Kwanini ishara, maajabu na miujiza mikubwa inafanywa na watu wanaoiamini Biblia tu?

Kwanini ishara, maajabu na miujiza mikubwa inafanywa na watu wanaoiamini Biblia tu?

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Katika historia ya ulimwengu, tumeshuhudia matendo makuu yasiyoelezeka kwa akili ya kibinadamu, kama vile wagonjwa kupona, viwete kutembea, mabubu kuongea, vipofu kuona, wafu kufufuka, na bahari kugawanyika. Jambo la kushangaza ni kwamba, ishara hizi kubwa zimefanywa tu na watu wanaoiamini Biblia kuwa ni Neno la Mungu. Kwanini?

Mifano ya haraka:
Musa, aliyeiamini Torati, aliigawanya Bahari ya Shamu (Kutoka 14:21).
Elia, nabii wa Mungu, alileta moto kutoka mbinguni (1 Wafalme 18:38).
Mitume, waliohubiri Injili, walifanya ishara nyingi: Petro alimponya kiwete, Paulo alimfufua Eutiko (Matendo 3:6-8; 20:9-12).

Labda utasema hiyo miujiza ilifanywa zamani. Siku hizi hakuna miujiza! Mimi sio wa zamani. Sawasawa na andiko la Yohana 14:12, nimeshuhudia miujiza mikubwa maishani mwangu...

Nimepona makumi ya magonjwa kwa kuweka mkono tu sehemu inayouma na kukemea kwa Jina la Yesu. Mara nyingi, nimeyafukuza mapepo yaliyokuja kunishambulia.

Kwa Jina la Yesu, 'nimewapiga stop', si mara moja, majambazi waliojaribu kunidhuru, nk, nk, nk

Mambo haya mazito siyasikii au kuyaona nje ya watu wanaoiamini Biblia na Yesu mtenda miujiza. Kwanini?

Kama huo sio ushahidi kwamba Biblia ni Neno la Mungu, nitajie sababu yako wewe...
Kwanini ishara, maajabu na miujiza mikubwa inafanywa na watu wanaoiamini Biblia tu?
 
"Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya." (Mk 16:17-18)
 
Miujiza ufanywa na mtu yeyeto aliyepewa karama za miujiza haijalishi anaeamini au la
Duh, The redemeer unamsahihisha Yesu aliyesema hivi:
Mk 16:17
"Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya."

Unapewaje karama ya miujiza kama huamini?
 
Mwanamalundi unamjua!?
Unamaanisha yule mzururaji na mcheza ngoma ambaye tukio la kifo chake liliitwa "hang'witulo gwa shigela."??
Kama ni huyo basi wewe gallow bird hujui hata kutamka jina lake: Tamka hivi: "Ngw'anamalundi" 😎
Huyo alikuwa anatumiwa tu na shetani kutenda miujiza feki. Shetani ana uwezo wa kuiga, kudanganya, na kuonyesha ishara za ajabu ili kuwapotosha watu wasimwamini Mungu wa kweli.

Kumbuka wale waganga wa Misri walijaribu kufanya miujiza kama ya Musa(Kutoka 7:10–12). Hata wachawi wa leo wanafanya miujiza ya kipepo pepo. Muulize Mshana Jr kabla hajaokoka alikuwa akifanya nini.

Miujiza ninayoizungumzia katika mada hii ni miujiza inayotokana na uweza wa Mungu.
 
Unamaanisha yule mzururaji na mcheza ngoma ambaye tukio la kifo chake liliitwa "hang'witulo gwa shigela."??
Kama ni huyo basi wewe gallow bird hujui hata kutamka jina lake: Tamka hivi: "Ngw'anamalundi" 😎
Huyo alikuwa anatumiwa tu na shetani kutenda miujiza feki. Shetani ana uwezo wa kuiga, kudanganya, na kuonyesha ishara za ajabu ili kuwapotosha watu wasimwamini Mungu wa kweli.

Kumbuka wale waganga wa Misri walijaribu kufanya miujiza kama ya Musa(Kutoka 7:10–12). Hata wachawi wa leo wanafanya miujiza ya kipepo pepo. Muulize Mshana Jr kabla hajaokoka alikuwa akifanya nini.

Miujiza ninayoizungumzia katika mada hii ni miujiza inayotokana na uweza wa Mungu.
Una uhakika gani mwana malundi hakufanya miujiza kwa uwezo wa Mungu?.. alitembea juu ya maji,alikausha miti mibichi kuwa kuni,alifukua majabali kwa mkono...
 
Kwani Islam ni dinii au kikundi cha wahuni waliojipachika madaraka ya kidini!?
 
Unamaanisha yule mzururaji na mcheza ngoma ambaye tukio la kifo chake liliitwa "hang'witulo gwa shigela."??
Kama ni huyo basi wewe gallow bird hujui hata kutamka jina lake: Tamka hivi: "Ngw'anamalundi" 😎
Huyo alikuwa anatumiwa tu na shetani kutenda miujiza feki. Shetani ana uwezo wa kuiga, kudanganya, na kuonyesha ishara za ajabu ili kuwapotosha watu wasimwamini Mungu wa kweli.

Kumbuka wale waganga wa Misri walijaribu kufanya miujiza kama ya Musa(Kutoka 7:10–12). Hata wachawi wa leo wanafanya miujiza ya kipepo pepo. Muulize Mshana Jr kabla hajaokoka alikuwa akifanya nini.

Miujiza ninayoizungumzia katika mada hii ni miujiza inayotokana na uweza wa Mungu.
Hahahahahaha una uhakika gani Ng'wanamalundi hamuombi Mungu wake??
 
Una uhakika gani mwana malundi hakufanya miujiza kwa uwezo wa Mungu?.. alitembea juu ya maji,alikausha miti mibichi kuwa kuni,alifukua majabali kwa mkono...
Wanaosimulia habari zake wanasema ujuzi wake wa kucheza ngoma aliupata kwa bibi mganga wa kienyeji. Hivyo ni wazi hata miujiza yote aliyoifanya ni ya kichawi.
 
Wanaosimulia habari zake wanasema ujuzi wake wa kucheza ngoma aliupata kwa bibi mganga wa kienyeji. Hivyo ni wazi hata miujiza yote aliyoifanya ni ya kichawi.
Kwa hiyo umesikia tu!?.. unajua tofauti ya uganga na uchawi?
 
Kwa hiyo umesikia tu!?.. unajua tofauti ya uganga na uchawi?
Hata wewe umesikia tu, maana sidhani kama ulikuwepo mwaka 1936 alipofariki.
Najua tofauti ya uganga na uchawi ila nafikiri tukianza kuelezana maana ya maneno hayo ya Kiswahili tutakuwa tumetoka nje ya lengo la mada. Au sio gallow bird?
 
Hahahahahaha una uhakika gani Ng'wanamalundi hamuombi Mungu wake??
Mimi sio Mkongwee kama wewe, ila habari nilizo nazo ni kwamba Ng'wanamalundi alifariki mwaka 1936 katika mazingira ya kichawi. Hakuwa anamuomba Mungu. Au kuna Ng'wanamalundi mwingine?
 
Hayo mnayoyafanya ni maigizo ya wazi.

Kama kweli mnaweza kuponya mbona hospitali zina wagonjwa wanateseka kila siku - hamuwaoni? Umewahi kutembelea MOI au KCMC wewe?
Hata Yesu hakuponya watu wote kila mahali alipoenda.
Mt 13:58
Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.

Wewe Ibn Unuq unafikiri watu wote MOI na KCMC wanamwamini Yesu? Hujui kuwa huko nako kuna Atheists wasiotaka hata kuombewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom