Katika maswala ya uumbaji wa binadamu jinsi anavyoelezwa kwenye vitabu vya Mungu kwamba binadam aliumbwa kwa udongo hii hoja ni kweli kabisa.
Hii hoja ni sahihi kwa sababu ya kwamba mwili wa binadamu ni udongo kutokana vyakula na Oksijeni anavyotumia katika maisha yake inatokana na mimea ambayo maisha yake kwa asilimia kubwa inategemea udongo.
Kwahiyo; Ng'ombe, kuku, na wanyama wote wanaoliwa nyama zao ni udongo.
Kwa hiyo mmea umesimama kama mashine ya kuchota kile kinachofaa kwenye udongo na kukitegeneza ili kiweze kujenga na kutegeneza mwili wa binadam kwa taratibu maalum.
Wadau na Wanasayansi wa JF, Hivi ni kweli hakuna uwezekano wa kutengeneza mwili wa binadamu kwa kutumia virutubisho muhumu vinavyopatikana kwenye vyakula tunavyokula.
Mungu alituumba kwa mfano wake, why tusiweze kuuumba na sisi mwili wa binadamu?
Nawasilisha.