Kwanini binadamu tunaogopa KIFO?

dumbi

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2018
Posts
988
Reaction score
1,545
Habari zenu wakuu?leo nilikiwa nafkiria kuhusu kifo nikawa najiuliza hilo swali hapo juu,kwanini watu hawazoei kifo ingawa ni jambo ambalo huwa linatokea kila siku katika jamii?
Mtu unazaliwa mpaka unakua unasikia habari za watu kufa kwa namna moja au nyingine wakiwa watoto vijana na wazee hakichagui umri wengine ni watu wa karibu yako lakini bado hauzoei.

Kuna msemo unasema kila nafsi itaonja mauti na wengi wanalijua hili kwamba lazima tufe hata tufanyeje, ukiiishi kwa wema utakufa ukiishi kwa ubaya utakufa, ukiwa maskini utakufa ukiwa tajiri utakufa sasa kwanini tunaogopa wakati hiki kifo hakiepukiki?inafikia muda watu huogopa kudai haki zao za msingi kwa kutishiwa kuuwawa wakati anajua atakufa tu!
Hiki kifo kinatumiwa kama silaha na watawala kufanya mambo yao bila ya tabu.

kwanini wanapokufa watu wetu wa karibu huwa tunalalamika na kuhuzunika?
Kama wapo wasioogopa kifo au kuondokewa na jamaa zao nadhani dunia nzima hawazidi %5

sasa swali langu ni hilo kwanini hiki kifo hakizoeleki?
Je kwasababu ya kutopewa elimu juu ya jambo hili au elimu inayotolewa ni ya kubahatisha yani hao wanayoifundisha hawana uhakika na wanalosema?
mwisho tufanyeje ili tukizoee kifo tusikiogope?

karibuni wote tujadili wenye kuamini Mungu yupo na wasio amini uwepo wake,wenye dini na msio na dini karibuni sana.
 
Kutokumuona binadamu mwenzio tena hii ni simanzi kubwa
 
Nafikiri mtoa mada case study yako umeangalia kwa upande wa afrika tu ambapo asilimia kubwa kufa ni jambo lisilozoeleka na tukio hilo umbatana na vilio vya kutosha. Kwa baadhi ya nchi za wenzetu ni tofauti kidogo msiba unaweza kutokea kwa Jirani usisikie fyuuu wala fyeee bali ni kimya kimya mpaka anapopumzishwa kwenye nyumba yake ya milele. Nafikiri issue kubwa ni uelewa na watu wanavyoperceive hilo tukio.
 
Ila trust me hatutaenda kokote mkuu Bali tunapokufa tunakuwa non-existed kama tunavyokuwa wakati hatujazaliwa.
Sijui kwa nini watu wanashindwa kuelewa hii

Ukifa unarud ulikotoka, ulipozaliwa ulikuwa wapi? non existance, so ukifa unakuwa non existance too

mfano mzuri ni ukilala usiku, huwa unakuwa wapi??
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…