Kwanini hatukufundishwa haya?

Kwanini hatukufundishwa haya?

Ushimen

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2012
Posts
42,414
Reaction score
104,851
Miaka ile, palifanyika jaribio la kupinduliwa kwa serikali ya Mwalimu Julus Kambarage Nyerere. Kinacho nifanya nianze kujiuliza maswali kuhusiana na tukio lile ni kama hivi:-

Kwanini serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania haijawahi kutoa tamko la kukanusha jaribio la kupinduliwa kwa Mwalimu Nyerere? Kama tukio lile halijawahi kukanushwa, najikuta ninaamini kwamba ni kweli jaribio la kuiangusha serikali ya Nyerere ni tukio la ukweli.

Lakini kwanini tukio lile halikuandikwa kwenye vitabu vya historia ya Tanzania? Kwanini tukio lile lilifichwa na halikufundishwa shuleni ili wanafunzi waweze kujua historia ya nchi yao?

Karibuni tujadili.

Na kwa wenye kujua kwanini tukio hili halikuwekwa kwenye vitabu vya historia.
 
Upo sahihi kwa haya ulioyaeleza,wewe ulitaka wafundishwe ili wajifunze nini? Lakini naamini tukio lile alikuwa kama la Burundi, maana Burundi ndio unaweza kusema watu wajifunze maana ilionekana serikali imeyumbishwa karibu wiki nzima, lakini kwa Tanzania hata dakika moja haikufika sasa watu watajifunza nini? Tanzania haijawai kupindiliwa kiongozi.
 
Mkuu sio kila kitu huandikwa na ndio maana hata Kambarage alivyokuwa analala na kuzikwa makaburini ili Watanganyika mpate uhuru haijaandikwa...
 
Mkuu sio kila kitu huandikwa na ndio maana hata Kambarage alivyokuwa analala na kuzikwa makaburini ili Watanganyika mpate uhuru haijaandikwa...

Lakini Watu8, hauoni kwamba mambo haya yasipo andikwa historia halisi itapotea?
Je, hauoni kwamba vizazi vijavyo vitakosa kujifunza yalio jiri na kubaki kama hadithi za kusadikika?
 
Last edited by a moderator:
Si hayo tu mkuu, vita ya Kagera nayo ni kizungumkuti, waasisi wa mapinduzi Zanzibar na makosa ya CCM katika utawala wake etc.
 
Dude lao
Nakushangaa mkuu, kama kweli hauoni umuhimu wa vizazi kuelezwa au kufundishwa kuhusu ukweli wa yaliojiri. Na pengine nikurekebishe ulipoteleza, hapo nikimaanisha jaribio la kupinduliwa kwa serikali ya Mwl. Nyerere, tena mara tatu katika miaka tofauti tofauti.

Asante Alexism. Haya ndio mambo niyapendayo mkuu, napenda sana kufunyua ukweli uliofichwa.

Dude lao
Japo historia haisemi wazi juu ya mambo mengi sana Tanganyika na Tanzania ya leo, lakini Mwalimu Nyerere tangu awe kiongozi wa nchi hii amenusurika mapinduzi MATATU.

Moja ni la mwaka 1964, la pili ni la mwaka 1970 na la mwisho ni la mwaka 1982.

Jaribio la kwanza ndilo lilipelekea kuundwa kwa JWTZ na lilizimwa kwa msaada wa Malkia wa Uingereza aliyetuma makomandoo maalumu na wakafanikiwa. Jaribio la pili ndilo lililopelekea kuundwa kwa usalama wa Taifa na kikosi maalumu cha ulinzi wa rais. Na jaribio la mwisho ndio lilipelekea kubadili sera ya usalama wa Taifa kwa kuwapandikiza kila kwenye sekta na kuwa kila mtu ni mlinzi wa nchi hii (usalama)

Leo nitazungumzia jaribio/ uasi wa 20 Januari 1964 na nini hasa ilikuwa chanzo cha uasi ule:

Kuasi kule kwa wanajeshi Januari 20 1964 (Tanganyika Rifles) wala sio jambo la zamani sana kiasi cha kusema kwamba historia ile imetupwa na hakuna anayesema ukweli, nilikuwa nahisi viongozi kama Mwalimu, Kawawa na Kambona wangeyaweka katika maandishi mambo yale muhimu katika historia ya nchi yetu kabla hawajatutoka. Hakuna mahali mambo haya yameandikwa na ndio maana vijana wanaotaka kujua historia ya nchi yao wanakuja na hizi hearsay.

Askari wale wa Tanganyika Rifles waliasi... Miongoni mwa mambo waliyokuwa wanadai ni hali nzuri ya maisha ya askari Mtanganyika, mshahara ulikuwa mdogo, hawakupandishwa vyeo na hakukuwa na Watanganyika katika vyeo vya juu ndani ya Jeshi lile.

Askari waliasi na kuingia mjini, na wengine walikwenda kwenye makazi ya maafisa wa Kiingereza (raia) na kuwashikilia. Waziri wa ulinzi wakati huo alikuwa Oscar Kambona. Mwalimu na Mzee Kawawa kwa usalama wao walitoroshwa na kwenda kujificha. Inasemekana maficho yao yalikuwa Kigamboni. Waziri wa ulinzi (Kambona) alijaribu kupita katika barracks na kuwaomba askari watulie bila mafanikio.

Hali ile iliendelea kuwa mbaya na Mwalimu kwa ushauri wa Kambona na Kawawa akaomba msaada kwa Uingereza ili waje waokoe hali ile ambayo ilikuwa inaelekea kuwa mbaya,kufuatia kuasi kwa askari wetu, askari wa Kenya na Uganda nao waliasi kwa sababu sawa kabisa na za uasi wa Tanganyika Rifles.

Malkia alituma kikosi maalumu cha askari wa Uingereza ambao walikuwepo katika ghuba ya Aden, askari hao walikuja na meli kubwa ya kivita HMS Centaur ambayo ilikuwa na makomandoo (45 RM),askari na helikopta. Walifanikiwa kutuliza maasi yale, na Mwalimu na Kawawa wakatoka mafichoni na kuonekana hadharani wakiwa na waziri wa ulinzi, ambaye alifanya kazi kubwa bila mafanikio kuwaomba askari (Waliokuwa wananuheshimu sana) waache uasi na madai yao yatafanyiwa kazi.
 
Ni kweli na ni ajabu kubwa kwamba watanzania hatupendi kuandika kama tusivyopenda kusoma. Hata historia tukufu ya kuhusika kwa Tanzania katika ukombozi wa karibu kila nchi ya Kusini mwa Africa (Msumbiji, Angola, Botswan. A. Kusini, Zimbabwe) na uhuru wa Malawi na Zambia, historia hizi tumezichukulia kama hadithi za mtaani.

Juzi tu Mh. Mugabe alichukizwa sana kwa jinsi bara la Africa lilivyomficha Nyerere na hasa hata watanzania wenyewe walivyomweka Mwalimu chini ya uvungu.

Nyerere ndio kiongozi mkubwa zaidi Africa, ndio kuliko Mandela na Nkurumah, kwa jinsi sisi watanzania tulivyo na aibu na tabia ya kufunika mambo yetu matukufu, basi hao viongozi wengine wanatukuzwa zaidi.

Hata vivutio vyetu vya utalii hatutangazi hadi wageni watusaidie. Mfano ni juzi tu kutangazwa kwa Tanzania kuwa nchi ya 1 yenye vivutio vikubwa na vizuri zaidi Africa (Africa best tuorist destination) lakini sisi tupo tu.

Kwa maoni yangu tatizo kubwa ni uvivu na ujinga mkubwa katika taifa letu.

Kumbuka hata Kiswahili ni chetu hasa lakini waandishi wakubwa wa vitabu vya Kiswahili na waalimu wakubwa wa Kiswahili nchi za nje ni Wakenya!

We are a shy nation, we have to change as soon as possible!!!
 
1964 yalikuwa maasi na si mapinduzi. Hakuna mwanajeshi aliyekuwa amepanga kupindua Nchi.

La mwaka 1982 lilikuwa jaribio la mapinduzi na wahusika walifikishwa mahakamani kwa uwazi, wakashtakiwa na kupatikana na hatia. Kifungo cha maisha, japo waliachiwa kwa msamaha wa Rais miaka kumi baadaye.
 
Kiujumla Historia ya Tanganyika imepuuzwa na watawwala. Iko wapi historia ya akina Abdallah Kassim Hanga, Iko wapi historia ya akina Tuntemeke Sanga, akina Tumbo, akina Oscar Kambona??
 
Lakini Watu8, hauoni kwamba mambo haya yasipo andikwa historia halisi itapotea?
Je, hauoni kwamba vizazi vijavyo vitakosa kujifunza yalio jiri na kubaki kama hadithi za kusadikika?

Ni kweli kuwa kama matukio yakiachwa pasipo kuandikwa au kuwekwa katika mitaala basi kumbukumbu zake zitapotea...
 
Last edited by a moderator:
Umetoa historia nzuri ambayo nahisi wengi hatukuijua.

Asate mkuu..
Nami nimeipata kupitia mitandaoni

Kiujumla Historia ya Tanganyika imepuuzwa na watawwala. Iko wapi historia ya akina Abdallah Kassim Hanga, Iko wapi historia ya akina Tuntemeke Sanga, akina Tumbo, akina Oscar Kambona??
Mussolin5, binafsi nimekua nikijuliza maswali kadhaa kuhusiana na kufichwa kwa mambo kama haya. Na ninapata mashaka sana linapokuja swala la kwanini mkuu wa kaya kipindi kile hakupenda ukweli huu uanikwe bayana?

JK alikua akiogopwa kuliko kawaida, je, kwanini alijenga mazingira ya kuogopeka kiasi hiki?

Pia sijapata kusoma popote kwenye uwazi kwamba JK aliwahi kukosea popote wakati wa utawala wake. Je, maana yake ni kwamba Mwalimu alikua mkamilifu na msafi Kama theluji?
 
Wale jamaa walishapewa adhabu yao, hakuna atakayejaribu hiyo kitu tena
 
Hivyo vitabu ukiangalia kwenye maktaba za Tanzania huwezi kuvikuta, lakini ukienda Ulaya unavikuta. Hii ni kuonyesha kiasi gani Watanzania hatuna historia ya kutunza historia na hatupendi kujifunza kutokana na historia.
 
Mtoa mada ujaribu kuelewa mambo.

Hakukuwa na jaribio la kumwangusha Mwl. Ila kulikuwa na mipango ya kuangusha serikali ya Mwl. mwaka 1983. Wote waliohusika walikamatwa kabla hata jaribio kufanyika.

Mwaka 1964 kulikuwa na uasi jeshini ambao nao ulitulizwa. Ni tofauti kubwa kusema jaribio na kusema kula njama/ kufanya mipango. Nadhani umenisoma mkuu.
 
Mtoa mada ujaribu kuelewa mambo.

Hakukuwa na jaribio la kumwangusha Mwl. Ila kulikuwa na mipango ya kuangusha serikali ya Mwl. mwaka 1983. Wote waliohusika walikamatwa kabla hata jaribio kufanyika.

Mwaka 1964 kulikuwa na uasi jeshini ambao nao ulitulizwa. Ni tofauti kubwa kusema jaribio na kusema kula njama/ kufanya mipango. Nadhani umenisoma mkuu.
casaNostra, nivema ungeweka hayo uyasemayo kwa ujazo ili nami nipate kujifunza kutoka kwa yale utakayo yaleta jamvini.
Ingependeza zaidi iwapo utatufafanulia hicho unacho mipango ya kuangusha serikali 1983 kama unalivyo ahinisha.
Jaribio/ Njama/ Uasi wa Jeshi, yote hayo yalimlenga Mwalimu.
Na sitaki kuamini kwamba haya yalitokea pasipo sababu, na hapa ndipo napata kuamini kwamba Jk ndie aliekua sababu mpaka kupelekea haya kutokea.
Kingine naona ume mention matukio haya mwaka 1983 na 1964. Je, hapakuwahi tokea tukio kama hilo au lakufanana na hayo katika wakati tofauti na 1983, 1964?

Nikirudi kwenye lengo kuu la kuleta Uzi huu hapa ni:-
Kwanini matukio haya hayakuwekwa kwenye vitabu vya historia?
Kwanini hatukufundishwa mashuleni walau tupate kujua yalio tokea kwenye historia ya nchi yetu?
Kwanini kama sio kweli serikali haujawahi kukanusha?
Kwanini matukio haya yalifichwa?
 
Last edited by a moderator:
wakuu wa mada hii binafsi ningependa kujua kuhusu hili jaribio la la mapinduzi la 1982.

Nimeweka mtiririko wa matukio haya kwa ufupi, kwa kumjibu mmoja wa wana jf kuli kurasa za juu mkuu
 
Kuna kesi ya uhaini,imekuwa reported kwenye vitabu vya sheria.Ni kesi maarufu Sana.Wanafunzi wengi WA sheria wameisoma.
 
Miaka ile, palifanyika jaribio la kupinduliwa kwa serikali ya Mwalimu Julus Kambarage Nyerere. Kinacho nifanya nianze kujiuliza maswali kuhusiana na tukio lile ni kama hivi:-

Kwanini serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania haijawahi kutoa tamko la kukanusha jaribio la kupinduliwa kwa Mwalimu Nyerere? Kama tukio lile halijawahi kukanushwa, najikuta ninaamini kwamba ni kweli jaribio la kuiangusha serikali ya Nyerere ni tukio la ukweli.

Lakini kwanini tukio lile halikuandikwa kwenye vitabu vya historia ya Tanzania? Kwanini tukio lile lilifichwa na halikufundishwa shuleni ili wanafunzi waweze kujua historia ya nchi yao?

Karibuni tujadili.

Na kwa wenye kujua kwanini tukio hili halikuwekwa kwenye vitabu vya historia.

Kamwulize Zacharia Hans Pope kama halikuwepo na kwa nini alitupwa kizuizini mpaka Mwinyi alipowasamehe baada ya kushauriana na Nyerere ndipo utajua lilikuwepo au la
 
Back
Top Bottom