Kwanini Makonda asifunguliwe kesi ya msingi Mahakamani?

EWGM's

JF-Expert Member
Jul 22, 2013
1,521
2,109
Nimefatilia Hili Saga La Bwana Mkubwa Makonda Kwa Muda Sasa Na Kila Kukicha Mambo Mapya Yanaibuka Kuhusu Yeye. Paul Makonda Ana Nia Safi Ya Kulisafisha Jiji Kuhusiana Na Madawa Ya Kulevya Lakini Taratibu Na Njia Sahihi Lazima Zifuatwe.

Amesema Anatumia Vyombo Vya Habari Ili Hata Mtoto Mdogo Wa Shule Msingi Ajue Kuwa Madawa Ya Kulevya Ni Hatari Na Wahusika Wake. Hivyo Wajiepushe Nayo Kwani Na Wao Wakishiriki Kwa Namna Moja Au Nyingine Wajue Hathari Zake Ikiwemo Kutajwa Hadharani.

Kwakusema Hivyo Ina Maana Aliowataja Kwenye Vyombo Vya Habari Kwa Namna Moja Au Nyingine Wanahusika Na Madawa Ya Kulevya. Hapo Juu Nimenukuhu Moja Ya Sababu Alizosema Makonda Kwanini Ametaja Majina Hadharani. Lakini Kwenye Kutaja Watu Lazima Uwe Na Ushahidi Na Uhakika Wa Uhusika Wao Mbadala Na Kutoa Kauli Mbili Zinazokinzana.

Pia Akaja Kusema "Aliowaita" Wakutane Na Wewe Pale Central Polisi Kwa Kamanda Siro Ili Mzungumze. Sasa Bwana Mkubwa Makonda Hapa Ndipo Ninapopata Kujiuliza Maswali. Kama Uliowaita Wanahusika Na Madawa Ya Kulevya Na Kuwatangaza Hadharani, Kwanini Usikabidhi Majina Yao Kwa IGP Au Kamanda Siro Ili Karatibu Za Kipolisi Zifuatwe, Na Mwisho Sheria Ichukue Mkondo Wake?

La Pili Kwanini Unataoa Kauli Zinazokinzana Kuhusiana Na Majina Unayoyataja? Kwa Mfano Umesema Umewataja Ili Hata Watoto Wa Shule (Jamii) Ijue Uhusika Wao Na Hapo Hapo Unasema Umewaita Ili Watoe Ushirikiano Na Kujua Ukweli Kutoka Upande Wao Kwa Shutuma Za Madawa Ya Kulevya?

Kimsingi Sitapenda Kuongelea Hadhi, Nyadhifa, Majina Yao Au Umuhimu Wa Majina Yao Kwa Jamii Na Kwa Familia Zao Sababu Haya Waziri Nape Aliyaelezea Kwa Ufasaha Kabisa Na Pia Havitazuia Uhalifu Wao Kama Kweli Walitenda.

Kwenye Hitimisho Ambako Kuna Hoja yangu Na Swali La Msingi Ni Kuwa Nchi Hii Inaendeshwa Kwa Kufuata Katiba, Kanuni na Sheria Za Nchi. Pia Hakuna Aliyejuu Ya Sheria na Katiba Za Nchi Na Hata Ukiwa Na Madaraka Kuna Maadili Na Kanuni Za Uongozi Lazima Zifuatwe Ili Kukuwezesha Kiongozi Kuheshimu Katiba, Sheria Na Kanuni Za Nchi Tulizojiwekea.

Tanganyika Law Society, Amnesty International, Tanzania & Zanzibar Human Rights Watch, Wanasheria Wa Kujitolea Kwa Wamekuwa Kimya Sana Kwenye Hili Swali La Msingi:

'Ni Kwa Mamlaka Yapi Na Kifungu Kipi Cha Sheria Kinachokumpa Ruhusa Mkuu Wa Mkoa Aite Watu Polisi Kutumia Vyombo Vya Habari? '
 
Matangazo ya ukimwi yalianza kutangazwa lini? Leo hii wananchi wangapi ni waathirika? Siwezi kushangaa maana hata baba alibadilisha hotuba ya marehemu


Amesema Anatumia Vyombo Vya Habari Ili Hata Mtoto Mdogo Wa Shule Msingi Ajue Kuwa Madawa Ya Kulevya Ni Hatari Na Wahusika Wake. Hivyo Wajiepushe Nayo Kwani Na Wao Wakishiriki Kwa Namna Moja Au Nyingine Wajue Hathari Zake Ikiwemo Kutajwa Hadharani."
 
Nchi hii watu fulani wakiguswa tu,wanakumbuka utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Listi ya mafisadi iliimbwa miaka 8,hatukusikia wanakumbusha kuhusu utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Muacheni Makonda afanye kazi,mwenye kuona kaonewa aende mahakamni akadai kusafishwa,mbona sheria zipo wazi kabisa
 
Ni wapi kaandika vibaya? Huo ni utaratibu tu wa ku-format text
Utaratibu wa wapi Mkavu? Kila neno katika sentensi unaanza na herufi kubwa mpaka kiunganishi nacho kinaanza na herufi kubwa? Nyie ndio mnampa kiki faizafoxy kwa ujinga kama huo!
 
Ni wapi kaandika vibaya? Huo ni utaratibu tu wa ku-format text

Ndugu Yangu Wala Usibishane Nao Sababu Zinajulikana Mtu Mweusi Ili Kumfichia Kitu Kiweke Kwenye Maandishi Kwisha kazi​
 
Nchi hii watu fulani wakiguswa tu,wanakumbuka utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Listi ya mafisadi iliimbwa miaka 8,hatukusikia wanakumbusha kuhusu utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Muacheni Makonda afanye kazi,mwenye kuona kaonewa aende mahakamni akadai kusafishwa,mbona sheria zipo wazi kabisa


Kwa Hiyo Hii Ndiyo Ile List Ya Miaka 8 Ya Raisi Kikwete Ya Wauza Madawa Ya Kulevya Papa?

Kwanza Uzi Hauzungumzii List Unazungumzia Katiba na Sheria Za Nchi Zinamruhusu Makonda Kuita Watu Polisi?
 
Nchi hii watu fulani wakiguswa tu,wanakumbuka utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Listi ya mafisadi iliimbwa miaka 8,hatukusikia wanakumbusha kuhusu utaratibu,sheria na katiba ya nchi.
Muacheni Makonda afanye kazi,mwenye kuona kaonewa aende mahakamni akadai kusafishwa,mbona sheria zipo wazi kabisa
List of Shame umewahi kuisoma ama unaisikia tu kwenye midahalo ya kwenye vijiwe vya kahawa!? Pale wote waliotajwa waliwekewa na ushahidi wao na wale walioitaja List Of Shame hawakuwa na serikali. Hoja hapa kama umekabidhiwa dhamana ya kuongoza serikali hutakiwi uwe unalalamika kama asiye na serikali. Duniani kote "Scandals" huanzishwa na walio nje ya serikali na si na walio ndani ya serikali.
 
List of Shame umewahi kuisoma ama unaisikia tu kwenye midahalo ya kwenye vijiwe vya kahawa!? Pale wote waliotajwa waliwekewa na ushahidi wao na wale walioitaja List Of Shame hawakuwa na serikali. Hoja hapa kama umekabidhiwa dhamana ya kuongoza serikali hutakiwi uwe unalalamika kama asiye na serikali. Duniani kote "Scandals" huanzishwa na walio nje ya serikali na si na walio ndani ya serikali.
Hahaaaa hamkawii kuremba.Unataka tuamini mawazo yako.huo ushahidi ni wa kwako na makamanda wenzako.
Alichofanya Mbowe ndio kinamrudia,Makonda akisema ana ushahidi atakuwa na tofauti gani na mBowe aliedai lowasa fisadi hasafishiki?Mwambie mwenyekiti wenu atii amri,au anaogopa kulala leo hadi jumatatu?
 
Natamani manji aende,


Hili Lilikuwa Swali La Msingi Kabisa Nilitegemea Vyombo Vinavyohusika Viulize Hiki Kitu Lakini Viko Kimya

Kipindi Kama Hiki Ndicho Namkumbuka Mtikila Alikuwa Anaisimamia Serikali Ifate Mstali
 
Back
Top Bottom