Mimi ni kijana wa miaka 21, lakini nimepitia maisha ya huzuni na msongo wa mawazo japo kwa nje naonekana mwenye furaha, historia yangu inasikitisha sana nimeamua kushare na ninyi, nilipokuwa na miaka 12 nilienda kuomba sindano ya kushonea kwa jirani kwa ajili ya kutengenezea mpira nilikua napenda sana mpira kwa bahati mbaya ile sindano ilinichoma, mwaka 2014 nikiwa na miaka 14 nilianza kuhisi dalili kadhaa za HIV na kuanzia huo mwaka mpaka leo nimekuwa mtu wa mawazo sana nimeshindwa kwenda kupima nikihisi ntakutwa nao, na yule mama naskia anao.
Ndugu zangu nilikuwa na akili sana darasani lakini kuanzia form one nilianza kufanya vibaya kwa sababu ya mawazo hayo, Form 4 nilifaulu kwa division III ya kawaida yote sababu ya mawazo, baba yangu alinidhihaki kwa matokeo sikumlaumu kwa sababu hakujua machungu niliyopitia na ninayo pitia, najiuliza kwanin Mungu ameruhusu mtu innocent kama mim niteseke mienendo yngu ni mizuri lakn kwanini hili baya linipate?
Chuo nimestopisha kwa sasa Nina mpenzi nimempima HIV yupo safe kabisa ananipenda sana Ila sijataka kuwa naye kimwili mpaka nitakapojua mstakabali wangu, wito wangu kwa wazazi vitu kama sindano na vitu vyenye ncha kali ni vya kuwa navyo nyumbani pia vitu kama sindano si vya kuazima tafadhalini, na sio kuwa kila anachopitia mtoto atakuelezea jaribuni kukaa na watoto wenu karibu, kwanin mruhusu wasiokua na hatia walie maisha yao yote?