Kwanini kamba za viatu hufunguka?

Kwanini kamba za viatu hufunguka?

Pyepyepye

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2017
Posts
1,940
Reaction score
3,842
Habari wanajamvi.

Ni imani yangu kuwa mu wazima wa afya. Naja kwenu nikiwa na imani na jukwaa hili, kwa imani hiyo naamini mtanisaidia kuondoka katika mtanziko huu.

Naomba kuelimishwa juu ya jambo hili la kamba za viatu, mara nyingi hata kama ninakua nimefunga na kukaza kiasi gani, bado nikifanya mizunguko kadha wa kadha, utakuta kamba za viatu zinalegea ama kufunguka kabisa.

Naomba kuwasilisha.
 
kuna ufungaji wake wa kamba hazifunguki hata utembee kutoka dar hadi mwanza kwa mguu, yani unafunga kamba wakati wa kuvaa unafungua kamba mwenyewe ukitaka kuvua viatu
hata ukitaka uvue viatu bila kufungua kamba unachomoa mguu na kamba zinabaki vilevile ulivyofunga
 
Hata hivyo kwa kawaida hutakiwi kuvaa viatu vinavyobana sana au vilivyokazwa/fungwa sana, hasa kwa watu wanene na wenye kisukari.
Nafikiri unakuwa hujafunga uzuri au aina ya kamba zenyewe
 
Hii hutokana na aina ya GIDAMU unazotumia zile zenye nyuzinyuzi za nylon huwa zinalegea zenyewe pale unapotembea.

Ukitumia zile za cotton tembea DAR MPAKA MORO hazifunguki ng'0
 
zinafunguka kwa sababu zimefungwa

kama usipo zifunga haziwezi funguka.maana zitakuwa ziko wazi.

kurusha miguu kwa muda mrefu kunafanya zilegee (kuteleza toka katika fundo ) hivyo kufunguka
 
Wanaume wa DSM hata kufunga kamba za viatu zikakaza mnashindwa du. Mnatia aibu
 
Kama hakuna ujumbe uliofichika basi punguza kutembea kama bata maji mkuu!
 
Hata akaze vipi, maisha yatalegea kama kamba za viatu
 
Ufungaji wako tu, utakuwa unafunga masikio ta panya baba yangu alikuwa ananiambiaga hivyo..!
 
Kuna namna tulifundishwa kufunga viatu tukiwa jkt nilikuwa nakaa navyo mguuni siku saba bila kufungua pamoja na mabio yote yale, huenda wewe unafunga kilegevu.
 
kuna ufungaji wake wa kamba hazifunguki hata utembee kutoka dar hadi mwanza kwa mguu, yani unafunga kamba wakati wa kuvaa unafungua kamba mwenyewe ukitaka kuvua viatu
hata ukitaka uvue viatu bila kufungua kamba unachomoa mguu na kamba zinabaki vilevile ulivyofunga
ndomana nimemwambia kuna ufungaji wa kamba ukifunga hazifunguki hadi ufungue mwenyewe

hata mm nilifundishwa JKT yani ukifunga kamba utakimbia weee utapiga kwata kamba hazifunguki haijalishi umevaa kiatu gani hata ikiwa raba na haijalishi aina ya kamba
Kuna namna tulifundishwa kufunga viatu tukiwa jkt nilikuwa nakaa navyo mguuni siku saba bila kufungua pamoja na mabio yote yale, huenda wewe unafunga kilegevu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom