Sun is Sun
JF-Expert Member
- Mar 13, 2024
- 1,153
- 1,699
Kwa muda sasa nimekuwa nikitumia mtandao wa Halotel lakini kila ninapohitaji msaada kupitia customer care napata usumbufu mkubwa. Ukipiga simu, unaweza usijibiwe kabisa au ukasubiri hata dakika 10 bila msaada wowote. Ukiandika kupitia mitandao yao ya kijamii wanajibu kwa kuchelewa au kwa ujumbe wa kawaida wa "tutafuatilia" bila majibu ya maana.
Kampuni kama Halotel inayohudumia maelfu ya Watanzania haipaswi kuwa na huduma mbovu kwa wateja kiasi hiki. Huduma kwa mteja ni sehemu muhimu ya mafanikio ya kampuni yoyote lakini hapa ni kama haitiliwi maanani kabisa.
Maswali kwa wanajukwaa:
Ni nani anayewajibika kwa huduma hii duni?
Wengine mmepata changamoto gani na Halotel au kampuni nyingine?
Tunapaswa kufanya nini kama wateja ili kubadili hali hii?
Kampuni kama Halotel inayohudumia maelfu ya Watanzania haipaswi kuwa na huduma mbovu kwa wateja kiasi hiki. Huduma kwa mteja ni sehemu muhimu ya mafanikio ya kampuni yoyote lakini hapa ni kama haitiliwi maanani kabisa.
Maswali kwa wanajukwaa:
Ni nani anayewajibika kwa huduma hii duni?
Wengine mmepata changamoto gani na Halotel au kampuni nyingine?
Tunapaswa kufanya nini kama wateja ili kubadili hali hii?