Kwanini mabinti wa Arusha wanashobokea wazungu??

Kwanini mabinti wa Arusha wanashobokea wazungu??

thebigbobo

Senior Member
Joined
Sep 25, 2014
Posts
168
Reaction score
17
Maisha ya Arusha ni tofauti na mikoa niliyotoka! Siku ya tatu baada ya kukanyaga ardhi ya Arusha nilishangaa kuona idadi kubwa ya wadada ni warembo sana,
Nikajua si muda nami nitapata mmoja basi kuna siku niliamua kwenda kiwanja maarufu VIA VIA nikakutana na mrembo mmoja! Anaitwa Anna. Tukaongea sana tukanywa tukabadilishana na namba za simu! Sasa nikabanwa na mkojo nikaenda chooni nikarudi nikakuta kabambiwa na Muzungu, nilivyomfata akaniambia nimtafute kesho yake. Mimi nikakasirika nikaenda kulala.
Asubuhi saa mbili akanipigia tuonane. Mimi nikajipiga moyo konde. Akapanga tuonane ICC, nilivyofika ICC kwa boda boda akanipokea tungaingia kwenye gari yake discovery 3. Mpaka palace hotel tukaongea sana. Anaonekana anamiaka 24 hivi kiumbo but akaniambia anamiaka 30 na ana watoto wawili machotara kila mtu na baba yake na kwasasa ameachana nao wote wawili. Na amejikubali kuishi kama single parent lakini tatizo kwa sasa anatamani kuolewa na kama nipo tayari niwemume wake wa ndoa.
Kwakweli mimi niligoma kabisa kwasababu alishobokea mzungu kwanza na mimi akaniweka chaguo la pili! Wewe ungekubali?
 
Mjanja wa mjini huyo, bora ulivyoshtuka
 
Mbona rahic tu mkuu fanya fanya nawe akuzaliee angalau mtt mmoja azidi kujaza watoto.kuoa usioe huyo yupo kimaslahi zaidi ya manji yanga
 
Mbona unaconclude mambo kana kwama umefanya utafiti kamilifu ili hali hujafanya hivyo ?

kwa hiyo kesho ukikuta huyo binti yupo na msanii utasema mabinti wa Arusha wanashobokea wasanii....mtondogoo utasema wanashobokea waendesha bodaboda.
 
Ukimuoa hao watoto wake ukiongozana nao utaonekana house boy
 
Back
Top Bottom