Kwako Rais Magufuli

Kwako Rais Magufuli

We endeleza mapambano nyuma ya keyboard,ila ukijitokeza mtaani ni kipigo tu mpaka utakapojua kujibidiisha na kuacha ulalamishi.Tatizo mmekariri kila anayepingana na nyie anafaidika serikalini.Walalamishi ni wale wale hata wakati wa JK,utazeeka ukiwa mlalamishi.Shauri yako.

Haitokusaidia kama utashindwa kuwasemea wasio na SAUTI,wakati wengine wanakula mpaka wanavimbiwa na kutapika kabisa kabisa kuna wengi zaidi wanakufa njaa au kwa magonjwa na hawana dawa hospitalini au chakula nyumbani.

Yawezekana tunatofautiana UTU na UBINADAMU,anyway kuna siku mnayemsifu leo akitoka hapo alipo atakuja kuwalaumu kwa kutomuonya.

Muda ni dawa.Usipoinywa leo hata kesho utainywa.

Endelea kupongeza serikali hata wakiendelea kuiba endelea kupiga makofi,siye tutaendelea kupiga makelele hata kuuza Tshirt tu zinatosha kuifanya serikali kukumbuka kwamba ni wakati unapita waamke.

Tanzania siyo ya watawala na familia zao,Tanzania ni yetu sote,hakuna mwenye uhalali au haki yakuua MTANZANIA mwenzake hatuka RWANDA au BURUNDI
 
Ukiangalia kwa makini walalamishi wote walizoea vya dezo. Imagine mtu toka darasa l a saba kapita kwa kuibia mtihani, form four kaiba paper, six kaiba paper, chuo kadesa kuepuka sup na disco mpaka kamaliza. huyu mtu akifika nje atataka kubebwa. eti graduate ambaye hawezi kutumia knowledge yake kujiajiri. kujiajiri si mpaka pesa unaweza kutumia elimu yako tu ikakutoa, andika proposals, business plan uza e.t.c Serikali haipo kukuletea maisha bora direct...yenyewe inaandaa mazingira ya kukuwezasha -ufanikiwe...barabara, reli n.k . halafu mtoa post anasema kuhusu ajira...mbona website kibao zinapost nafasi za kazi. PAMBANA NA HALI YAKO.
 
Alianza vizuri ilamekosa muelekeo na hii ni adhabu yake maana anayelinda watu si serikali ni Mungu. Mungu angemlinda na yote ila karuhusu ili kumfundisha kitu na kama anamasikio ya rohoni ataelewa. Kila jambo tulifanyalo tumtegemeze Mungu siyo baada ya shida. Kabla hujaongea sikiliza Mungu anakueleza nini juu ya utakalo kusema. Lissu mtetezi wa wanyonge au anajaribu kufanya nchi iwe ngumu kuongozeka kila siku anaajenda.

Unataka kukwamisha vitu mpaka hueleweki wewe ni mtanzania au nani? kila kitu unakiongea wewe, kwa kejeli unamkejeli mtu anaitwa mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama na Amiri jeshi mkuu, umeshika kalamu na masikio yako hewani kusubiri tuu anateleza wapi ili upate cha kusema hivi anatetea mtanzania gani jamani kwa jinsi hii. Hutoi muongozo unatafuta matatizo. Alijua anafuatiliwa mbona asitafute hao walinzi toka nje ya nchi mnasubiri shida itokee muite wapelelezi kutoka nje?

SMG ipigwe kwenye nyumba inayoishi watu wengi miliyo ya risasi isisikike kwa wengine jamani ?

Dereva mara kiti kililazwa mara alinilalia mimi ???? asihojiwe hatutaki mtabadili kesi who cares nini kinaendelea sasa?

Mwisho yatakuwa yale yale ya Ben Saanane kapotea hapana yupo tunaye kwenye vijiwe mtaani sis tupo mkichoka mtatuambia.
 
Ukiangalia kwa makini walalamishi wote walizoea vya dezo. Imagine mtu toka darasa l a saba kapita kwa kuibia mtihani, form four kaiba paper, six kaiba paper, chuo kadesa kuepuka sup na disco mpaka kamaliza. huyu mtu akifika nje atataka kubebwa. eti graduate ambaye hawezi kutumia knowledge yake kujiajiri. kujiajiri si mpaka pesa unaweza kutumia elimu yako tu ikakutoa, andika proposals, business plan uza e.t.c Serikali haipo kukuletea maisha bora direct...yenyewe inaandaa mazingira ya kukuwezasha -ufanikiwe...barabara, reli n.k . halafu mtoa post anasema kuhusu ajira...mbona website kibao zinapost nafasi za kazi. PAMBANA NA HALI YAKO.
Ukichaa unasura nyingi usipotambua unaweza aibika mbele za watu.
 
Unakosea wewe kumjibu hivo huyo bado anamachungu..sasa ilitakiwa umjibu kama alivoeleza nakuyatoa machungu yake..
Anyway ngoja na mimi kidoooogo japo nimfariji huenda maimivu yake yakapungua na kama alitumwa atarudisha marejesho kwa waliomtuma

stickvibrator,
Mfariji ni mmoja tu naye ni Mungu wa Mbinguni.
Jamaa na Marafiki watakupa pole,hongera n.k lakini ni faraja ya muda tu. Huyu kijana ameeleza msongo wake wa mawazo alio nao na ni uhalisia wa kile anacho kipitia pamoja na Watz wengine...!!!
JPM asome waraka huu autafakari kwa kina......! Kuna nchi zina watu wanaitwa ''Suicide Bombers''( Wanaojitolea muhanga) walianza hivihivi kwa msongo wa mawazo unaosababishwa na Watawala.Ili kumaliza msongo kwa kulipiza kisasi wakaamua kuvaa mabomu....!!!Kumbuka nao ni binadamu sawa tu na huyu Mtanzania anayelalamika hapa pamoja na wengine wengi.......!!!
This is a Time bom waiting to explode at any time 't'...!!!!!
 
Watu waliwaonya wakiwaambia ni kati ya malucifer wakubwa duniani hamkusikia na bado sasa anapoteza anauwa bado kidogo atatafuna vichwa vyenu
 
Mkuu wewe jua kitu kimoja huwezi shindana na serikali,fanya yako.Hiyo hali ipo mioyoni mwenu tu,mtaani maisha yanasonga kama kawaida.Lissu alijidanganya na nyie mkamchochea akajiona Hero.,wangapi hapa walimwambia anachokitafuta atakipata?,. Kama unataka uongozi wa nchi subiri 2020 ugombee ila usiwatoe watu kwenye mipangilio iliyopo.Mnamuita mwanasheria msomi,wanasheria wengine hawajasoma?,haya yupo wapi sasa?.,hii dunia fanya yako,serikali achana nayo huwezi shindana nayo,itakula kwako.Kama una hasira sana hama nchi,urudi Lowassa akiwa Raisi,kama hujazeekea huko huko.
Wewe ni mjing..a sana, sio tusi ni maelezo.
 
Ukiamua kushinda kwenye mitandao ya kijamii,lazima maisha yawe magumu.Ukipita mitaaani hasa maeneo ya machinga,mama ntilie,waendesha pikipiki,wauza mitumba,wauza kahawa,matunda.. Sokoni na kila sehemu,karibu nchi nzima watu wanaendelea na maisha yao ya kila siku,kwa amani na furaha tele.Nyie mliomaliza vyuo na wote mnategemea mchukuliwe na serikali na kila mtu anataka kazi ya TRA na tai kubwa ndo mna wakati mgumu.Hii sio sasa hivi tu,ni miaka yote,tofauti ni kuwa huko nyuma kuna ndugu walikuwa wanawa boost kidogo kidogo kwenye uchumi,zamu hii wamebanwa.Kuwa mbunifu,kulalamika hakusaidii.Ukibisha endelea kuilalamikia serikali,kama una uwezo wa kuiondoa kila la heri,ila yatakayokukuta utahadithia.Kama huna uwezo kuwa mbunifu,mambo yakufanya ni mengi hata ukiwa na elfu 50 tu.Uhuru wa kuabudu upo mkubwa tu,uhuru wa kuzungumza upo mkubwa tu,tatizo ni linapoletwa swala kisiasa,BAVICHA mnataka kumuombea Lissu himizaneni kila mtu alipo TZ nzima amuombee Lissu kwa wakati wake,au mpange kuanzia saa 9 jioni nchi nzima mumuombee Lissu kila mtu alipo,au kila mtu aende kanisani kwake na wa misikitini waende huko huko,hii ya kukusanyana Manzese na wa mikoani wakusanyane wapi?... Ukimchukulia JPM kwa jicho la kisiasa lazima umchukie,ila ukimuangalia kwa jicho la kujinasua hana baya,wewe pambana na hali yako,awamu zote zilizopita watu walalamishi kama wewe hawajawahi kukosekana,wapo tu.
Kua mkweli, wote hao wanalia.
 
Mfalme amekuwa na kiburi na shibe. Amesahau wenye kiu na njaa
 
Back
Top Bottom