje? hadi traffic kutoa taarifa za uwingi wa mikokoteni!!


weye ulitaka mbeya iitweje?
A.iitwe kijij?
B.iitwe mji?
C.iitwe manispaa?
D............?

Alafu ulivyokuwa mbulula, unasema umesikia wakisema kuna mikokoten ming.....

Nilifikili umefanya utafiti kwa kutembelea majiji tuliyonayo na ukarejea ktk SIFA STAHIKI ZA MKOA KUITWA JIJI na hatimaye kuja na mchanganuo\hoja nzito za kulikandia jiji la mbeya.Weye waja hapa na hadith za Umbea eti sababu tu umesikia wakisema.
 
M nimetoka dar,sasa niko arusha,bahat nzur mbeya ndio mkoa naotokea zaidi ya dar kuwa na folen kali,hii mikoa mengne wanaodai ina foleni ni uzush tu,foleni inatembea,labda siku hyo itokee wagombea wa urais wanapita ndio kutakuwa na jam tena siyo ya kuilinganisha na dar ukisimamishwa ili mkulu apite
 
To be frank,Mbeya na Mwanza kidogo unaweza hona hadhı ya jiji kwa kuzingatia idadi ya watu na ukubwa wa eneo la mji.LAKINI Tanga na Arusha hakıka sıo majiji bali manispaa.Arusha unaweza izunguko yote ndani ya saa1 na kwa miguu ukaimaliza.Tanga vivo hvyo.
 
Mbeya si jiji kama Mbeya ni jiji na tukuyu ni jiji
 
weye ulitaka mbeya iitweje?
A.iitwe kijij?
B.iitwe mji?
C.iitwe manispaa?
D............?
Jiji la Mikokoteni...

Alafu ulivyokuwa mbulula, unasema umesikia wakisema kuna mikokoten ming.....
yah!! ilikuwa taarifa na nimesikia ulitaka nione ndiyo niandike?
Wewe siyo Mbulula ni Mbuzurwa!!!

Nilifikili umefanya utafiti kwa kutembelea majiji tuliyonayo na ukarejea ktk SIFA STAHIKI ZA MKOA KUITWA JIJI na hatimaye kuja na mchanganuo\hoja nzito za kulikandia jiji la mbeya.Weye waja hapa na hadith za Umbea eti sababu tu umesikia wakisema.

Kwani issue ni nini hapa? mbona unasoma afu unaingiza hisia.... nilishangazwa sana na taarifa ya watu kutahadharishwa na waendesha mikokoteni,
Ni taarifa kutoka kwa traffic Mbeya!! we unataka niseme huyo traffic kakosea? badala ya kusema magari kasema mikokoteni?
 
Tanzania majiji ni mawili tu
Dar na Mwanza...Mbeya ni 'big village'
Arusha nayo ni 'big village'.....

Uliza watu wa arusha kuna barabara ngapi za lami....za kuingia na kutoka Arusha..
jibu utakalopewa ndo utajiuliza ni jiji au big village

Arusha at least, ila Mbeya bado local sana.
 
ulipokuwa o-level kwenye civics hukusoma qualifications za jiji?

jiji sio wingi wa magari mfano mzuri ni jiji la Sidney Australia, ni jiji lililo kwenye top ranks kidunia lakini ishu ya foleni za magari hakuna...

ume over translate!!!
 
Mtoa post namfananisha na mkuu mmoja iv alisema tz inapiga hatua yaani maendeleo kutokana na uwepo wa foleni, du! it is shameful

correct him/her kama una hoja ya msingi...
 
Mbeya haina hadhi kabisa ya kuitwa jiji. Nilipokwenda mbeya 2010 nilishangaaa sana kuona jinsi kulivyo na nilivyo ambia. Hapafai kuitwa jiji. Na center ya jiji sijui ni wapi. Mwanjelwa eh au wapi?
 
Ivi centa ya jiji la mbeya ni wapi mwanjelwa au huku stend
 
Mbeya city, wilaya ya mbozi tafuteni mtoa Uzi mumhoji vzr.
 
Nimeshangazwa na nilichokisikia asubuhi, taarifa za barabarani (radio one).

Arusha wamesema barabara zina msongamano wa magari sehemu za kuingilia jijini,
Mwanza the same, Dar magari yamejaa na kuna foleni...

Kutoka Mbeya magari ni machache ila waendesha mikokoteni ndiyo wengi madereva wawe makini...
Mbeya jiji na uwingi wa waendesha mikokoteni inakuwaje? hadi traffic kutoa taarifa za uwingi wa mikokoteni!!

CCM Mtandao walihakikisha maendeleo haysingii Mbeya.
 
ume over translate!!!

wewe ina judge kwa kusikia kwenye redio one... mi majiji yote ya tz nimefika kasoro Tanga tu...
so naona kabisa kwa hadhi ya majiji mengine, mbeya nayo ni jiji...
sifa za jiji ni pamoja na idadi ya watu/makazi, pato la halmashauri, miundombinu, universities availability, shughuli za uzalishaji+viwanda nk...

uwepo wa foleni haipo kabisa kwenye sifa za jiji
 
Tanzania majiji ni mawili tu
Dar na Mwanza...Mbeya ni 'big village'
Arusha nayo ni 'big village'.....

Uliza watu wa arusha kuna barabara ngapi za lami....za kuingia na kutoka Arusha..
jibu utakalopewa ndo utajiuliza ni jiji au big village

Tatizo mnatumia standards za New York na London!
Kwani sifa za kuwa jiji ni nini?
Nafikiri idadi ya wakazi ni sifa mojawapo kubwa!
 
Back
Top Bottom