Kwanini Marais huongezewa muda?

Ndata

JF-Expert Member
Mar 2, 2017
226
321
Kumeibuka kundi kubwa la wazalendo wa nchi hii kutaka ukomo wa madaraka uondolewe kwenye katiba yetu ili kuruhusu Magufuli aongoze kwa awamu tatu au nne zaidi.

Hili sio jambo geni duniani. Hata Marekani wamewahi kufanya hivi mwaka 1940 Roosevelt alipochaguliwa kuongoza kwa awamu ya tatu na 1944 aliporuhusiwa kugombea kwa awamu ya nne bahati mbaya akafariki. Baada yake mfumo huo uliondolewa.

Sababu za kuongezewa muda ni zilezile tunazoziongelea Tanzania, Magufuli ni mfano wa viongozi aina ya Mao wa China, Nyerere wa Tanzania na Roosevelt wa Marekani. Hawa ni wajenga nchi.

Viongozi aina hii huchukua Muda kupatikana, ndio maana baada ya Mao wa China kiongozi mwingine wa aina yake ni huyu kapatikana kizazi chetu hichi na tunaona wachina wamemuondolea kabisa ukomo wa uongozi.

Tanzania baada ya Nyerere wamepita viongozi watatu hadi kuja kumpata mwingine mwenye mawazo, malengo na itakadi kama ya Nyerere, kwanini tusimuongezee muda ilihali Nyerere aliongoza kwa awamu zaidi ya nne kama tukihesabu miaka mitano mitano.

Mfumo wa uchaguzi ubaki kama ulivyo kila baada ya miaka mitano na pale Magufuli atakapochoka au kufariki katiba ibadilishwe kurudi kwenye mfumo tuliozoea hadi pale atakapopatikana mjenga nchi mwingine.

Shauri lililopo mahakamani lililofunguliwa na Mkulima ni shauri la kizalendo na lenye maana kubwa kuliko hoja za wanaompinga.

Wakati hoja kuu ya wapinzani ni Rais kubadilika pale anapogundua kaondolewa ukomo suala la uchaguzi kila baada ya miaka mitano nadhani linaweza imaliza hoja yao kabisa. Kama hawana imani na tume ya uchaguzi hio ni issue tofauti sana na kilio chetu wazalendo cha Magufuli kuondolewa term limit kwa faida ya nchi hii.

Ombi kwa wazalendo wengine wengi huu ni muda wa kuungana na Mkulima kimawazo, ushauri na kumuwezesha pale anapikwama ili asije akashindwa kwa vitu vidogo ambavyo tungeweza kuchangia.

Cwu.
 
China sasa hivi wapo kwenye mchakato wa kubadili katiba Xi Jinping aongezewe muda ngoja sasa pro Magu walisikie hili kwao ndio itakuwa kama vile ni uhalali na jamaa wao aongezewe muda.

Wakati hao watu wawili ukiwalinganisha ni kama mbingu na ardhi.
 
Ili ilweje mbona kuna viongozi wengi saana walio tamani kuendelea lakini hawajaruhusu jambo hilo litokee? Na kama litatokea ni bora na maraisi wastaafu warudi tena ili iwe raisi na kwao kujaribu tena bahati yao
 
Wachina Walifanya na wanafanya (Mao na Huyu wa sasa)

Wamarekani walifanya (Rooservert)

Chadema wanafanya (mwenyekiti wao mjenga chama hawajambadilisha mwaka wa ngapi sijui sasa)


Sis ni nani?
 
Ili ilweje mbona kuna viongozi wengi saana walio tamani kuendelea lakini hawajaruhusu jambo hilo litokee? Na kama litatokea ni bora na maraisi wastaafu warudi tena ili iwe raisi na kwao kujaribu tena bahati yao
Wananchi ndo wanaamua
Kama vipi ipigwe kura ya wananchi wanataka nini

Magu aruhusiwe kuendelea
 
Haya anayoyafanya Magufuli kila mtu anaweza kuyafanya, na sio kuyafanya tu, hata demokrasia ataiiheshumu. Huko ccm watu wanaoweza kuyafanya haya ni wachache, sasa tatizo la ccm isiwe ni Tatizo la nchi nzima. Kiongozi mzuri huheshimu njia ya kukaa madarakani kihalali, lakini ukishaona kiongozi anakaa madarakani kwa kufubaza mifumo na kisha yeye kujigeuza ndio mfumo huyo ni mlevi wa madaraka kama walevi wengine. Huko ccm anaweza kuwa hata mwenyekiti wa maisha, na huo uwezo wake baada ya miaka 10, atauweka kwenye ilani ya chama chake utekelezwe. Ila mwisho ni miaka 10 fullstop.
 
Acheni mambo ya kijinga! Mtakuja kuliingiza hili Taifa kwenye machafuko yasiyo na kichwa wala miguu. Leo hii ndugu yenu Nkurunzinza wa Burundi anashindwa hata kutoka nje tu ya ikulu yake kwa hofu ya kupinduliwa.

Sababu ni moja tu; Kujiongezea muda wa kuitawala Burundi kimabavu na wakati muda wake ulishakwisha kikatiba. Hivyo basi, huyo mtu wenu kama mnamuona anawafaa sana, basi mpeni hadhi ya kuwa rais wa maisha wa familia zenu! Ila kwa mustakabari wa amani ya nchi yetu, tunaomba katiba yetu iheshimiwe.
 
Naona mmeanza kampeni mapema wakati ata awamu ya kwanza haijakwisha , tusubiri 2024 kelele za hii mambo zitakuwa mingi

Yeye afanye mambo yake katika awamu yake ..na wengine wapewe kuongoza
 
China sasa hivi wapo kwenye mchakato wa kubadili katiba Xi Jinping aongezewe muda ngoja sasa pro Magu walisikie hili kwao ndio itakuwa kama vile ni uhalali na jamaa wao aongezewe muda.

Wakati hao watu wawili ukiwalinganisha ni kama mbingu na ardhi.
Mkuu mbona katiba ya China ina zaidi ya miaka tangu imebadilishwa ili Xi awe rais wa maisha?
 
Haya anayoyafanya Magufuli kila mtu anaweza kuyafanya, na sio kuyafanya tu, hata demokrasia ataiiheshumu. Huko ccm watu wanaoweza kuyafanya haya ni wachache, sasa tatizo la ccm isiwe ni Tatizo la nchi nzima. Kiongozi mzuri huheshimu njia ya kukaa madarakani kihalali, lakini ukishaona kiongozi anakaa madarakani kwa kufubaza mifumo na kisha yeye kujigeuza ndio mfumo huyo ni mlevi wa madaraka kama walevi wengine. Huko ccm anaweza kuwa hata mwenyekiti wa maisha, na huo uwezo wake baada ya miaka 10, atauweka kwenye ilani ya chama chake utekelezwe. Ila mwisho ni miaka 10 fullstop.
Aliyekwambia miaka kumi NI Haki ya kizaliwa ni nani.? Hii mifumo imewekwa na watu na inaweza kubadilishwa wakati wowote watu hao hao wakiamua. Fullstop
 
Sbb kubwa wazalendo wanataka Mh. JPM aongezewe muda si kingine bali ni speed kubwa ya maendeleo ya wazi kabisa, yaani maendeleo huhitaji kuelezewa, unaona kwa macho yako kwa muda mfupi sana, pia kawafuta kabisa majambazi, wezi, wala rushwa, mafisadi, watumishi hewa na wenye vyeti feki, uzembe na uvivu serikalini, wazungu wezi wa rasilimali za nchi yetu wamekubali kulipa share deal kwa serikali kwa kila sekta iwe madini, simu, utalii, etc..

Ni mengi mengii mengiiii makuu Mh. JPM kayafanya kwa speed ya ajabu, wakati mwingine nashangaa haya yanawezekana vipi? Kama siamini, ila naona kwa macho yangu, najisemea Eeh Mungu, huyu Rais wa sasa kwanini asikae walau hata miaka yote hadi akatae au apewe na wananchi hata miaka 20 tu dunia nzima itashangaa kwa hatua kubwa tutakayo piga ya maendeleo, China mwaka huu imempa Xi aongozee China bila kuwa na kikomo, yote sbb ya maendeleo ya haraka sana hadi US wanawaheshimu na wanaogopa sana China.. Sisi watanzania ni uamuzi wetu sasa tuamue, Katiba ni yetu, katiba sio Biblia au Quran, tunaweza kuamua sisi wananchi..

Itachukua miaka mingi sana mbele kuja kumpata Rais aina ya John Magufuli, ni ngumu sana.. Mungu tupe macho tuone, wengine wanaangalia demokrasia, sisi tunaangalia maendeleo..
 
Kwa nini hoja hii inakuja kwa kasi ktk kipindi ambacho Rais hajamaliza hata miaka yake mitano ya uongozi wake? Kitu gani kinachohamasisha hivi sasa na kutufanya kupoteza uvumilivu wa kusubiri mwaka mmoja uliobaki ili tufike 2020 twende kwenye uchaguzi mwingine?

Kama mambo mazuri ya kupigiwa mfano yamefanyika, si chema kitajiuza na kibaya kujitembeza? Mbona Watanzania tunataka kuiingiza nchi yetu ktk mgogoro wa kikatiba usiokuwa na maana? Mimi nahisi hoja hii ingalikuja 2024 pengine ingeweza kuwa na mashiko, kwa kuwa tungalikuwa na uwanja mpana wa kufanya tathimini ya kina.
 
Haya anayoyafanya Magufuli kila mtu anaweza kuyafanya, na sio kuyafanya tu, hata demokrasia ataiiheshumu. Huko ccm watu wanaoweza kuyafanya haya ni wachache, sasa tatizo la ccm isiwe ni Tatizo la nchi nzima. Kiongozi mzuri huheshimu njia ya kukaa madarakani kihalali, lakini ukishaona kiongozi anakaa madarakani kwa kufubaza mifumo na kisha yeye kujigeuza ndio mfumo huyo ni mlevi wa madaraka kama walevi wengine. Huko ccm anaweza kuwa hata mwenyekiti wa maisha, na huo uwezo wake baada ya miaka 10, atauweka kwenye ilani ya chama chake utekelezwe. Ila mwisho ni miaka 10 fullstop.
Unaweza kuwa sahihi shida hatujaona mpaka Leo baada ya nyerere rais wa pili ni Magufuli wengine nadhan walikuwa viongozi wakuu wa nchi
 
Kumeibuka kundi kubwa la wazalendo wa nchi hii kutaka ukomo wa madaraka uondolewe kwenye katiba yetu ili kuruhusu Magufuli aongoze kwa awamu tatu au nne zaidi.

Hili sio jambo geni duniani. Hata Marekani wamewahi kufanya hivi mwaka 1940 Roosevelt alipochaguliwa kuongoza kwa awamu ya tatu na 1944 aliporuhusiwa kugombea kwa awamu ya nne bahati mbaya akafariki. Baada yake mfumo huo uliondolewa.

Sababu za kuongezewa muda ni zilezile tunazoziongelea Tanzania, Magufuli ni mfano wa viongozi aina ya Mao wa China, Nyerere wa Tanzania na Roosevelt wa Marekani. Hawa ni wajenga nchi.

Viongozi aina hii huchukua Muda kupatikana, ndio maana baada ya Mao wa China kiongozi mwingine wa aina yake ni huyu kapatikana kizazi chetu hichi na tunaona wachina wamemuondolea kabisa ukomo wa uongozi.

Tanzania baada ya Nyerere wamepita viongozi watatu hadi kuja kumpata mwingine mwenye mawazo, malengo na itakadi kama ya Nyerere, kwanini tusimuongezee muda ilihali Nyerere aliongoza kwa awamu zaidi ya nne kama tukihesabu miaka mitano mitano.

Mfumo wa uchaguzi ubaki kama ulivyo kila baada ya miaka mitano na pale Magufuli atakapochoka au kufariki katiba ibadilishwe kurudi kwenye mfumo tuliozoea hadi pale atakapopatikana mjenga nchi mwingine.

Shauri lililopo mahakamani lililofunguliwa na Mkulima ni shauri la kizalendo na lenye maana kubwa kuliko hoja za wanaompinga.

Wakati hoja kuu ya wapinzani ni Rais kubadilika pale anapogundua kaondolewa ukomo suala la uchaguzi kila baada ya miaka mitano nadhani linaweza imaliza hoja yao kabisa. Kama hawana imani na tume ya uchaguzi hio ni issue tofauti sana na kilio chetu wazalendo cha Magufuli kuondolewa term limit kwa faida ya nchi hii.

Ombi kwa wazalendo wengine wengi huu ni muda wa kuungana na Mkulima kimawazo, ushauri na kumuwezesha pale anapikwama ili asije akashindwa kwa vitu vidogo ambavyo tungeweza kuchangia.

Cwu.
Acheni ujinga nani anamawazo, malengo na maono kama Nyerere?

Huyu asieweza hata kujieleza kwa kiswahili?
Huyu anayependelelea kwao hadi amehamishia mbuga ya wanyama na kujenga uwanja Wa Ndege Wa kimataifa kwao? Nyerere alikuwa hivi?

Huyu anaegopa watu kuhoji? Anaishia kuwavurumishia mvua ya risasi!

Ukweli ni huu nchi hii haijawahi kuwa na kiongozi mbovu na muovu kama huyu! Tuondoleeni mashudu yenu hapa!!
 
Back
Top Bottom