Kwanini kwa wanawake tu na sio wanaume?

Kwanini kwa wanawake tu na sio wanaume?

deebo

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2013
Posts
353
Reaction score
229
Habar za majukum wakuu? Bila kupoteza muda niende kwenye point..

Katika uelewa wangu hua naona wanawake hujengewa iman kua katika maisha yao pamoja na kua na ndoto zao, NDOA ni kama sahani ya kubebea hizo ndoto zao... NDOA kwa wanawake ni swala linalochukuliwa kama bahati tena ina paswa kutokea katika umri flan. Mwanamke akifikisha miaka 27+ hajaolewa inakua kama kadoda hivi, hata saikologia yake haiwi sawa kutokana na misingi ya iman iliopo kwenye jamii kuhusu ndoa na wanawake..

Kwa upande wa sisi wanaume pressure sio kubwa sana juu ya ndoa.. Ni kama chaguo la maamuz kwa wakat tutaopenda sisi.. Watu wanachelewa sana kuoa ila haiwi na uzito kama mwanamke atavyo chelewa kuoa..

Kwann wanaume tusiwe na pressure sawa na wanawake juu ya ndoa? Kwa mtazamo wangu tunge punguza wimbi kubwa la wanawake wanao saka ndoa kwa udi na uvumba.. Ila shida ni kua mwanaume ndoa ni kama option hadi pale mvi zinapo tokea ndo ulazima unaeza anza tokea..

Vipi kama uhitaj wa ndoa ungekua wa kiwango sawa kwa pande zote mbili?

Napenda kuwasilisha, tupate mitazamo yenu wakuu juu ya swala hili..
 
Nadhani sisi wanaume kwakuwa ndio tunamamlaka kubwa ya kuchagua nioe lini na nani
lakin tukija upande wa wanawake hawakupewa mamlaka ya kujipangia aolewe na nani na ni lini so lazima awe na pressure

uihitaji ungekuwa kwa pande zote nafikiri hata sisi wanaume tungekuwa na pressure tukitegemea kwamba daaah umri ukisonga sana ndio basi tena wanawake watanikataa
 
Kuoa vibibi inahitaji moyo, labda uwe mstaafu na mafao yako.
Huwa nawaonea huruma sana wanawake walio kwenye 30s na hawajaolewa, mbaya zaidi unakuta hana hata mtoto. Hata hivyo nina mpango wa kuanza kuwafariji hawa mabibi, nitakuwa nawaoa kwa mkataba.
 
Pale eden baada ya mwanamke kumsikiliza shetani, Mungu alimpa laana 3 mojawapo ni tamaa zake juu ya mwanaume nae atamtawala. Ndo maana mpk leo mwanamke anaona mwanaume ni wa thamani kuliko chochote kwake, bila kujali mwanaume huyo anamtesa yeye bado ataganda hapo.
 
Hiyo haitokei kwa Wanawake ama Wanaume wote.

Ndoa ingawa ni muhimu ila si kila kitu kwa Mwanamke ila kutimiza Ndoto zake.

Mwanamke anaweza asiwe katika ndoa ila akawa msaada tegemezi katika Taifa na Dunia kuliko mwenye Ndoa, ambaye anaweza ishia kuwa goalkeeper ndoani.

Tukiendelea na mtazamo huu inamaana tutakuja kukosa Madaktari wakubwa, Wahandisi na Marubani wabobezi Wanawake.
 
Hiyo haitokei kwa Wanawake ama Wanaume wote.

Ndoa ingawa ni muhimu ila si kila kitu kwa Mwanamke ila kutimiza Ndoto zake.

Mwanamke anaweza asiwe katika ndoa ila akawa msaada tegemezi katika Taifa na Dunia kuliko mwenye Ndoa, ambaye anaweza ishia kuwa goalkeeper ndoani.

Tukiendelea na mtazamo huu inamaana tutakuja kukosa Madaktari wakubwa, Wahandisi na Marubani wabobezi Wanawake.
Nimekupenda bure kabisa......siku zote huwa nakuelewa sana
 
Sio wanawake wote wana Bp yakuolewa mkuu,wengine wana ndoto zao,mimi nilikataa kuolewa wakati nasoma wanaume wanakuja kuleta posa tena wenye Hadhi zao nilikata nikasema nataka kusoma sababu Dad alikua anaona watoto wa kike mzigo na sana alikua ana tumia hela nyingi sana kuwasomesha Kaka zetu shule za ghali sisi watoto wa kike alikua anasema nyie watoto wa kike ni bidhaa mbovu,unamsomesha mtoto unalipa fees nyingi matokeo yake anakujia na mimba mara anataka kuolewa sasa akija mtu kutaka kuoa mnakwendaa, kama kulikua kuna kitu kinaniumiza moyo ni hicho why atuite bidhaa mbovu?
na leo bidhaa zile mbovu ndio zina msaidia kuliko hao wakiume alowaona ndio wenzie..
 
Habar za majukum wakuu? Bila kupoteza muda niende kwenye point..

Katika uelewa wangu hua naona wanawake hujengewa iman kua katika maisha yao pamoja na kua na ndoto zao, NDOA ni kama sahani ya kubebea hizo ndoto zao... NDOA kwa wanawake ni swala linalochukuliwa kama bahati tena ina paswa kutokea katika umri flan. Mwanamke akifikisha miaka 27+ hajaolewa inakua kama kadoda hivi, hata saikologia yake haiwi sawa kutokana na misingi ya iman iliopo kwenye jamii kuhusu ndoa na wanawake..

Kwa upande wa sisi wanaume pressure sio kubwa sana juu ya ndoa.. Ni kama chaguo la maamuz kwa wakat tutaopenda sisi.. Watu wanachelewa sana kuoa ila haiwi na uzito kama mwanamke atavyo chelewa kuoa..

Kwann wanaume tusiwe na pressure sawa na wanawake juu ya ndoa? Kwa mtazamo wangu tunge punguza wimbi kubwa la wanawake wanao saka ndoa kwa udi na uvumba.. Ila shida ni kua mwanaume ndoa ni kama option hadi pale mvi zinapo tokea ndo ulazima unaeza anza tokea..

Vipi kama uhitaj wa ndoa ungekua wa kiwango sawa kwa pande zote mbili?

Napenda kuwasilisha, tupate mitazamo yenu wakuu juu ya swala hili..
ndo hivyo mkuu tunatofautiana kwa mengi kwa suala la kijinsia
 
Sio wanawake wote wana Bp yakuolewa mkuu,wengine wana ndoto zao,mimi nilikataa kuolewa wakati nasoma wanaume wanakuja kuleta posa tena wenye Hadhi zao nilikata nikasema nataka kusoma sababu Dad alikua anaona watoto wa kike mzigo na sana alikua ana tumia hela nyingi sana kuwasomesha Kaka zetu shule za ghali sisi watoto wa kike alikua anasema nyie watoto wa kike ni bidhaa mbovu,unamsomesha mtoto unalipa fees nyingi matokeo yake anakujia na mimba mara anataka kuolewa sasa akija mtu kutaka kuoa mnakwendaa, kama kulikua kuna kitu kinaniumiza moyo ni hicho why atuite bidhaa mbovu?
na leo bidhaa zile mbovu ndio zina msaidia kuliko hao wakiume alowaona ndio wenzie..
100% wanawake ni wepesi sana kukumbuka wazee na ndugu zao. Wanaume huwa wana uzito fulani na ukikuta ndio wameshikika na wake zao hali huwa mbaya zaidi
 
".....NDOA kwa wanawake ni swala linalochukuliwa kama bahati tena ina paswa kutokea katika umri flan. Mwanamke akifikisha miaka 27+ hajaolewa inakua kama kadoda hivi, hata saikologia yake haiwi sawa kutokana na misingi ya iman iliopo kwenye jamii kuhusu ndoa na wanawake.. "

Hii ni kweli mkuu tofauti na sisi wanaume ambao tunaweza kuoa hata na miaka 50 ila mwanamke anazeeka/chakaa mapema ndio maana wanashauriwa waolewe mapema..
 
Sio wanawake wote wana Bp yakuolewa mkuu,wengine wana ndoto zao,mimi nilikataa kuolewa wakati nasoma wanaume wanakuja kuleta posa tena wenye Hadhi zao nilikata nikasema nataka kusoma sababu Dad alikua anaona watoto wa kike mzigo na sana alikua ana tumia hela nyingi sana kuwasomesha Kaka zetu shule za ghali sisi watoto wa kike alikua anasema nyie watoto wa kike ni bidhaa mbovu,unamsomesha mtoto unalipa fees nyingi matokeo yake anakujia na mimba mara anataka kuolewa sasa akija mtu kutaka kuoa mnakwendaa, kama kulikua kuna kitu kinaniumiza moyo ni hicho why atuite bidhaa mbovu?
na leo bidhaa zile mbovu ndio zina msaidia kuliko hao wakiume alowaona ndio wenzie..
Dah mkuu pole sana kwa hayo.. Mabadiliko yana maumivu.. Tusichoke kubadilisha mitazamo ya namna hii.. So saiv umeolewa? Uliolewa katika umri gan?
 
100% wanawake ni wepesi sana kukumbuka wazee na ndugu zao. Wanaume huwa wana uzito fulani na ukikuta ndio wameshikika na wake zao hali huwa mbaya zaidi
Hii kitu ni kwel.. Ila nadhan sabab kubwa ni mbili.. Moja intensity ya majukum ya mwanaume, ukioa una hudumia familia mbil pamoja na ww na mke wako.. Ila pili, inategemea na roho ya mke ulie nae.. Kuna wanawake wanakaba hawatak usaidie ndugu na jamaa zako..
 
Hii kitu ni kwel.. Ila nadhan sabab kubwa ni mbili.. Moja intensity ya majukum ya mwanaume, ukioa una hudumia familia mbil pamoja na ww na mke wako.. Ila pili, inategemea na roho ya mke ulie nae.. Kuna wanawake wanakaba hawatak usaidie ndugu na jamaa zako..
Ndugu yawezekana ukawa sahhihi lakini kuna baadhi ya wanaume hata ndoa hawana,lakini nyumbani hawakumbuki kabisaa
 
Tanzania hii na bado ninyi mna hamu ya kuwaza ndoa! Great sinker
 
Habar za majukum wakuu? Bila kupoteza muda niende kwenye point..

Katika uelewa wangu hua naona wanawake hujengewa iman kua katika maisha yao pamoja na kua na ndoto zao, NDOA ni kama sahani ya kubebea hizo ndoto zao... NDOA kwa wanawake ni swala linalochukuliwa kama bahati tena ina paswa kutokea katika umri flan. Mwanamke akifikisha miaka 27+ hajaolewa inakua kama kadoda hivi, hata saikologia yake haiwi sawa kutokana na misingi ya iman iliopo kwenye jamii kuhusu ndoa na wanawake..

Kwa upande wa sisi wanaume pressure sio kubwa sana juu ya ndoa.. Ni kama chaguo la maamuz kwa wakat tutaopenda sisi.. Watu wanachelewa sana kuoa ila haiwi na uzito kama mwanamke atavyo chelewa kuoa..

Kwann wanaume tusiwe na pressure sawa na wanawake juu ya ndoa? Kwa mtazamo wangu tunge punguza wimbi kubwa la wanawake wanao saka ndoa kwa udi na uvumba.. Ila shida ni kua mwanaume ndoa ni kama option hadi pale mvi zinapo tokea ndo ulazima unaeza anza tokea..

Vipi kama uhitaj wa ndoa ungekua wa kiwango sawa kwa pande zote mbili?

Napenda kuwasilisha, tupate mitazamo yenu wakuu juu ya swala hili..
Anakudai ndoa.anakujw kubadirika sasa hapo ndio atutaki ujinga kama
 
Tanzania hii na bado ninyi mna hamu ya kuwaza ndoa! Great sinker
Kwanini tusiwazie Ndoa mkuu, hali ya kuwa tumejiandaa? Na umri unasogea
Maamuzi ni yetu. Wewe andaa michango tu. Usitukatishe tamaa.
 
Kuoa vibibi inahitaji moyo, labda uwe mstaafu na mafao yako.
Huwa nawaonea huruma sana wanawake walio kwenye 30s na hawajaolewa, mbaya zaidi unakuta hana hata mtoto. Hata hivyo nina mpango wa kuanza kuwafariji hawa mabibi, nitakuwa nawaoa kwa mkataba.
kwenda huko? 30's nani kakwambia ni bibi jamani
bado yuko kwenye ulingo wa ujana hadi afike 45 so usilete zako hapa
 
Kwa sabab Jibu lipo kweny ii mistari miwili

"a woman finds a husband and life ends, A man finds a wife and life begins. "
 
Back
Top Bottom