Kwanini ccm hawapendi usafiri wa reli

Kwanini ccm hawapendi usafiri wa reli

Trezo

Member
Joined
Aug 24, 2014
Posts
54
Reaction score
14
Muda mrefu sana Reli zote tatu kubwa na zenye kuweza kuinua uchumi wa nchi na bado ikatoa ajira kwa vijana wengi wa Tanzania lakini chama chetu cha mapinduzi kimeshindwa kuendeleza mradi huu matokeo yake reli ya Tanga na Moshi ni kama mabaki ya kale imebaki historia mashuleni.
Nauliza tuu ni kwamba hatuna uchungu na hii reli au madhumuni ya kujenga reli yalishatimia na hakuna tena biashara ya utumwa tena ndo maana ccm wameamua kuipotezea.Nitaandaa mjadala wa kitaifa kuona ni jinsi gani ajali za barabarani zinavyomaliza ndugu zetu kwa kasi ya ajabu,lakini tungekuwa na usafiri wa treni watu wangejichagulia aina ya usafiri wanaotaka.mimi binafsi napenda sana usafiri wa treni.
 
Ni hivi,suala la usafiri wa reli na watawala lina mgongano wa kimaslahi mdau,na ni kwamba watawala wengi wanamiliki malori,matajiri wengi wanamiliki malori na ni wafadhili wa SOSOEM,
Kihistoria reli imesaidia uchumi wa nchi kubwa mbalimbali(Germany,Belgium,Uk and US).
Jamaa nachoona hawatak kuihuisha reli kwa sababu itaharibu mipango yao ya kibiashara
 
Ukiongozwa na wasio na maono utaishia kulalamika kila siku! Hakuna visionally leader katika CCM ya leo! wengi wamebaki kuwa wasaka tonge tu including huo mkuu wenu wa nchi!

Nchi zote ulimwenguni tena zaidi zile ambazo zimeendele zinathamini na ziimeimarisha usafiri wa reli na anga. Siyo kwamba hawana barabara za lami, wanazo nyingi na nzuri sana kuliko sisi huku wadengereko! Lakini cha ajabu wanauthamini sana huu usafiri wa reli! Hii ni kutokana na sababu za kiuchumi kwamba usafiri wa reli kiuchumi ni nafuu kwa wananchi na serikali kwa ujumla wake. Leo hii chanzo moja wapo ya mfumko wa bei za bidhaa na hata chakula unatokana kuongezeka kwa gharama za usafirishaji.

Huku kwetu umatumbini ambako ndiko tumejaa hohe hae ndio kwaanza hatuna hata mpango wa kuuboresha reli zilizopo achilia mbali kujenga mpya! Tatizo hatuna viongozi wanaotamani kuleta maendeleo ya nchi, tuna aina ya viongozi wananotamani kuendeleza vifamilia vyao huku wakiwaacha waliowachagua waishi wajuavyo wenyenwe!

TUSILALAMIKE, TUCHUKUE HATUA, TUBADILISHE UONGOZI KAMA HATUA YA AWALI YA KULETA MABADILIKO KATIKA NCHI YETU! OTHERWISE WE WILL ALWAYS BE IN THIS COMMOTION!
 
1. Biashara za mafuta ya magari (petrol, diesel nk) zinamilikiwa na makada na mafisadi wa ccm

2. Maloli ya mizigo na makampuni ya usafiri wa mabasi wamiliki wake wakubwa ni makada wa ccm na familia zao

3. Usafiri wa treni hushusha bei za bidhaa nakuathiri mapato na faida kubwa kwa mafisadi hasa makada wa ccm na familia zao

Hivyo njia pekee ya kuendeleza ushenzii kwa kuwanyonya watanzania nikuharibu kabisa mifumo ya huduma

zinazomilikiwa na umma kama Reli, shilika la Ndege la Taifa, kilimo, meli nk.

Wachawi na wahalifu wa hii mifumo ni ccm na ufisadi ndani ya serikali
 
Kuhusu ajali ni mipango ya mungu...ata iyo tren inaweza ikateketeza watu na pengne ukaona bora hata usafiri mwingne...
 
Observation nzuri hii mkuu, kiukweli kama reli ingekuwa inatumika kikamilifu yaani hata lifespan ya barabara zetu ingeongezekana maana barabara zinatengenezwa 2008 kufikia 2011 zinatengenezwa upya tena
 
hawapendi usafiri wa reli kwa sababu malori yanawasaidia kusomba watu na kuwapeleka kwenye mikutano yao ..ccm ni wapuuzi sana
 
Wengi wao ni wamiliki wa malori makubwa, sasa treni ikibeba mizigo mikubwa wao wale wapi? Chezea madisadi wewe!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Na wenye malori ndio walio haribu reli kwa kuzingowa
 
Back
Top Bottom