Von zelewisky
Senior Member
- Apr 26, 2013
- 183
- 50
'nchi yetu ni kisiwa cha amani'..hii kauli inaukweli ? Au tunadanganyana tu hapa?
Wewe unaamini Injili?ama ni injili ipi unayoizungumzia kama sio Mathayo,Marko, Luka na Yohana?Kama huziamini nawe sio Kafir?Ndugu kilanga kwanza unajua maana ya kafir?Unamjua aliyelianzisha kuwaita makafir?Lengo nikufahamishana kwania njema tu.Maana ya neno kafir ni mpingaji au mkanushaji wa MUNGU na yale aliyoyatolea habari kupitia vitabu vitukufu.eg Periyar and you his supporter.Ili usiwe kafiri usipinge hata moja kati ya haya yafuatayo na kuyafanyia kazi.
1.Mungu ni mmoja tu,hakuzaa wala hakuzaliwa.
2.uwamini mitume wote bila kubagua hata mmoja.egMUSA,IBRAHIM,IS'HAAQ,YAAKUB,DAUD,ISSA,MUHAMMAD ETC.
3Uwamini vitabu vyake vyote vinne,Zabur,Taurat,Injil na Qur'an.quran ndio zama zake hizi.
4.Uwamini malayka wake wote.eg gibriel(Gabriel),Mikael,Israfil,Ridhwaan etc.
5.Uwamini uwepo wa siku ya kufufuliwa watu woote na kukusanywa mbele ya Molawao mlezi.
6.uwamini "qadar"yaani heri ama shari haimfiki mtu ila mungu ameliandikia liwe.
Hivyo Mungu mwenyewe ameamua kuwaita wale wote wasiomini hatakama ni mojatu ni makafir.Lakini pia ukiamini bila kutekeleza amri na kuacha makatazo unakua Mnafiq.yaani nusu Muumini na nusu kafir.
"Ama uwaeleze ukweli ama usiwaeleze makafir hawaamini"qur'an 2:8.
Nduguzangu hayo ni magumu mno kuyaamini ila kwawenyeimani sana ndio maana mungu mwenyewe anasema hao ndi watakao faulu na malipo yao hayana mwisho.kwamaana wataonekana kituko hapa Duniani nao watavumilia tu.
Kwa akili yako ya darasani (achana na ya ahera) unakaa na kukubali kweli kwamba hapo uislam uko sahihi? Basi kwa mantiki nyingine hapo ndipo chanzo cha migogoro ya kidini kwa wale ninaowaita fanatics. Kusadiki ni kuamini. Imani na ukweli ni vitu viwili tofauti. Haya ndio yale ya kuwafananisha binadamu wengine na karagosi kisa tu Mtume kasema hayo. Kaa na ukweli wako na uwafundishe wengine kuthamini walio wa imani tofauti na uislam.
Wayahudi waliwadharau watu wa mataifa mengine kisa tu wao ni Taifa teule. Wakawaona Wasamaria kuwa ni taifa lililodhalilika na kuwatenga. Mwisho kwa kuwa walifanya mioyo yao kuwa migumu, basi upendo wa Mungu ukahama kwao na kwenda kwa mataifa. Hicho kipande chaweza kuwa ndio mwanzo wa matatizo yaliyoko.
Raia fulani,
Elimu ya darasani ni mawazo ya binadamu kama mimi!
Huwa naamini zaidi maneno ya MUNGU kuliko ya binadamu!
Kama hukusoma comment yangu kwa haraka basi ulifeli kuianalyze!
sijaona mafundisho ya MTUME(S.A.W)..
Ya kuwaita binadamu wingine kikaragosi hii ni propaganda na kama alifundisha hivyo basi nisingeona hata umuhimu wa kujadiliana na wewe!
Katika dhambi kubwa mojawapo ni kuuwa kiumbe cha MUNGU hata panya au paka..... Iweje uislamu uamrishe kuuwa binadamu????!!!
Kiimani naamini hivyo ila hiyo siyo sababu ya kumwaga damu za watu!
Kama kuna muislamu kafanya hivi basi analo lakujibu mbele ya MUNGU! Na amefanya hivyo lwa interst yake binafsi na haikubaliki!
Raia fulani,
I real smpathyz with what happened in arusha na ofcoz sikufurahi hata kidogo
NAOMAB KUJUA,
JE NIVIASHIRIA VIPI VINAWEZA KUTUTAMBULISHA KUWA TUKIO FULANI LILILOLETA MAAFA NI UGAIDI,VISASI AU NI UDINI.tafadhali nijulisheni
Kiranga kaingiaje hapa?Dogo unamjua Kiranga wewe?nakuonea huruma kwa sababu kwa post yako hii kila mkongwe hapa JF anakuona mburula!
nilikuwa namjibu Kikwajuni One aliyekuwa anambeza Kiranga kuwa amesoma shule za kata kwa uandishi wake,Je nawe unamjua Kiranga?Msome tena kwenye nyuzi zake za nyuma!Kiranga kaingiaje hapa?
nilikuwa namjibu Kikwajuni One aliyekuwa anambeza Kiranga kuwa amesoma shule za kata kwa uandishi wake,Je nawe unamjua Kiranga?Msome tena kwenye nyuzi zake za nyuma!
Hoja nzito zisijibiwe na kuchukuliwa kirahisi! Vijana punguzeni emotions hili suala linahitaji upelelezi wa kina. Ikigundulika waislm hawahusiki nyny mnaowatuhumu sura zenu mtaziweka wapi?
Ndugu kilanga kwanza unajua maana ya kafir?Unamjua aliyelianzisha kuwaita makafir?Lengo nikufahamishana kwania njema tu.Maana ya neno kafir ni mpingaji au mkanushaji wa MUNGU na yale aliyoyatolea habari kupitia vitabu vitukufu.eg Periyar and you his supporter.Ili usiwe kafiri usipinge hata moja kati ya haya yafuatayo na kuyafanyia kazi.
1.Mungu ni mmoja tu,hakuzaa wala hakuzaliwa.
2.uwamini mitume wote bila kubagua hata mmoja.egMUSA,IBRAHIM,IS'HAAQ,YAAKUB,DAUD,ISSA,MUHAMMAD ETC.
3Uwamini vitabu vyake vyote vinne,Zabur,Taurat,Injil na Qur'an.quran ndio zama zake hizi.
4.Uwamini malayka wake wote.eg gibriel(Gabriel),Mikael,Israfil,Ridhwaan etc.
5.Uwamini uwepo wa siku ya kufufuliwa watu woote na kukusanywa mbele ya Molawao mlezi.
6.uwamini "qadar"yaani heri ama shari haimfiki mtu ila mungu ameliandikia liwe.
Hivyo Mungu mwenyewe ameamua kuwaita wale wote wasiomini hatakama ni mojatu ni makafir.Lakini pia ukiamini bila kutekeleza amri na kuacha makatazo unakua Mnafiq.yaani nusu Muumini na nusu kafir.
"Ama uwaeleze ukweli ama usiwaeleze makafir hawaamini"qur'an 2:8.
Nduguzangu hayo ni magumu mno kuyaamini ila kwawenyeimani sana ndio maana mungu mwenyewe anasema hao ndi watakao faulu na malipo yao hayana mwisho.kwamaana wataonekana kituko hapa Duniani nao watavumilia tu.
Kwa nini viongozi na wenye mamlaka wakiongozwa na Rais waseme kuwa lile ni tendo la kigaidi? Kwa nini isiwe ni hujuma ya kidini? Pamekuwepo na mfululizo wa matukio haya yakilenga jumuiya ya kikristo pande zote mbili za Muungano; Bara na visiwani. Wakristo wamejeruhiwa, wakristo wameuawa. Kwa nini bado iwe ni ugaidi? Kwa nini walengwe wakristo na sio taasisi za kiserikali na shughuli zingine zisizo za kidini?
Akihojiwa na BBC-Focus on Africa, Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa (hope niko sahihi) Peter Kalage naye amepinga kuwa si hujuma ya kidini bali ni ugaidi. Kwamba tunaoleana, tunaishi pamoja, n.k. Hayo ya kujamiiana (sio tusi-socializing) yanaweza kuhalalisha kupinga kilichotokea kwamba si hujuma ya kidini? KWani migogoro ya kidini huja kama radi? Au tuelezwe kama kuna evolution hapa, kwamba hatua ya kuelekea mgogoro wa kidini kwanza lazima hali ipitie ugaidi...
Wala kauli za wenye dhamana zisitutishe kwamba wanaharakati na wanasiasa wanaozungumzia haya masuala na kuituhumu serikali kwamba watapotezwa. Wameshapotezwa wengi na sio nia yao kuacha kuwapoteza. Kauli kama hizo zinatolewa waziwazi na hawa viongozi. Mei Mosi Mkuu wa Mkoa Arusha akasema waandishi wanaoiandika vibaya serikali watashughulikiwa. Nako Bungeni waziri anasema 'wanaosema ukweli' mchungu.
Lini tutasema kuwa hujuma hii ni ya kidini na hii ni ya kigaidi? Urahisi wa kutuhumu ugaidi unatoka wapi? Kama viongozi hawataki kusikia kauli ya UDINI, na kama inawakereketa basi wahakikishe kuwa huu mgogoro unamalizwa. Kama alivyosema Lema; hekima si kuwaita viongozi wa kidini Ikulu. Hekima ni kutatua tatizo lililopo.
Mwisho, Mods naomba msiunganishe mada yangu na zilizopo.
Tatizo ya shule za kata,hata uandishi wako,haueleweki vizuri.
Tumesahaulishwa ujangili wa kinana kimtindo,usalama na ccm are behind this
lete ushahid alau robo unaoonyesha kuwa Qur'aan al karym ina contradiction kisha ntakupa contradiction luluki toka kwenye bible..
mimi nimekuelewa mkuu. Turudi hapo kwenye neno fanatic. Katika dini zote hawa watu wapo. Hata katika mambo yasiyo ya kiimani wapo. Hawa hutafsiri mambo katika face value. Linapoingia suala la imani ndio huwa mbaya zaidi. Mbaya kuliko ni hapo mafundisho yenu yanaposema kuna allah tu. Kwa muumini mwenye akili fupi na mtazamo finyu na kwa bahati mbaya aliyelishwa maneno na walimu wake wa kidini si ataamini kuwa wakristo hawana huyo allah? Ni mapagani tu? Ni makafir tu? Sasa akiwa na mtazzamo huo halafu anaambiwa hawa makafir ndio wanawatawala watu halal wa allah si ndio chuki zinaanzia hapo? Naamini wewe ni kati ya waelewa wazuri sana. Kusikitika inatosha? Umechukua hatua gani kuona kuwa hawa wa imani yako hawatekelezi uasi dhidi ya wakristo?
Kichekesho kingine sasa umeingia mchezo wa kuwanunua vijana wa kikristo au kuwashawishi kwa namna wajuayo ili watekeleze mambo ambayo yataonekana yana utata. Kijana wa bajaji ana hasira kiasi gani na umati ule wa waumini? Ana hasira kiasi gani na imani yake? Anataka kuwaua ili iweje? Mwisho nasema hakuna dini ya Mungu, bali kuna watu wa Mungu.
... Dini yenyewe - in the context of our dominant Abrahamic religions- ni ugaidi, kwa hiyo hizi habari za kuziosha dini zionekane tofauti na ugaidi zinachekesha.
....
Mkuu, pamoja na yote uliyoeleza kuhusu dini, hebu tuliangalie suala hili kwa mazingira (context) ya Tanzania ya leo chini ya utawala wa awamu ya nne. Tukitaka kuliweka tukio la Arusha kwenye mazingira ya udini basi tutakuwa tumelirahisisha sana na kufanikisha matakwa ya wanaopenda lionekane hivyo ili wao waje na gia ya upatanishi, usuluhishi na ujenzi wa umoja, amani, utulivu na mshikamano wa taifa. Bila shaka unawafahamu ni akina nani hao. Ndio wimbo wao rasmi siku hizi. Umeshawasikia wakikimbilia kuitisha kongamano la masheikh na maaskofu kutafuta "suluhu" ya "tatizo la udini linalotuandama".
Kwangu mimi kilichotokea Arusha ni ugaidi uliotokana na serikali kushindwa kazi (failure of government). Dini, kwa vyovyote vile utakavyoitazama, imetumika kama nyenzo tu. Tukianzia kwenye harakati za kisiasa ambapo viongozi na wanachama wa chama tawala tangu mwanzo wamekuwa wakisikika mara nyingi wakitumia hoja ya kuonyesha kuwa vyama vya upinzani haviwezi kulinda umoja na mshikamano wa watanzania kama chama chao. Walianza kwa kutishia machafuko kama yaliyotokea Rwanda 1994, kisha wakaja na kuvihusisha vyama hivyo na dini za uislamu (CUF) na ukristo (CHADEMA) kisha ukoo, ukabila, ukanda. Baada ya hapo tukaanza kusikia "mfumo kristo", MOU kati ya kanisa na serikali, mahakama ya kadhi, kujiunga na OIC, n.k.
Tunachotakiwa kufanya kama Watanzania ni kuihoji serikali (ya CCM) itoe majibu thabiti yasiyo na shaka kuhusu masuala yote hayo. Hususan iweke wazi kabisa mtazamo/msimamo wake hususan kuhusu madai ya kuwepo "mfumo kristo", MOU, OIC, ubalozi wa Vatican, mahakama ya kadhi, BAKWATA, na yanayoelekeana na hayo yenye mtazamo wa kidini. Na iwe wazi kabisa kwamba msimamo wake unatokana na madaraka kamili iliyo nayo ili kuondoa shaka kwamba kuna shinikizo zito toka upande wa dini fulani ambalo haina uwezo wa kulipinga. Nimekuwa najiuliza inakuwaje kundi la watu wanataka kuandamana kwenda kumng'oa Katibu wa Baraza la Mitihani ambaye ni mteule wa Rais kama kwamba yeye aliyemteua hana ubavu wa kumuondoa akivurunda au kumtetea kama yuko sahihi? Lazima kuna mazingira yametengenezwa kueneza mitazamo fulani (ya kidini) katika jamii ili kuigawa kwa manufaa ya kundi fulani la walio madarakani. Hapo serikali haiwezi kukwepa wajibu.
Kwa kifupi tukio la Arusha si mzozo wa kidini bali ni dini kutumika kama fursa ya kuwaimarisha watu wasio na utu wala maadili ya kibinadamu ili kuingia na/au kudumu kwenye nafasi za madaraka zitakazowawezesha kufanikisha ulaji haramu/uhujumu wa rasilimali za nchi bila kuhojiwa. Wakiguswa tu wanaingiza vigezo vya kidini. Na wanaohoji kwa unafiki nao wanaangalia dini za wahojiwa. Hatuwezi kuendelea namna hiyo. Dini za kweli zinataka watu wawe safi, watenda haki, walio na utu na kiasi. "Udini wa Tanzania" unaenezwa na watu walafi wasio na simile kwenye haramu kadhaa. WAONGO.
Wanachotaka kusema ni kwamba dini haifundishi kupigana mabomu, ugaidi ndo unafundisha hivyo. Kwa hivyo suala la mabomu haliwezi kuwa la kidini, ni la kigaidi. Hata kama jumuiya za kidini zitahusika lisiangaliwe kama suala la kidini, liangaliwe kama suala la kigaidi.
Kitu ambacho si cha kweli. Biblia na Kurani zinafundisha vita vya kidini. In a fence sitting, wishy washy way of course, as almost anything in these books is taught.
Dini yenyewe - in the context of our dominant Abrahamic religions- ni ugaidi, kwa hiyo hizi habari za kuziosha dini zionekane tofauti na ugaidi zinachekesha.
Ukiangalia neno "terrorism" linahusisha mzizi wa "terror". Kupata matokeo unayoyataka kwa kuogofya watu.
Dini zinazohubiri moto haziwezi kusema si za "kigaidi" kwa sababu zinataka waumini wake wafanye kwa mujibu wa mafunzo yake (Uislamu/ Ukristo) kwa kuogopa moto. Moto ambao as far as we can realistically tell, haupo.
If that is not terrorism I don't know what is.