Sbb kubwa wazalendo wanataka Mh. JPM aongezewe muda si kingine bali ni speed kubwa ya maendeleo ya wazi kabisa, yaani maendeleo huhitaji kuelezewa, unaona kwa macho yako kwa muda mfupi sana, pia kawafuta kabisa majambazi, wezi, wala rushwa, mafisadi, watumishi hewa na wenye vyeti feki, uzembe na uvivu serikalini, wazungu wezi wa rasilimali za nchi yetu wamekubali kulipa share deal kwa serikali kwa kila sekta iwe madini, simu, utalii, etc..
Ni mengi mengii mengiiii makuu Mh. JPM kayafanya kwa speed ya ajabu, wakati mwingine nashangaa haya yanawezekana vipi? Kama siamini, ila naona kwa macho yangu, najisemea Eeh Mungu, huyu Rais wa sasa kwanini asikae walau hata miaka yote hadi akatae au apewe na wananchi hata miaka 20 tu dunia nzima itashangaa kwa hatua kubwa tutakayo piga ya maendeleo, China mwaka huu imempa Xi aongozee China bila kuwa na kikomo, yote sbb ya maendeleo ya haraka sana hadi US wanawaheshimu na wanaogopa sana China.. Sisi watanzania ni uamuzi wetu sasa tuamue, Katiba ni yetu, katiba sio Biblia au Quran, tunaweza kuamua sisi wananchi..
Itachukua miaka mingi sana mbele kuja kumpata Rais aina ya John Magufuli, ni ngumu sana.. Mungu tupe macho tuone, wengine wanaangalia demokrasia, sisi tunaangalia maendeleo..