Kwanini CCM na CHADEMA tu?

SAU ilikufa nadhani Malima ndiye alikuwa huko lakini akarudi CCM na ukawa mwisho wa SAU kama sijakosea . NI kachama kalikuwa na uislam ile mbaya




hii ni kweli kabisa lakini kuna kachama kamoja nilikuwa na kasikia wanakiita sauti ya umma(sau)
lakini nao sasa wamelala sijui niukata au ni nini
 
Kila nyakati zina mwanzo na mwisho wake kwahy usishangae sana kuna vipindi tofauti
NCCR-MAGEUZI VS CCM (1995)
CUF VS CCM ZENJI (2000)
CHADEMA VS CCM (2010...........
 
SAU ilikufa nadhani Malima ndiye alikuwa huko lakini akarudi CCM na ukawa mwisho wa SAU kama sijakosea . NI kachama kalikuwa na uislam ile mbaya

Malima alikuwa NRA ambacho mwanzilishi wake ni Urutu Abubabari Urutu
 
hapo kwenye red mbona hiko chama sijawahi kukisikia?
 
Hata kama vipo katika ndoa lazima CUF japo isikike basi kinafanya nini ndani ya ndoa, maana tunaisikia tuu CCM, kumbuka katika ndoa kila upande unawajibu wake
Inawezekana ni ndoa ya kikristo hivyo CUF ni mwanamke hawezi fanya kitu anatekeleza maagizo ya KICHWA ambayo ni CCM hii imetulia hata kama anaumia shuruti amuone Padre au mchungaji ha ha ha hii imetulia.
 
siku lazima kuwe na juu na chini.haiwezekani vitu vyote vikawa juu au chini.vyama vya siasa hivyo hivyo kuna ambavyo matendo yake yanavutia wananchi huku vingine vikionekana kama muunganiko wa wasanii.ccm ni chama tawala hivyo lazima kiongelewe sana.Chadema licha ya kuwa chama kikuu cha upinzani lakini matendo yake na sera zake zina mashiko kwa wengi wa watanzania hivyo kuwa na shauku ya kujua mengi kuliko vyama vingine kama Tlp ambacho ni chama cha mtu binafsi au CUF bi mdogo wa ccm au hata Nccr-mageuzi asiyejitambua hata kama ni mpinzani wa nini maana anapingana mpaka na wapinzani wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…