Christopher H.Bomola
Member
- Nov 10, 2014
- 48
- 19
Toka kuibuliwa kwa hoja ya escrow nimeshangazwa mno na ukimya wa makamanda wa chama chetu CHADEMA kulizungumzia na kulisimamia kidete suala la fedha za escrow?,kama tunavyofanyaga kwenye kashfa nyingine za ufisadi,kama EPA na Richmond,na kilichoniumiza zaidi ni kitendo cha mwenyekiti kuacha suala lililoko mezani yani escrow na kuibua mjadala wa gesi, Je chadema hautaki mjadala huu kwa vile umeibuliwa na msaliti wa chadema?,au ni kweli kuna ukweli kuhusu tuhuma za kambi inayomsapoti zitto kuwa baadhi ya viongozi wakuu upinzani wamo kwenye payroll ya Escrow (ingawa tuhuma hii imekaa kisiasa)..karibuni tujadili wakuu.