sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Hali inayoendelea katika chaguzi za CCM ni ushahidi tosha kuwa sasa chama kimekosa dira na mwelekeo.Makada waaminifu kama mzee Kingunge amesema cha kimepoteza taswira na kuwa chama cha wenye pesa,Mh. Sumaye alisema chama hiki bila kutoa rushwa huwezi kupata uongozi na vijana nao wanatwangana viti na kutuhumiana kupokea rushwa.
Kama madhumuni ya chama yamegeuka na chama kukubali kutumia nguvu kubwa ya kifedha ili kujikita kiuongozi tuna haja gani ya kuwa na chama kama hiki.Chama kimekuwa pango la wanyang'anyi kwa kupora rasilimali za taifa.
Ukiangalia safu yake ya uongozi kuelekea uchaguzi wa 2015 napata wasiwasi kama lengo lao ni madaraka au kuna zaidi ya madaraka.Huwezi leo hii kumchagua mjumbe wa NEC ilihali kiongozi huyo na sifa za ujambazi kisha ukajinadi umejipanga kimkakati,wasiwasi wetu kama nchi inakabidhiwa kwa majambazi basi ujue wanyonge hawana pa kukimbilia.
Kama kweli CCM inataka kusimama imara ni fursa muhimu kukifanyia reform ili kuwakimbiza wezi na mafisadi ambao wameifikisha nchi hapa tulipo.Hatuwezi kuwa na chama kinachowagawa Watanzania kwa misingi ya udini na ukabila tuka baki salama.Hta mwalimu aliwahi kusema dhambi hii ya ubaguzi tukiacha ikapita itatutafuna wote.CCM ya mwalimu ilijali maadili na heshima ya kuthamini utu wa mtu kinyume na CCM ya leo inayo uza utu wa mtu kwa kuwafukuza juu ya ardhi yao na kuwakabidhi wakoloni wa kigeni.
Chama kinahitaji wa kina Kolimba ambao wanaweza kuwaeleza ukweli na kuwakosoa viongozi viwavi wa madaraka katika kutafuna keki ya taifa.Wananchi hatuwezi kufanya mbuzi wa kafara kila unapofika uchaguzi kwa kuhongwa ili kuuza utu na haki yetu kwa bei isiyotosha kununua hata pipi.Reformation kwa CCM ndiyo njia pekee ya kukinusuru angalu 2015 kiwekambi rasmi ya upinzani,vinginevyo kitapoteza hata hiyo nafasi ya upendeleo.
Kama madhumuni ya chama yamegeuka na chama kukubali kutumia nguvu kubwa ya kifedha ili kujikita kiuongozi tuna haja gani ya kuwa na chama kama hiki.Chama kimekuwa pango la wanyang'anyi kwa kupora rasilimali za taifa.
Ukiangalia safu yake ya uongozi kuelekea uchaguzi wa 2015 napata wasiwasi kama lengo lao ni madaraka au kuna zaidi ya madaraka.Huwezi leo hii kumchagua mjumbe wa NEC ilihali kiongozi huyo na sifa za ujambazi kisha ukajinadi umejipanga kimkakati,wasiwasi wetu kama nchi inakabidhiwa kwa majambazi basi ujue wanyonge hawana pa kukimbilia.
Kama kweli CCM inataka kusimama imara ni fursa muhimu kukifanyia reform ili kuwakimbiza wezi na mafisadi ambao wameifikisha nchi hapa tulipo.Hatuwezi kuwa na chama kinachowagawa Watanzania kwa misingi ya udini na ukabila tuka baki salama.Hta mwalimu aliwahi kusema dhambi hii ya ubaguzi tukiacha ikapita itatutafuna wote.CCM ya mwalimu ilijali maadili na heshima ya kuthamini utu wa mtu kinyume na CCM ya leo inayo uza utu wa mtu kwa kuwafukuza juu ya ardhi yao na kuwakabidhi wakoloni wa kigeni.
Chama kinahitaji wa kina Kolimba ambao wanaweza kuwaeleza ukweli na kuwakosoa viongozi viwavi wa madaraka katika kutafuna keki ya taifa.Wananchi hatuwezi kufanya mbuzi wa kafara kila unapofika uchaguzi kwa kuhongwa ili kuuza utu na haki yetu kwa bei isiyotosha kununua hata pipi.Reformation kwa CCM ndiyo njia pekee ya kukinusuru angalu 2015 kiwekambi rasmi ya upinzani,vinginevyo kitapoteza hata hiyo nafasi ya upendeleo.