Kwanini baada ya kuoana tumeachana?


Sidhani kama inawezekana kuishi pamoja miaka 8 halafu muwe mnaishi kwa aina ya mimi na sio sisi

Mtakuwa mmezaa na huduma zote zinafanyika kama wanandoa kinachokosekana hapo ni ile hati tu ambayo ndio kisheria inawafanya nyie kuwa wanandoa lakini kijamii nyie tayari ni wanandoa

Swali ni kuwa baada ya kudshirikiana yote hayo kwa muda wote huo,inakuwaje baada ya kuipata ile hati ambayo inatutambulisha kisheria kuwa ni wanandoa ndoa inatushinda?
 

Kwa watu wengi ndoa ni zaidi ya hati.
Nina rafiki yangu aliolewa, ila kama kawaida alishakutana kimwili na jamaa mara kibao, alikuwa anaenda kwa jamaa anakaa wanapika na kupakua...lakini cha ajabu akanambia kuwa siku ya harusi alikuwa anatetemeka, alikuwa anawaza wakifika room itakuaje, na akanambia siku ile alihisi tofauti wakati wanamake love...

So huo ni mfano tu wa matumaini walonayo watu kabla ya kufunga ndoa, tena wanayakuza matumaini haya kisaikolojia na wanataka yatokee katika nyanja zote....yani katika kupanga matumizi basi mtu anaona akishaoa tena basi ajue mshahara wa mkewe au mumewe wote unaishia wapi..
Kama mume mlevi basi mke anajipa moyo kuwa baada ya ndoa ataacha na atakuwa anawahi kurudi nyumbani...
Kama mchepukaji basi mtu atavumilia akiamini baada ya ndoa ataacha....!

Kwa watu wengi ndoa ni zaidi ya makaratasi!
 
Kukosea kuchagua, kufata vitu fulani vipendezavyo moyo, tamaa, kutoridhika na hali ya mwenzako, fitina, vyote hivi vinachangia ndoa kuvunjika mapema baada ya kufungwa
 
Mi naona watu wakishafunga ndoa wanaona wameshakula viapo kila mmoja anajiachia atakavyo, hamna anaeogopa tena kuachwa.Uvumilivu ukikosekana apo ndio kuachana kunafuata.Hii inakua tofauti na pale ambapo bado hamjapata vyeti vya kuhalalishwa kila mmoja anakua na uoga flani.
 

Kama mtu amekuwa mlevi kwa miaka 8 halafu utarajie mkifunga bdoa atabadilika ni tatizo kubwa sana

Inawezekana tatizo linaloonekana hapa ni la kisaikolojia zaidi

Mtu mlikuwa mnapakuana kila leo halafu siku ya ndoa unaogopa

Unaogopa nini sasa?

Ai ile kwamba "huu sasa ni mzigo wangu hadi kifo"?
 

Kwahiyo unajichunga kwa iaka 8 halafu baada ya ndoa tu unafungulia!?
 

Nafikiri hilo ndo jibu, labda kabla ya ndoa mtu alikuwa anawaza kuwa wanaweza kuachana muda wowote, na ukishakuwa na mawazo hayo huwezi kuwa responsible asilimia zote kwa mwenzio kwa sababu unawaza anythig can happen, at any time...

Ila baada ya ndoa unawaza huyu tena ndo wangu, hadi kifo...unajifeel responsible kwake...sasa hapa hata yale mapungufu yake utayaona...chongo utaliona chongo wala si kengeza tena....!

Watu wengi na mimi nikiwemo tunaamini ndoa ni "nchi ya maziwa na asali"
 
Tatizo mi naona miaka ya hivi karibuni tumekosa hofu ya mungu..kukurupuka kwenye maamuzi unakuta mtu anaamua kuolewa ili alipe fadhila...mwingine amekurupuka tu kutokana umri umemfika kwahyo unakuta anataka aolewe faster mwisho wa siku wakiingia kwenye ndoa wanachoka kwa sababu hakuna true love iliyowaunganisha...! Sababu ingine uaminifu kwenye ndoa umekosekana sikuhizi hii michepuko inaleta hasira sana kwenye ndoa.inafikia kufanya ndoa nyingi kuvunjika
 
Aisee .....!!

Surely, kuna ndugu yangu aliishi na mwanaume miaka kama kumi bila ndoa.Walikua na migogoro ya kawaida tu.Baada ya kufunga ndoa migogoro ikawa mikubwa zaidi ingawa hawajaachana.Af kwenye ile thread yako nyingine( ya kusifiwa) mbona umekataa kunielewesha.
 

Aisee ......

Unadhani matarajio ndio tatizo pekee kwenye jambo hili na hakuna kingine ambacho kibafanya watu ambao wameishi kwa amani na utulivu kwa miaka zaidi ya 7 na kuja kuachana muda mfupi tu baada ya kufunga ndoa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…