Kwanini CCM ya Sasa Imekosa Watetezi kwenye Social Media Mithiri ya Cypirian Musiba na akina Zack wa Twitter?

Bush Dokta

JF-Expert Member
Apr 11, 2023
12,570
21,089
Katika hali ya kushangaza kumetoka aidha mgomo au chama kimekosa Mvuto kabisa.

Wengine wanadai aaah wapi sio kukosa mvuto bali chama hakitoi maokoto kama zamani hivyo watu wanaovutwa na mafumba wamekikacha.

Enzi za huko nyuma tulishuhudia social media zilizobamba kwenye anga la Tanzania.

Walizuka watu binafsi waliofadhiliwa na kujifadhili kukitetea chama (Die Hard Platforms) kwa mbivu na mbichi.

Media za Twitter, Youtube na Facebook kama zote.

Awamu hii naona Kuna Ukame mitandaoni.

Je, shida ni nini?
 
Hakuna Cha kutetea. Maji, umeme, mfumuko wa Bei etc, ndio maana CCM kwa Sasa imejificha kwa makonda.
 
Like siyo kura
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…