Kwanini abiria wa Mabasi tunanyanyasika hivi?

Kwanini abiria wa Mabasi tunanyanyasika hivi?

ganjaone

Member
Joined
Aug 17, 2014
Posts
22
Reaction score
2
binafsi nakerwa sana na hii tabia ya wamiliki wa mabasi haswa mikoani.abiria mnalipa nauli halali kabisa ila inapotokea gari limeharibika njiani siku zote abiria tunanyanyasika sana.wahusika wanakuwa na majibu ya hovyo na kutoa taarifa za uongo bila kujali kuwa kila mtu anajali shughuri zake na wakati.

kwanini gari linapoharibika hawa watu hawataki kurudisha kiasi flani cha nauli ili pande zote zipate haki?mnashindwa kuwatafutia watu usafiri mbadala basi rudisheni kiasi cha nauli ili kufidia safari iliyobaki kwa kila abiria.kwanini sisi wasafiri ndio tuingie hasara kila siku?maisha magumu na nyinyi mnazidi kutukandamiza.kuna umuhimu wa kuwa na sheria ya kuwalinda maslahi ya wasafiri.BASI LA ALLY'S urambo to mwanza mlichotufanyia jana hakifai kuigwa.
 
Pole sana mkuu.
Naona umekasirika mbaya mpaka unataka kujidhuru!!!.
 
binafsi nakerwa sana na hii tabia ya wamiliki wa mabasi haswa mikoani.abiria mnalipa nauli halali kabisa ila inapotokea gari limeharibika njiani siku zote abiria tunanyanyasika sana.wahusika wanakuwa na majibu ya hovyo na kutoa taarifa za uongo bila kujali kuwa kila mtu anajali shughuri zake na wakati.

kwanini gari linapoharibika hawa watu hawataki kurudisha kiasi flani cha nauli ili pande zote zipate haki?mnashindwa kuwatafutia watu usafiri mbadala basi rudisheni kiasi cha nauli ili kufidia safari iliyobaki kwa kila abiria.kwanini sisi wasafiri ndio tuingie hasara kila siku?maisha magumu na nyinyi mnazidi kutukandamiza.kuna umuhimu wa kuwa na sheria ya kuwalinda maslahi ya wasafiri.BASI LA ALLY'S urambo to mwanza mlichotufanyia jana hakifai kuigwa.


Pole sana, hiyo yote inatokana na mamlaka husika kuwekwa mifukoni mwa wamiliki wa hayo mabasi, na kama wangekuwa ni waadilifu basi wangetumia taarifa hizi kuwachukulia hatua stahiki, lakini kwakuwa nchi hii inakwenda iendavyo, basi tu ndugu yangu amini kuwa ipo siku Mungu atawalipa sawia na matendo yao
 
Pole sana, hiyo yote inatokana na mamlaka husika kuwekwa mifukoni mwa wamiliki wa hayo mabasi, na kama wangekuwa ni waadilifu basi wangetumia taarifa hizi kuwachukulia hatua stahiki, lakini kwakuwa nchi hii inakwenda iendavyo, basi tu ndugu yangu amini kuwa ipo siku Mungu atawalipa sawia na matendo yao


Ni ukweli japo mchungu sana kumeza.
 
naweza kutofautiana na mawazo marxlups kidogo. Mamlaka inayoshughulikia hiyo mambo ni SUMATRA na hawa jamaa hawana longo longo wala nini. Abiria akichelewesha safari kwa zaidi ya saa tatu mfululizo mwenye basi anawajibika kurudisha au kumtafutia usafiri mbadala kama basi limeharibika. Anyways , watakuja tuu kutupa maelekezo lakini nahisi wewe utakua hata tiketi huna, maana kila mikoa hawa jamaa wana ofisi zao, nakumbuka Green Star walifungiwa na faini lukuki juu
 
Back
Top Bottom