EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Pamoja na jitihada anazofanya Makonda kuonyesha anaendana na kasi ya Magufuli, kwa kuwaweka ndani mara kwa mara viongozi wa wananchi wakiwemo wafanyakazi wa Ardhi Kinondoni na mbunge wa Ubungo, kuupa deadline utawala wa Urafiki na jitihada zingine, lakini sijaona wala kumsikia rais akimpongeza tofauti na Kikwete aliyekuwa akimpongeza mara kwa mara hadi kufikia hatua ya kumteua kuwa mkuu wa wilaya baada ya kuonyesha uwezo wa kumdhibiti mzee Warioba.
Ina maana rais Magufuli hazioni juhudi za Makonda au anazipuuza?
Ina maana rais Magufuli hazioni juhudi za Makonda au anazipuuza?