Kituko
JF-Expert Member
- Jan 12, 2009
- 9,555
- 9,330
Najaribu Kuangalia kiundani, ni sababu gani kubwa ya Lowasa na wenzie kuzalilishwa na chama chao, huku mwenyekiti wake ambaye pia ni swahiba wake mkubwa akiwa kimya?, nasema kuzalilishwa na chama chake (nje ya CCM ni hatua iliyopaswa kufanywa na hata vyombo vya sheria vilipaswa kumshtaki/kuwashitaki),
Lowasa alitumia nguvu nyingi binafsi kumuweka mwenyekiti wa CCM kwenye uongozi wa nchi, lakini sasa inakuwaje MWENYEKITI ANASHINDWA KUMTETEA? Na kama ni UFISADI basi hata JK mwenyewe yumo kundini, lakini kwa nini Lowassa
nikijaribu kupambanua napata hoja moja tu URAIS WA 2015,
Nadhani katika historia ya CCM uchaguzi wa 2015 utakuwa ni uchaguzi ambao haujawahi kutokea, ni uchaguzi ambao unaweza kukiua kabisa CCM
Mpaka sasa naona kuna wagombea sita ambao wana nguvu kubwa ndani ya CCM na ambao wameshaanza Kampeni za kichinichini na za kwenye public kutafuta popurarity
1) Lowassa
2) Membe
3) Hussein Mwinyi
4) Mark Mwandosya
5) Fredirick Sumaye na
6) Asharose Migiro
6: Migiro
Hana Influencial sana labda ataingia kwenye mchakato na kupata nguvu kwa sababu ya Jinsia
5: Sumaye
Kambi yao kwa muda mrefu imekuwa ikidhoofishwa na sasa wamejipanga/wanajipanga ili waweze kurudi na Sumaye ndio anaonekana kuwa ni potential akitegemea nguvu za Mkapa, Mramba, Apson nk, japokuwa haonekani kama yupo imara lakini kwa ndani/chinichini yupo kwenye kampeni nzito
4: Mwandosya
Kwa muda mrefu amekuwa akitamani kuingia Magogoni lakini ameonekana kuwa hana Mvuto sana na kwa kweli alikuwa ameshapoteza kutokana na siasa za kutengwa (Kupewa wizara zisizo na kelele za kupata popularity), Lakini kwa Uchaguzi uliopita na siasa za mbeya zilivyo, Mwandosya ndio anaonekana kuwa ni miongoni mwa watu muhimu katika kukijenga chama Mbeya na kiukweli Mwandosya-akiwa na Mboma anajitahidi sana kurudi kwenye chati ili ifikapo 2015 awe na sauti ndani ya NEC
3: Hussein Mwinyi
Alikuwa Mbunge Tanzania Bara, swali la kujiuliza imekuwaje aende kugombea Zanzibar, lakini kiukweli huo ulikuwa ni mpango madhubuti wa CCM na labda UWT, kama Kelele za wazanzibar zikiwa Raisi wa 2015 ni lazima atoke Zanzibar basi Hussein Mwinyi atakuwa ndio Chaguo la CCM, kwa hiyo yeye yupo hapo kama spare tyre tu
2: Membe
Kwa Mtazamo wangu Nadhani huyu ndio chaguo la ****** na labda UWT, nina sababu lakini nitaziweka baadae
1: Lowassa
Nadhani kila mtu anamzungumzia huyu Bwana, na yeye mwenyewe alishajiweka kwenye hiyo class ya Presidential Material, Nyendo zake, nguvu zake na hata kampeni zake zilikuwa zinaelekeza hivyo, amejenga nguvu kubwa ndani ya CCM na labda serikalini pia,
Swali Linabaki kwa nini CCM wanamtoa Lowassa sadaka kama ndio mwenye nguvu kuliko wote tunaowategemea kutoka CCM?
Kwa mtazamo wangu Lowassa sio Chaguo la ****** na wala UWT (japo ni maswahiba wakubwa), Kwa mambo JK aliyofanyiwa na Lowassa kuanzia 1995 na mpaka anaupata urais kwake ni vigumu sana kumtosa Lowassa akiwa macho makavu, njia pekee ni hii iliyotumiwa sasa ya kupitia Chamani-NEC na ili kumtolea uwezo wake alionao ndani ya NEC basi ilipasa wamtoe kwa nguvu, na kwa sababu Lowassa ana nguvu ya RA na Visenti basi ilibidi wote watolewe ndani ya chama (kwa gia ya ufisadi) ili asiwe (Lowassa) na uwezo wa kufurukuta 2015,
Ni mtizamo wangu tu
Lowasa alitumia nguvu nyingi binafsi kumuweka mwenyekiti wa CCM kwenye uongozi wa nchi, lakini sasa inakuwaje MWENYEKITI ANASHINDWA KUMTETEA? Na kama ni UFISADI basi hata JK mwenyewe yumo kundini, lakini kwa nini Lowassa
nikijaribu kupambanua napata hoja moja tu URAIS WA 2015,
Nadhani katika historia ya CCM uchaguzi wa 2015 utakuwa ni uchaguzi ambao haujawahi kutokea, ni uchaguzi ambao unaweza kukiua kabisa CCM
Mpaka sasa naona kuna wagombea sita ambao wana nguvu kubwa ndani ya CCM na ambao wameshaanza Kampeni za kichinichini na za kwenye public kutafuta popurarity
1) Lowassa
2) Membe
3) Hussein Mwinyi
4) Mark Mwandosya
5) Fredirick Sumaye na
6) Asharose Migiro
6: Migiro
Hana Influencial sana labda ataingia kwenye mchakato na kupata nguvu kwa sababu ya Jinsia
5: Sumaye
Kambi yao kwa muda mrefu imekuwa ikidhoofishwa na sasa wamejipanga/wanajipanga ili waweze kurudi na Sumaye ndio anaonekana kuwa ni potential akitegemea nguvu za Mkapa, Mramba, Apson nk, japokuwa haonekani kama yupo imara lakini kwa ndani/chinichini yupo kwenye kampeni nzito
4: Mwandosya
Kwa muda mrefu amekuwa akitamani kuingia Magogoni lakini ameonekana kuwa hana Mvuto sana na kwa kweli alikuwa ameshapoteza kutokana na siasa za kutengwa (Kupewa wizara zisizo na kelele za kupata popularity), Lakini kwa Uchaguzi uliopita na siasa za mbeya zilivyo, Mwandosya ndio anaonekana kuwa ni miongoni mwa watu muhimu katika kukijenga chama Mbeya na kiukweli Mwandosya-akiwa na Mboma anajitahidi sana kurudi kwenye chati ili ifikapo 2015 awe na sauti ndani ya NEC
3: Hussein Mwinyi
Alikuwa Mbunge Tanzania Bara, swali la kujiuliza imekuwaje aende kugombea Zanzibar, lakini kiukweli huo ulikuwa ni mpango madhubuti wa CCM na labda UWT, kama Kelele za wazanzibar zikiwa Raisi wa 2015 ni lazima atoke Zanzibar basi Hussein Mwinyi atakuwa ndio Chaguo la CCM, kwa hiyo yeye yupo hapo kama spare tyre tu
2: Membe
Kwa Mtazamo wangu Nadhani huyu ndio chaguo la ****** na labda UWT, nina sababu lakini nitaziweka baadae
1: Lowassa
Nadhani kila mtu anamzungumzia huyu Bwana, na yeye mwenyewe alishajiweka kwenye hiyo class ya Presidential Material, Nyendo zake, nguvu zake na hata kampeni zake zilikuwa zinaelekeza hivyo, amejenga nguvu kubwa ndani ya CCM na labda serikalini pia,
Swali Linabaki kwa nini CCM wanamtoa Lowassa sadaka kama ndio mwenye nguvu kuliko wote tunaowategemea kutoka CCM?
Kwa mtazamo wangu Lowassa sio Chaguo la ****** na wala UWT (japo ni maswahiba wakubwa), Kwa mambo JK aliyofanyiwa na Lowassa kuanzia 1995 na mpaka anaupata urais kwake ni vigumu sana kumtosa Lowassa akiwa macho makavu, njia pekee ni hii iliyotumiwa sasa ya kupitia Chamani-NEC na ili kumtolea uwezo wake alionao ndani ya NEC basi ilipasa wamtoe kwa nguvu, na kwa sababu Lowassa ana nguvu ya RA na Visenti basi ilibidi wote watolewe ndani ya chama (kwa gia ya ufisadi) ili asiwe (Lowassa) na uwezo wa kufurukuta 2015,
Ni mtizamo wangu tu