Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Watanzania kwa pamoja tumekubaliana kwamba kutokana na majukumu makubwa waliyonayo Viongozi na watendaji waandamizi serikalini, ambayo yanahitaji akili iliyotulia, kuna umuimu mkubwa kutumia rasilimali kidogo tuliyo nayo ili kuhakikisha watu hao wanaishi peponi; hata kama kwa kufanya hivyo italazimu wananchi wa kawaida/wadogo waishi kwa kula majani. Wabunge wetu wako katika kundi hilo adimu. Kinachonishangaza, ni kwanini wabunge hao wamepewa shs.90 milioni tu kwaajili ya kununua gari, wakati magari iliyopewa mihimili mingine ya dola yana thamani ya shs. 200 milioni na kuendelea!