Kwani ukimaliza chuo ni lazima uote Kitambi

Kwani ukimaliza chuo ni lazima uote Kitambi

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2012
Posts
3,401
Reaction score
1,618
Asante Mungu kwa hii siku nyingine, leo MCHUNGUZI HURU na kuja na uchunguzi mwingine.......

Vijana wengi wa kitanzania (wa kiume) yaani baada ya kumaliza tu chuo unakuta wameota vitambi, utakuta kijana ulikuwa ukisoma nae chuo alikuwa yupo kama Kagame lakini baada ya kumaliza chuo unakutana nae unaanza kuhisi umemfananisha au ni yeye. Shida ni nini wadau?

Na si ana hela, hapana, utakuta anafanya volunteering somewhere halipwi chochote hata nauli tu lakini bado kitambi kinamuota au mwingine hana kazi kabisa lakini ana bonge la tumbo. Kuna siri gani nyuma ya vitambi na kumaliza chuo?

Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)
 
Last edited by a moderator:
Asante Mungu kwa hii siku nyingine, leo MCHUNGUZI HURU na kuja na uchunguzi mwingine.......

Vijana wengi wa kitanzania (wa kiume) yaani baada ya kumaliza tu chuo unakuta wameota vitambi, utakuta kijana ulikuwa ukisoma nae chuo alikuwa yupo kama Kagame lakini baada ya kumaliza chuo unakutana nae unaanza kuhisi umemfananisha au ni yeye. Shida ni nini wadau?

Na si ana hela, hapana, utakuta anafanya volunteering somewhere halipwi chochote hata nauli tu lakini bado kitambi kinamuota au mwingine hana kazi kabisa lakini ana bonge la tumbo. Kuna siri gani nyuma ya vitambi na kumaliza chuo?

Dr. MCHUNGUZI HURU (PhD)

Mkuu Kote Umenikuna ILA Kwa Kumtaja Na Kumtumia Kama Mfano Hasi My Role Model Paul Kagame NIMESIKITIKA. Na Nasusa Sichangii..............( Just Kidding ). Uzi Umetulia Japo Nahisi Kama Vile Unatulenga Wengi Wetu Humu JF!
 
Mtoa mada naungana nawewe kwa 100%. Hata mie kimekuja hata sina kazi maaulumu. Nadhani akili ikiwa imetulia kidogo ndio sababu maana kupiga msuli sio kitu cha masihara eti.
 
Stess za course work, test, UE, madesa, sup, disco....!

Stress za bum, unachelewa kupewa na ukipewa ndani ya wiki tatu lishakata....

Kwa kulala pia stress...umebebwa hostel....kitanda cha futi tatu mnalala wawili...tena ukute ni mishababi ya nguvu...ukilala hata ndoto nzuri huoti....!

Bado hujapiga pasi ndefuu.....hatariii

Hapo stress za mapenzi weka pembeni...

Acha tu watoke vitambi....
 
kuna baadhi ya wakaka tulimaliza nao.....................

nikikutana nao wana vitambi hao siku hizi
 
Mkuu Kote Umenikuna ILA Kwa Kumtaja Na Kumtumia Kama Mfano Hasi My Role Model Paul Kagame NIMESIKITIKA. Na Nasusa Sichangii..............( Just Kidding ). Uzi Umetulia Japo Nahisi Kama Vile Unatulenga Wengi Wetu Humu JF!

Hapo Kwa KAGAME NAKUUNGA MGUU KABISA.
 
Mimi namuanga mkono mtoa mada,japo uchunguzi wake hujakamilika kutokana nakutofanya uchunguz akinifu ili apatekujua sababu ni nn,lakin hata mm hilo suala nimeliona kwa vijana wengi baada ya kuhtmu vyuo wanaleta vtambi baada ya muda mfupi
 
KIRIBA TUMBO ni utapia mlo kama utapia mlo mwingine wowote. Binafsi naona ni aibu hasa kwa KIJANA kuwa na kiriba tumbo (Kitambi)....... what a mess!!!!!

Tuchunge tunachokula na kunywa.
1. Kama unapenda sana kula na kunywa upende na mazoezi
2. Kama hupendi mazoezi basi jichunge ulaji na unywaji wako (Biere)

Vinginevyo... Sio afya kuwa na Kitambi.
 
Samahan MCHUNGUZI HURU , hivi kitambi ni kitu kizuri au kibaya?
 
hahahahahaa maada inanihusu mdau, hadi naona mwili sio wangu, nishajiuliza sana, nilichokigundua mimi na kupumzika kutokana na stress vitisho vya chuo.
 
KIRIBA TUMBO ni utapia mlo kama utapia mlo mwingine wowote. Binafsi naona ni aibu hasa kwa KIJANA kuwa na kiriba tumbo (Kitambi)....... what a mess!!!!!

Tuchunge tunachokula na kunywa.
1. Kama unapenda sana kula na kunywa upende na mazoezi
2. Kama hupendi mazoezi basi jichunge ulaji na unywaji wako (Biere)

Vinginevyo... Sio afya kuwa na Kitambi.

kweli mkuu vijana wengi tuna tabia ya kutopenda mazoez..Mimi huwa baada ya mishemishe huwa nakimbia jioni saa 1,sasa huwa nawaomba company vijana wahapa kitaa tukimbie nao wote wavivu..kitambi kwa kijana kibaya sana na ntakikataa milele..
 
Uko sahihi...
ila hii yote ni kurelax au kujiachia baada ya kutoka JELA ya kuwa chini ya maelekezio yanayokuweka kwenye hali ya kutokua na uhuru wa kujiamulia.

Maisha ya Chuo ni maisha ya utumwa wa kukutengenezea maisha ya mbele ambayo huna halkika nayo kama yatakua mazuri au yakawaida. Hapo lazima uchoke masomo plus uhuru wa kupimiwa......
 
Samahan MCHUNGUZI HURU , hivi kitambi ni kitu kizuri au kibaya?

Kitambi ni aina ya malnutrition, yaani mtu ame-over feed, hivyo chakula cha ziada ambacho hakina kazi kutokana na mwili kuhitaji kiwango flani tu so kinachobaki kinamfanya mtu aote kitambi(obesity) au anenepe bila formula.
 
Mi mbona miaka kibao na hata dalili ya kitambi sina...au nirudi tena chuo
 
To most of people ni psychological zaidi....kuwa huru kuondokana na stress za mitihani supu disco 😛lane::flypig::israel::israel::lock1:
 
Back
Top Bottom