Kijakazi
Platinum Member
- Jun 26, 2007
- 10,428
- 17,747
Hivi ni kwanini ktk nchi zooote barani Afrika zaidi ya 50, Watz wengi hupenda kujipima na kujilinganisha na Kenya tu?
Na hii ni kuanzia Viongozi mpaka Wananchi yaani kwa mfano kuna nchi nyingi sana Afrika ambazo zinaizidi Nchi yetu kiuchumi kwamba zina Uchumi mkubwa kuliko wetu, sasa ni kwa nini tuwe tunajilinganisha na Kenya tu?
Hata kwenye malengo ya Nchi utasikia Viongozi (wetu) mwaka fulani tutaipita Kenya, hata kama tukijenga Kiwanja cha mpira utasikia ni kikubwa AM nzima (na hapo wanamaanisha nchi mbili tu UG na hasa Kenya), hata kama ni ukumbi wa Disko tu utasikia ni mkubwa hata Kenya hamna, kwanini tusiseme hiki Kiwanja ni kikubwa Afrika Nzima?
Hata kwenye bandari lengo ni kuizidi Bandari ya Mombasa tu, sasa kwanini isiwe kuwa na Bandari kubwa na yenye ufanisi kushinda zote Afrika nzima? yaani tushindane na Beira, Durban, Djibouti n.k ni kwa nini Kenya tu?
Ukija kwenye Reli ni hivyo Mshindani na wakujilinganisha naye ni Kenya tu! Kwanini isiwe Kongo, Zambia, Malawi, Zimbabwe, Ethiopia n.k
Ukija kwenye Utalii ni hivyo hivyo lengo SIYO kupata watalii wengi kuliko nchi zote Afrika, hapana bali ni kuwa na Watalii wengi kuliko Kenya, sasa ni kwanini? Kwa nini Siyo lkuliko Zimbabwe au AK au Misri?
Kuna anaye jua sababu hasa, ni kwa nini Kipimo chetu ni Kenya tu? Na je kama tukifanikiwa kuwazidi Kenya Kiuchumi, tutakuwa tumefanikiwa nini hasa?
Na hii ni kuanzia Viongozi mpaka Wananchi yaani kwa mfano kuna nchi nyingi sana Afrika ambazo zinaizidi Nchi yetu kiuchumi kwamba zina Uchumi mkubwa kuliko wetu, sasa ni kwa nini tuwe tunajilinganisha na Kenya tu?
Hata kwenye malengo ya Nchi utasikia Viongozi (wetu) mwaka fulani tutaipita Kenya, hata kama tukijenga Kiwanja cha mpira utasikia ni kikubwa AM nzima (na hapo wanamaanisha nchi mbili tu UG na hasa Kenya), hata kama ni ukumbi wa Disko tu utasikia ni mkubwa hata Kenya hamna, kwanini tusiseme hiki Kiwanja ni kikubwa Afrika Nzima?
Hata kwenye bandari lengo ni kuizidi Bandari ya Mombasa tu, sasa kwanini isiwe kuwa na Bandari kubwa na yenye ufanisi kushinda zote Afrika nzima? yaani tushindane na Beira, Durban, Djibouti n.k ni kwa nini Kenya tu?
Ukija kwenye Reli ni hivyo Mshindani na wakujilinganisha naye ni Kenya tu! Kwanini isiwe Kongo, Zambia, Malawi, Zimbabwe, Ethiopia n.k
Ukija kwenye Utalii ni hivyo hivyo lengo SIYO kupata watalii wengi kuliko nchi zote Afrika, hapana bali ni kuwa na Watalii wengi kuliko Kenya, sasa ni kwanini? Kwa nini Siyo lkuliko Zimbabwe au AK au Misri?
Kuna anaye jua sababu hasa, ni kwa nini Kipimo chetu ni Kenya tu? Na je kama tukifanikiwa kuwazidi Kenya Kiuchumi, tutakuwa tumefanikiwa nini hasa?