Kwanini Dodoma na si Dar es Salaam?

bnhai

JF-Expert Member
Jul 12, 2009
2,802
2,335
Jibu la kisiasa ni kwamba tunasogeza huduma kwa wananchi. Huduma zipi? Tunasogeza maendeleo kwa wananchi. Kwahiyo baada ya Dodoma tutahamia wapi?

Rais Magufuli anatamani nchi iwe ya asali kwa miezi kadhaa. Hivi karibuni kaanzisha mipango mingi saana yenye gharama kubwa.

Kuna flyovers (sijui zitasalimika maana watu wanahama), kuna mradi wa mwendo kazi Mbagala, ujenzi wa reli wa standard gauge (trillion 16 - budget yetu trillion 29), elimu bure kwa sekondari, kuna ule mradi wa barabara Dar mpaka Chalinze, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu na miradi mingineyo.

Hili la Dodoma ni kuvuruga bajeti bila mpangilio. Mpango huu hata kama upo ukienda kwa taratibu tutapoteza nini? Wafanyakazi wanaambiwa wiki ijayo wawe Dodoma.

Hawa sio mbuzi kwamba hawahitaji kujipanga. Wanafamilia zao. Huu mpango ulivyo kuna ulazima gani wa kuikurupua serikali nzima kwa haraka? Kwanini tusipange. Hivi kipaumbele ni makao makuu au upatikanaji wa maji.
Wananchi wanashirikishwaje katika mipango inayowahusu.

Mheshimiwa mwenye nchi, mipango yenye kukurupuka huvuruga uchumi. Fikiria mwekezaji amekopa na anataka kuweka jengo la ofisi pale Posta. Ghafla unaibuka na mpango mkubwa kama huu.

Ni nani mwenye fikra timilifu atawekeza kwenye viwanda bila kufahamu mipango ya serikali. Nchi hujenga kwa mipango imara na yenye kueleweka.

Dira ya tunapoelekea lazima iwe wazi na ifahamike. Tumerithi mipango mingi saana kutoka tawala zilizopita.

Kuna mipango ya kijamaa ambayo tuliitia kapuni kimya kimya na mengineyo. Teknolojia imebadilika na kurahisisha kila jambo.

Wananchi wanahitaji huduma na sio sura za viongozi wa serikali hapa Dodoma.
 
Unaongelea budget gani mkuu?????. Ile budget ya wabunge wa CCM ni budget hewa. Mkuuu hana tabia ya kufata budget ya bunge. Yeye hufanya anacho amua hata kipind ni wazir pesa za wizara yake zilikuwa zikitumiwa tofaut na bunge lilivyopanga. Sasa kama ndyo amekua mkuu wa nchi ile budget ya CCM ni hewa yeye kila siku atakuwa anakuja na maamuz yake.
 
Unaongelea budget gani mkuu?????. Ile budget ya wabunge wa CCM ni budget hewa. Mkuuu hana tabia ya kufata budget ya bunge. Yeye hufanya anacho amua hata kipind ni wazir pesa za wizara yake zilikuwa zikitumiwa tofaut na bunge lilivyopanga. Sasa kama ndyo amekua mkuu wa nchi ile budget ya CCM ni hewa yeye kila siku atakuwa anakuja na maamuz yake.
Hizi vurugu za kukurupuka zinaumiza kila sekta. Familia na biashara zinahitaji mipango. Watu wanasoma budget na mipango ya serikali ili wafanye mambo yao. Wawekezaji watakimbia. Katika yote anayozungumza haonyeshi kusisitiza suala la ajira kwa vijana. Walikuja na namba ya ajira 70,000+ kisha wakazindua wafanyakazi hewa. Hizi vurugu hapana.
 
Unaongelea budget gani mkuu?????. Ile budget ya wabunge wa CCM ni budget hewa. Mkuuu hana tabia ya kufata budget ya bunge. Yeye hufanya anacho amua hata kipind ni wazir pesa za wizara yake zilikuwa zikitumiwa tofaut na bunge lilivyopanga. Sasa kama ndyo amekua mkuu wa nchi ile budget ya CCM ni hewa yeye kila siku atakuwa anakuja na maamuz yake.
Dah... Ndiyo hasa aina ya kiongozi tunayemtaka kwa wakati huu.... Miaka zaidi ya 50 ya pereteperete tupo palepale... Hebu tujaribu njia nyingine... "Karume Kenge aende shule"
 
Dah... Ndiyo hasa aina ya kiongozi tunayemtaka kwa wakati huu.... Miaka zaidi ya 50 ya pereteperete tupo palepale... Hebu tujaribu njia nyingine... "Karume Kenge aende shule"
Mkuu nchi haijaribiwi. Ni lazima tupange. Tutakwama. Ile budget yenyewe hatujui itatoka wapi. Tumehama kwenye viwanda, tunahamia uwekezaji wa majengo Dodoma.
 
Sijui kwa nini, ukiniuliza sina sababu, lakini hili la Dodoma ninamuunga mkono! Serikali za ccm zote hata ziwe na mipango mizuri vipi utekelezaji wake huwa ni hasara tu kwa taifa! Waende tu tena haraka, na mbeleni huko wauze au wagawe kwa ajili ya matumizi tofauti majengo yaliyokuwa mali za wizara na idara tofauti za serikali jijini! Hii ifanyike ili kuondoa kabisa uwezekano asije akatokea muhuni mwingine akaamua kuirudisha serikali Dar! Hahaaa, wakwende tu huko Dom.
 
Mkuu nchi haijaribiwi. Ni lazima tupange. Tutakwama. Ile budget yenyewe hatujui itatoka wapi. Tumehama kwenye viwanda, tunahamia uwekezaji wa majengo Dodoma.
Dah.. Tumepanga miaka mingapi bana?? Kuna wanamipango wangapi wenye PhD huko serekalini?? Na bado tuko palepale... Mnatutia hasira tu..Muda wa mijadala umeisha Karume kenge lazima aende shule..
 
Huuu mpango wa kwenda dom sio wakubana matumiz hta kidogo ni mpango wa kupiga madeal
 
Mkuu nchi haijaribiwi. Ni lazima tupange. Tutakwama. Ile budget yenyewe hatujui itatoka wapi. Tumehama kwenye viwanda, tunahamia uwekezaji wa majengo Dodoma.
Hiyo mipango miaka 50 imeleta tija gani?

Bora tu risk tukipatia tutafurahi tukishindwa tunachakujifunza kuliko hii statusquo iliyopo Jan to Dec hata template ya budget tangu izaliwe chi haibadiliki
 
Hiyo mipango miaka 50 imeleta tija gani?

Bora tu risk tukipatia tutafurahi tukishindwa tunachakujifunza kuliko hii statusquo iliyopo Jan to Dec hata template ya budget tangu izaliwe chi haibadiliki
Kuhamisha nchi ndio kuleta tija? Yaani mume afanye makosa kwa miaka yote, akizidiwa anabadili mke kuwa ndio kisingizio cha kukwama. Tatizo la Tanzania si yalipo makao makuu. Tunahitaji mtu atakayepanga na kusimamia mipango kwa uadilifu. Bila kupanga ni kazi bure.
 
Hakuna kurudi nyuma wadada wenyewe wameshatangulia Dodoma ina watumishi wa serikali ndio wenye michepuko hii ya mjini kwenu
 
Sijui kwa nini, ukiniuliza sina sababu, lakini hili la Dodoma ninamuunga mkono! Serikali za ccm zote hata ziwe na mipango mizuri vipi utekelezaji wake huwa ni hasara tu kwa taifa! Waende tu tena haraka, na mbeleni huko wauze au wagawe kwa ajili ya matumizi tofauti majengo yaliyokuwa mali za wizara na idara tofauti za serikali jijini! Hii ifanyike ili kuondoa kabisa uwezekano asije akatokea muhuni mwingine akaamua kuirudisha serikali Dar! Hahaaa, wakwende tu huko Dom.
Duh umenifurahisha, ni kweli hakuna sababu zaidi ya makabrasha ya kikao cha baraza la mawaziri cha mwaka 1973. Tunakwendaje huko kwa Matonya? Nauli iko wapi? Tunatengeneza unnecessary uncertainty to businesses and potential investment. It is very hard to script Dr Magufuli's thoughts. With no template, we cannot hold our leaders' accountable. Yaani hatujui mheshimiwa akiibuka atasema nini? Huenda akaamua kufuta flyovers zote. Maana nchi ndio inahama hivyo.
 
Jibu la kisiasa ni kwamba tunasogeza huduma kwa wananchi. Huduma zipi? Tunasogeza maendeleo kwa wananchi. Kwahiyo baada ya Dodoma tutahamia wapi?

Rais Magufuli anatamani nchi iwe ya asali kwa miezi kadhaa. Hivi karibuni kaanzisha mipango mingi saana yenye gharama kubwa.

Kuna flyovers (sijui zitasalimika maana watu wanahama), kuna mradi wa mwendo kazi Mbagala, ujenzi wa reli wa standard gauge (trillion 16 - budget yetu trillion 29), elimu bure kwa sekondari, kuna ule mradi wa barabara Dar mpaka Chalinze, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu na miradi mingineyo.

Hili la Dodoma ni kuvuruga bajeti bila mpangilio. Mpango huu hata kama upo ukienda kwa taratibu tutapoteza nini? Wafanyakazi wanaambiwa wiki ijayo wawe Dodoma.

Hawa sio mbuzi kwamba hawahitaji kujipanga. Wanafamilia zao. Huu mpango ulivyo kuna ulazima gani wa kuikurupua serikali nzima kwa haraka? Kwanini tusipange. Hivi kipaumbele ni makao makuu au upatikanaji wa maji.
Wananchi wanashirikishwaje katika mipango inayowahusu.

Mheshimiwa mwenye nchi, mipango yenye kukurupuka huvuruga uchumi. Fikiria mwekezaji amekopa na anataka kuweka jengo la ofisi pale Posta. Ghafla unaibuka na mpango mkubwa kama huu.

Ni nani mwenye fikra timilifu atawekeza kwenye viwanda bila kufahamu mipango ya serikali. Nchi hujenga kwa mipango imara na yenye kueleweka.

Dira ya tunapoelekea lazima iwe wazi na ifahamike. Tumerithi mipango mingi saana kutoka tawala zilizopita.

Kuna mipango ya kijamaa ambayo tuliitia kapuni kimya kimya na mengineyo. Teknolojia imebadilika na kurahisisha kila jambo.

Wananchi wanahitaji huduma na sio sura za viongozi wa serikali hapa Dodoma.
Alishasema hii nchi ni tajiri..kwa nini hutaki ..yeye unajua hazina kuna shilingi ngapi...kama hutaki kwenda Dom acha kazi vijana wapo wengi sana mtaani wanahitaji ajira
 
Kuhamisha nchi ndio kuleta tija? Yaani mume afanye makosa kwa miaka yote, akizidiwa anabadili mke kuwa ndio kisingizio cha kukwama. Tatizo la Tanzania si yalipo makao makuu. Tunahitaji mtu atakayepanga na kusimamia mipango kwa uadilifu. Bila kupanga ni kazi bure.
Acha kutoka povu basi...mi nimeshahamia Dodoma tayari nacheza na fursa
 
Jamaa wa Dar walizoea kuwaita watanzania wenzao kuwa ni wa mikoani sasa tuone wakifika Dodoma wagogo wakawaita wa mikozi watasemaje. Magufuri awagawaie watumishi viwanja pale Dodoma ili hela walizopiga zamani tuzione pale. Dodoma ikue na Dar Isinyae kidogo na Gesi izalishe umeme Mtwara ndio kilichokuwa kilio chetu. Hatukufurahi Dar kupora makao makuu ya nchi kwa muda wote huo. Kwa vile kuna polisi ila mapema tungeandamana kudai makao makuu Dodoma, Dar Mji gani wa kuamka saa 10 usiku. Watumishi wanaotoa maamuzi na kutengeneza sera wana usingizi ndio maana miaka hamsini ya Dar haikutusaidia.
 
Jibu la kisiasa ni kwamba tunasogeza huduma kwa wananchi. Huduma zipi? Tunasogeza maendeleo kwa wananchi. Kwahiyo baada ya Dodoma tutahamia wapi?

Rais Magufuli anatamani nchi iwe ya asali kwa miezi kadhaa. Hivi karibuni kaanzisha mipango mingi saana yenye gharama kubwa.

Kuna flyovers (sijui zitasalimika maana watu wanahama), kuna mradi wa mwendo kazi Mbagala, ujenzi wa reli wa standard gauge (trillion 16 - budget yetu trillion 29), elimu bure kwa sekondari, kuna ule mradi wa barabara Dar mpaka Chalinze, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa elimu ya juu na miradi mingineyo.

Hili la Dodoma ni kuvuruga bajeti bila mpangilio. Mpango huu hata kama upo ukienda kwa taratibu tutapoteza nini? Wafanyakazi wanaambiwa wiki ijayo wawe Dodoma.

Hawa sio mbuzi kwamba hawahitaji kujipanga. Wanafamilia zao. Huu mpango ulivyo kuna ulazima gani wa kuikurupua serikali nzima kwa haraka? Kwanini tusipange. Hivi kipaumbele ni makao makuu au upatikanaji wa maji.
Wananchi wanashirikishwaje katika mipango inayowahusu.

Mheshimiwa mwenye nchi, mipango yenye kukurupuka huvuruga uchumi. Fikiria mwekezaji amekopa na anataka kuweka jengo la ofisi pale Posta. Ghafla unaibuka na mpango mkubwa kama huu.

Ni nani mwenye fikra timilifu atawekeza kwenye viwanda bila kufahamu mipango ya serikali. Nchi hujenga kwa mipango imara na yenye kueleweka.

Dira ya tunapoelekea lazima iwe wazi na ifahamike. Tumerithi mipango mingi saana kutoka tawala zilizopita.

Kuna mipango ya kijamaa ambayo tuliitia kapuni kimya kimya na mengineyo. Teknolojia imebadilika na kurahisisha kila jambo.

Wananchi wanahitaji huduma na sio sura za viongozi wa serikali hapa Dodoma.
Hivi wewe una akili kichwani?
Hivi mtihani wa darasa la nne ulifaulu kweli?
Hivi mji mkuu wa tanzania ni upi?
 
Dah... Ndiyo hasa aina ya kiongozi tunayemtaka kwa wakati huu.... Miaka zaidi ya 50 ya pereteperete tupo palepale... Hebu tujaribu njia nyingine... "Karume Kenge aende shule"
The 50 yrs of your concern we didn't plan to fail, we failed to plan. Today, your proposal is to go forward without a plan! Kweli wewe una roho mbaya.
 
wakati mwingine kudiriki kushindwa ni kujiingiza kwenye gharama zisizo za lazima. Nchi bado inachangamoto nyingi tu za msingi ;kama kiongozi anahitaji akumbukwe kwamba aliifanyia kitu flani Tanzania ni bora akafuata taratibu na kutokua na haraka ya utekelezaji wa mambo ya msingi anayotaka kuyafanya.


Uku tukiwa bado tunalaumu Sera ya elimu bure kuonekana chanzo cha Sera ya kubana matumizi;linaibuka tena jingine la kuhamia Dodoma. Tunapokwenda hatupafahamu ukweli ndo huo.
 
Back
Top Bottom