Hakuna mtu aliyepinga kwenda Dodoma tatizo ni mipango.Mgonjwa huwa tumaini ndilo linalompa nguvu...ujiandaye kwenda kijijini...safari ya Dodoma ni lazima ila wale wanaohusika tu...wewe tafuta fursa ya kuwasaidia masikini kule kijijini..
Hoja yangu haihitaji kutetewa inasimama yenyewe...inakumulika kila siku kama ambavyo huwezi kukwepa mwale wa jua either unampenda au unamchukia Mungu!
Huu ni uswahili unaofanya ndio maana hatukuendelea muda mrefu kwa kuwa serikali ilijaa watu wenye mawazo ksma yako.Ukiyasoma na kumweleza mtu ni kama yana hekima fulani lakini ni pepo zito la umaskini ndilo linaweza kukyongoza kusema hivyo.Ndio maana mwingine anaoa hana hata kitanda lakini miaka kadhaa baadae anamiliki jumba la kifahari wakati mwingine anajipanga kabla ya kuoa lakini maisha yake yanabaki ya kawaida hadi anazeeka.Haya mambo ya kung'ang'ania Dar ni kuumiza watu wengi wanao fuata huduma Dar wakati watu wale wale wachache wanazidi kufaidika na pesa tunazowapelekea katika mahoteli nk.Bora kundi lingine la watu lianze kufaidi hicho wanachofaidi watu wa Dar.Jibu la kisiasa ni kwamba tunasogeza huduma kwa wananchi. Huduma zipi? Tunasogeza maendeleo kwa wananchi. Kwahiyo baada ya Dodoma tutahamia wapi?
Rais Magufuli anatamani nchi iwe ya asali kwa miezi kadhaa. Hivi karibuni kaanzisha mipango mingi saana yenye gharama kubwa.
Kuna flyovers (sijui zitasalimika maana watu wanahama), kuna mradi wa mwendo kazi Mbagala, ujenzi wa reli wa standard gauge (trillion 16 - budget yetu trillion 29), elimu bure kwa sekondari, kuna ule mradi wa barabara Dar mpaka Chalinze, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu na miradi mingineyo.
Hili la Dodoma ni kuvuruga bajeti bila mpangilio. Mpango huu hata kama upo ukienda kwa taratibu tutapoteza nini? Wafanyakazi wanaambiwa wiki ijayo wawe Dodoma.
Hawa sio mbuzi kwamba hawahitaji kujipanga. Wanafamilia zao. Huu mpango ulivyo kuna ulazima gani wa kuikurupua serikali nzima kwa haraka? Kwanini tusipange. Hivi kipaumbele ni makao makuu au upatikanaji wa maji.
Wananchi wanashirikishwaje katika mipango inayowahusu.
Mheshimiwa mwenye nchi, mipango yenye kukurupuka huvuruga uchumi. Fikiria mwekezaji amekopa na anataka kuweka jengo la ofisi pale Posta. Ghafla unaibuka na mpango mkubwa kama huu.
Ni nani mwenye fikra timilifu atawekeza kwenye viwanda bila kufahamu mipango ya serikali. Nchi hujenga kwa mipango imara na yenye kueleweka.
Dira ya tunapoelekea lazima iwe wazi na ifahamike. Tumerithi mipango mingi saana kutoka tawala zilizopita.
Kuna mipango ya kijamaa ambayo tuliitia kapuni kimya kimya na mengineyo. Teknolojia imebadilika na kurahisisha kila jambo.
Wananchi wanahitaji huduma na sio sura za viongozi wa serikali hapa Dodoma.
Nchi haiwezi kukwama.Na kama kuna mtu anadhani atakwamisha ajue atakwama yeyeMkuu nchi haijaribiwi. Ni lazima tupange. Tutakwama. Ile budget yenyewe hatujui itatoka wapi. Tumehama kwenye viwanda, tunahamia uwekezaji wa majengo Dodoma.
Kwahiyo hoja ni kugawana kufaidi? Niliuliza swali la msingi, Huduma gani watu wanafuata Dar wakati wa utandawazi?Huu ni uswahili unaofanya ndio maana hatukuendelea muda mrefu kwa kuwa serikali ilijaa watu wenye mawazo ksma yako.Ukiyasoma na kumweleza mtu ni kama yana hekima fulani lakini ni pepo zito la umaskini ndilo linaweza kukyongoza kusema hivyo.Ndio maana mwingine anaoa hana hata kitanda lakini miaka kadhaa baadae anamiliki jumba la kifahari wakati mwingine anajipanga kabla ya kuoa lakini maisha yake yanabaki ya kawaida hadi anazeeka.Haya mambo ya kung'ang'ania Dar ni kuumiza watu wengi wanao fuata huduma Dar wakati watu wale wale wachache wanazidi kufaidika na pesa tunazowapelekea katika mahoteli nk.Bora kundi lingine la watu lianze kufaidi hicho wanachofaidi watu wa Dar.
Unadhani nchi kukwama ni kama gari litakavyoonekana? Zile purukushani za wiki hii tunahamia, na mie mwezi ujao. Ziko wapi? Huo ndio mkwamo.Nchi haiwezi kukwama.Na kama kuna mtu anadhani atakwamisha ajue atakwama yeye
Kazi nyingi za serikali hazifanyiki kwenye mitandao mkuu hili lazima ulijueKwahiyo hoja ni kugawana kufaidi? Niliuliza swali la msingi, Huduma gani watu wanafuata Dar wakati wa utandawazi?
Unadhani nchi kukwama ni kama gari litakavyoonekana? Zile purukushani za wiki hii tunahamia, na mie mwezi ujao. Ziko wapi? Huo ndio mkwamo.
Transformation nyingi zinazofanyika sasa hivi zinategemea teknolojia. Tungewekeza kwenye hili, hayo mengine yangekuwa historia. Yaani mtu kusafiri na kupeleka barua inatakiwa habari hii ifike mwisho. Mfano tenda na maombi ya kazi hufanywa online. Tujiimarishe kwenye maeneo mengine pia.Kazi nyingi za serikali hazifanyiki kwenye mitandao mkuu hili lazima ulijue