Kwanini kwaya,mapadri na maaskofu wa Katoliki hawapo ktk safari ya matumaini kuunga mkono?

Jumong S

JF-Expert Member
Jul 3, 2013
7,312
10,494
Nimeangalia tangu ile series ya mh Lowasa kutembelewa na wachungaji, mashehe na watu mbali mbali kushawishiwa kugombea urais sikuwaona hawa maparokia wakijiunga na safari ya matumaini. Nikaangalia pale Karume kwenye ufunguzi wa kutia nia sikuwaona maparoko au maaskofu wa Kikatoliki wakijitokeza waziwazi kumuunga mkonyo mheshimiwa. Je, hawa wapendwa tuseme hawapo ktk ile safari ya matumaini?

KWAYA
Imejitokeza tabia ya wasanii wa nyimbo za injili kuwaimbia watia nia na kuwanadi. Alianza Bahati Bukuku, niliyemheshimu kuanza kumuimbia Mh Lowasa huku akimfananisha na Mfalme Suleiman. Kabla, sijaishiwa mshangao nimeshuhudia Rose Mhando, Matha Mwaipaja, Njole, Bon Mwaitege na mama wa maadili nimpendae Upendo Nkone wakiimba eti wana imani na Mwigulu Nchemba. Hapa nikaona kweli injili inatumika kupiga mihela na hawa wanaotuimbia daima injili. Hawana tofauti na Diamond au Linux au Kiba au Mzee Yusufu.

Cha ajabu hawa wakatoliki na kwaya zao siwaoni wakimuimbia au kumnadi mtia nia wa CCM au UKAWA. Sasa najiuliza, wenyewe tuwaweke kundi gani?
 
Nimeangalia tangu ile series ya mh Lowasa kutembelewa na wachungaji, mashehe na watu mbali mbali kushawishiwa kugombea urais sikuwaona hawa maparokia wakijiunga na safari ya matumaini. Nikaangalia pale Karume kwenye ufunguzi wa kutia nia sikuwaona maparoko au maaskofu wa Kikatoliki wakijitokeza waziwazi kumuunga mkonyo mheshimiwa. Je, hawa wapendwa tuseme hawapo ktk ile safari ya matumaini?

KWAYA
Imejitokeza tabia ya wasanii wa nyimbo za injili kuwaimbia watia nia na kuwanadi. Alianza Bahati Bukuku, niliyemheshimu kuanza kumuimbia Mh Lowasa huku akimfananisha na Mfalme Suleiman. Kabla, sijaishiwa mshangao nimeshuhudia Rose Mhando, Matha Mwaipaja, Njole, Bon Mwaitege na mama wa maadili nimpendae Upendo Nkone wakiimba eti wana imani na Mwigulu Nchemba. Hapa nikaona kweli injili inatumika kupiga mihela na hawa wanaotuimbia daima injili. Hawana tofauti na Diamond au Linux au Kiba au Mzee Yusufu.

Cha ajabu hawa wakatoliki na kwaya zao siwaoni wakimuimbia au kumnadi mtia nia wa CCM au UKAWA. Sasa najiuliza, wenyewe tuwaweke kundi gani?

Wakatoliki Huwa Hatuna Muda Mchafu Kama Huo Wa Kujipendekeza Kwani Tuna Mambo Mengi Sana Ya Kufanya Na Hatuamini Ktk Matumaini Bali Tunaamini Ktk Reality. Kusema " Safari Ya Matumaini " Ina Maana Unaishi Kwa Probability Na Mkristo Wa Kweli Hasa Wa Kikatoliki Huwa Anajiamini Kwa Chochote Na Lolote Na Kuwafananisha Hao Viongozi Wa Katoliki Na Wengine Uliowataja Ni Sawa Na Kufananisha Utajiri Mkubwa Wa Kidunia Wa Carlos Slim Na Tajiri Wa Mikoa 29 Tu Ya Tanzania Mzee Kijana Reginald Mengi.
 
Mmmh, kazi iko. Au watia nia hawajapenyeza shekeli huko? Nawashangaa wachungaji wetu hata hawakemei. Yaani kama Gwajima ye ukimpelekea kesi hii hakawii kukwambia ukale malimao
 
Mkuu sio ukweli .Mh Rowasa alikuwa mkoan kagera maneno aliyoyasema Askofu mkuu wa jimbo la Rulenge Ngara yanadhihirisha uwepo wa ukatoliki katika safari ya matumaini
 
Mkuu sio ukweli .Mh Rowasa alikuwa mkoan kagera maneno aliyoyasema Askofu mkuu wa jimbo la Rulenge Ngara yanadhihirisha uwepo wa ukatoliki katika safari ya matumaini

Issue ni kujionesha wazi wazi majukwaani, kuwaimbia, akina Gwajima na Wachungaji wengi walitoa hata maombi kuibariki safari ya matumaini. Hakuna Theologian Wa Kikatoliki alofanya hivyo hadi sasa.
 
Wakatoliki Huwa Hatuna Muda Mchafu Kama Huo Wa Kujipendekeza Kwani Tuna Mambo Mengi Sana Ya Kufanya Na Hatuamini Ktk Matumaini Bali Tunaamini Ktk Reality. Kusema " Safari Ya Matumaini " Ina Maana Unaishi Kwa Probability Na Mkristo Wa Kweli Hasa Wa Kikatoliki Huwa Anajiamini Kwa Chochote Na Lolote Na Kuwafananisha Hao Viongozi Wa Katoliki Na Wengine Uliowataja Ni Sawa Na Kufananisha Utajiri Mkubwa Wa Kidunia Wa Carlos Slim Na Tajiri Wa Mikoa 29 Tu Ya Tanzania Mzee Kijana Reginald Mengi.

Colour coding for?
 
Mapadre wengi wana zaidi ya degree moja. Wamepikwa vizuri kichwani, hawawezi kudanganywa na Mwizi, yaani mtu hasie na Moral Authority ya kukemea ufisadi.

Mapadre hawawezi kushadadia mtu alietumikia nchi hii zaidi ya Miaka 30 halafu leo hii aibuke na kusema kuwa atabadilisha nchi hii. Waache hao wachungaji wa ovyo kama akina Gwajima waambatane na Safari ya mafisadi
 
Wakatoliki Huwa Hatuna Muda Mchafu Kama Huo Wa Kujipendekeza Kwani Tuna Mambo Mengi Sana Ya Kufanya Na Hatuamini Ktk Matumaini Bali Tunaamini Ktk Reality. Kusema " Safari Ya Matumaini " Ina Maana Unaishi Kwa Probability Na Mkristo Wa Kweli Hasa Wa Kikatoliki Huwa Anajiamini Kwa Chochote Na Lolote Na Kuwafananisha Hao Viongozi Wa Katoliki Na Wengine Uliowataja Ni Sawa Na Kufananisha Utajiri Mkubwa Wa Kidunia Wa Carlos Slim Na Tajiri Wa Mikoa 29 Tu Ya Tanzania Mzee Kijana Reginald Mengi.

Nilitaka kukubaliana na wewe, ila ulipomtaja Mengi tu, nimerudisha akili yangu tu square zero.......naitafuta post yako nyingine
 
Mkuu sio ukweli .Mh Rowasa alikuwa mkoan kagera maneno aliyoyasema Askofu mkuu wa jimbo la Rulenge Ngara yanadhihirisha uwepo wa ukatoliki katika safari ya matumaini
Umemsahau na Ruzoka wa Tabora. Njaa ni njaa tu, haijui katoliki wala protestant.
 
Njaa ni njaa tu, hauna dini wala kabila. Kuna maaskofu kadhaa wa kikatoliki wako pamoja na Lowassa kwenye safari ya matumani, wapo walionyesha wazi wazi kumuunga mkono(kama kule Tabora, Kagera) wapo wengine hawakuja hadharani.

Jambo la wazi ni kuwa mfumo wa kikatoliki hautoi nafasi kwa mapadri na maaskofu kujichanganya sana na maisha ya kijamii ya watu ikiwemo siasa, viongozi wa kikatoliki wamejengwa kwenye nidhamu ya woga sana, hawako huru sana kuweka hisia zao hadharani, wanaishi kwenye mazingira ya upweke upweke sana hivyo ni vigumu sana kuona wakijichanganya.
Mwisho, Ukatoliki unaongozwa na kusimamiwa na Papa kutoka Vatcan, hivyo mapadri wa kikatoliki wanaweza kuhamishwa na kupelekwa popote kufanya kazi za kikanisa, so it is very risk for them to be involved openly in political game, itakula kwao.

Kuhusu kwaya hilo liko wazi, ni waimbaji binasfi na vikundi vidogo vidogo binafsi vya nyimbo za Injili ndio wamekuwa wakiimba kwenye harakati za wanasiasa, kwa kuwa wanafanya hivyo kwa malipo ya Pesa na wakati mwingine kwa mapenzi yao binafsi, Kwaya hazifanyi hivyo kwa kuwa
nyingi ziko chini ya makanisa, ni kuimba kwa kujitolea na zina watu wengi tofautitofauti hivyo ni complicated procedure kuzipata.
 
Njaa ni njaa tu, hauna dini wala kabila. Kuna maaskofu kadhaa wa kikatoliki wako pamoja na Lowassa kwenye safari ya matumani, wapo walionyesha wazi wazi kumuunga mkono(kama kule Tabora, Kagera) wapo wengine hawakuja hadharani.

Jambo la wazi ni kuwa mfumo wa kikatoliki hautoi nafasi kwa mapadri na maaskofu kujichanganya sana na maisha ya kijamii ya watu ikiwemo siasa, viongozi wa kikatoliki wamejengwa kwenye nidhamu ya woga sana, hawako huru sana kuweka hisia zao hadharani, wanaishi kwenye mazingira ya upweke upweke sana hivyo ni vigumu sana kuona wakijichanganya.
Mwisho, Ukatoliki unaongozwa na kusimamiwa na Papa kutoka Vatcan, hivyo mapadri wa kikatoliki wanaweza kuhamishwa na kupelekwa popote kufanya kazi za kikanisa, so it is very risk for them to be involved openly in political game, itakula kwao.

Kuhusu kwaya hilo liko wazi, ni waimbaji binasfi na vikundi vidogo vidogo binafsi vya nyimbo za Injili ndio wamekuwa wakiimba kwenye harakati za wanasiasa, kwa kuwa wanafanya hivyo kwa malipo ya Pesa na wakati mwingine kwa mapenzi yao binafsi, Kwaya hazifanyi hivyo kwa kuwa
nyingi ziko chini ya makanisa, ni kuimba kwa kujitolea na zina watu wengi tofautitofauti hivyo ni complicated procedure kuzipata.

Nimekuelewa mkuu. Kwa hiyo wakatoliki nao wamo wanaopiga mpunga wa watia nia kimya kimya?
 
Back
Top Bottom