Kwanini Benjamin Sitta anautaka umeya kwa nguvu zote? Kuna nini nyuma yake?

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,449
Huyu jamaa Benjamin Sitta ni diwani wa kata ya Msasani, kabla ya uchaguzi wa ndani wa vyama huyu jamaa hakuwa anakubalika hata na chama chake kabisa, ipo wazi na anajua hilo, ila sijui ilikuwaje hadi akapitishwa yeye? Mi na wewe hatujui lakini pia baada ya kupitishwa akapata upinzani mkali kutoka UKAWA, kulikuwa na wagombea wawili wenye nguvu sana wa CUF na CHADEMA ambapo CUF ilikuwa na mzee maarufu lakini haijajijenga kichama, huku CHADEMA kukiwa na kijana aliyejiwekea mizizi miaka mitano nyuma ila ndani ya chama chake kukiwa na makundi ya wanaomtaka na wasiomtaka, hatimaye likapita jina lake.

Sasa hapo ndipo kukatokea sintofahamu kubwa, CUF hawataki kuachia kata na CHADEMA hawataki kuachia kata,na hili kosa namlaumu sana Halima Mdee (mbunge wa Kawe) ikatokea kipindi chote cha kampeni yule mzee wa CUF akaenda kuhiji huko Maka, huku mwenzie Ben Sitta akimaliza mitaa kwa kampeni (sisemi alivyokuwa anatoa, ila Mungu anajua na yeye anajua) baada ya hapo ndipo CHADEMA wakaanza kufanya kampeni kimyakimya kuona mwenzao wa CUF hayupo, mgombea wa CHADEMA hakuondoa jina lake NEC kwa hiyo kata ikawa na wagombea watatu(CCM, CUF na CHADEMA)

Ila taarifa za huyu Ben Sita kuutaka Umeya zilikwepo kabla ya uchaguzi, ikasemekana jamaa anautaka Umeya wa Kinondoni na wala shida si Udiwani zilienea sana hizi taarifa hatimaye sasa imetimia na hata wagombea wa UKAWA zikaenea taarifa kwamba jamaa ndie aliyewagawa ili apite kiuraini kwa sababu bila CUF na CHADEMA kuweka wagombea wote basi Ben sitta Udiwani aliusikia kwenye bomba maana zile kura za CUF na CHADEMA ukizichanganya CCM waliachwa mbali, sasa maswali ya kujiuliza ni je kwanini huyu jamaa anautaka umeya wa Kinondoni sana? Au ndio harakati za kuutaka ubunge wa Kinondoni 2020? Au kuna ajenda gani kubwa kwake?
 
Ametumwa na uchwara......

We ukusikia lile zuio la kurusha tukio la matokeo ilikuwa ni maagizo kutoka juu?......
 
Usiulize maswali utafukua makaburi, na mwishowe utataka kujua kwanini meya mstaafu katangulia mbele ya haki, kwanini dart, kwanini uda, kwanini,, kwanini siyo nzuri kaa kimya...
 
Huyu jamaa Benjamin Sitta ni diwani wa kata ya Msasani, kabla ya uchaguzi wa ndani wa vyama huyu jamaa hakuwa anakubalika hata na chama chake kabisa, ipo wazi na anajua hilo, ila sijui ilikuwaje hadi akapitishwa yeye? Mi na wewe hatujui lakini pia baada ya kupitishwa akapata upinzani mkali kutoka UKAWA, kulikuwa na wagombea wawili wenye nguvu sana wa CUF na CHADEMA ambapo CUF ilikuwa na mzee maarufu lakini haijajijenga kichama, huku CHADEMA kukiwa na kijana aliyejiwekea mizizi miaka mitano nyuma ila ndani ya chama chake kukiwa na makundi ya wanaomtaka na wasiomtaka, hatimaye likapita jina lake.

Sasa hapo ndipo kukatokea sintofahamu kubwa, CUF hawataki kuachia kata na CHADEMA hawataki kuachia kata,na hili kosa namlaumu sana Halima Mdee (mbunge wa Kawe) ikatokea kipindi chote cha kampeni yule mzee wa CUF akaenda kuhiji huko Maka, huku mwenzie Ben Sitta akimaliza mitaa kwa kampeni (sisemi alivyokuwa anatoa, ila Mungu anajua na yeye anajua) baada ya hapo ndipo CHADEMA wakaanza kufanya kampeni kimyakimya kuona mwenzao wa CUF hayupo, mgombea wa CHADEMA hakuondoa jina lake NEC kwa hiyo kata ikawa na wagombea watatu(CCM, CUF na CHADEMA)

Ila taarifa za huyu Ben Sita kuutaka Umeya zilikwepo kabla ya uchaguzi, ikasemekana jamaa anautaka Umeya wa Kinondoni na wala shida si Udiwani zilienea sana hizi taarifa hatimaye sasa imetimia na hata wagombea wa UKAWA zikaenea taarifa kwamba jamaa ndie aliyewagawa ili apite kiuraini kwa sababu bila CUF na CHADEMA kuweka wagombea wote basi Ben sitta Udiwani aliusikia kwenye bomba maana zile kura za CUF na CHADEMA ukizichanganya CCM waliachwa mbali, sasa maswali ya kujiuliza ni je kwanini huyu jamaa anautaka umeya wa Kinondoni sana? Au ndio harakati za kuutaka ubunge wa Kinondoni 2020? Au kuna ajenda gani kubwa kwake?
Andiko lako limejaa dhana na chuki binafsi,kila mtu ana haki ya kugombea nafasi za kisiasa
 
Mimi ningeweza kukujibu kwa ufupi, kufikia hatua fulani katika maisha ni njozi. Na ukisimama kwa kujiamini katika kufikia lengo hilo unafanikiwa. Kama ni kijana ni lazima uwe na malengo tangu mapema unataka kuwa nani katika maisha yako. Ukifanikiwa asiwepo wa kukuuliza sababu ndiyo malengo yako. Malengo ya Sitta ni kuwa akifanikiwa lazima awe Meya na amekuwa, tunashukuru hakusema Nikiwa Diwani lazima niwe kibaka. Nasasa amekuwa Meya lazima awe na malengo mengine ikiwezekana Uwaziri Mkuu
 
kwa ule usanii uliofanyika juzi nimeamini mtoto wa nyoka ni nyoka...
baba yake huyo jamaa alifanya usanii kwenye bunge la katiba kwa kufosi kuwapigisha kura wajumbe wengi feki ili mradi tu hiyo katiba yao feki ipite, huyu jamaa naye kwenye uchaguzi wake wanatolewa wajumbe halali wa upinzani na kuchomekwa wajumbe wao feki ili mradi tu kura zao zitoshe...
tuna safari ndefu.
 
Rais Magufuli ndiye yuko nyuma ya hii kasheshe. kumbuka mzee situmai ni rafki wa jpm hivyo uzandiki wote anaujua tu
 
Usiulize maswali utafukua makaburi, na mwishowe utataka kujua kwanini meya mstaafu katangulia mbele ya haki, kwanini dart, kwanini uda, kwanini,, kwanini siyo nzuri kaa kimya...
Hilo la Meya wa jiji mstaafu na kutangulia kwenye haki v/s DART and UDA linataka thread yake ya kiuchunguzi kabisa.
Ila la Emmanuel yaweza kuwa baada ya mzee kuugua wanataka wamuenzi kabisa kijana huku mzee anaona sio kusubiri kama Mlingwa
 
Back
Top Bottom