Kwako mkurugenzi mkuu wa NIDA

Kwako mkurugenzi mkuu wa NIDA

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,523
Mimi ni Mtanzania na ninatakiwa kupata pasi mpya ya kusafiri. Moja ya sharti ya kupata pasi hii ni kuwa na kitambulisho cha Taifa au kuwa na nakala ya kitambulisho baada ya kuwa na namba ya kitambulisho cha Taifa.

Tumeelezwa kuwa nakala ya kitambulisho (kama huna kitambulisho) unaweza kuprint kutoka kwenye website yenu.

Nimefuata taratibu zote ili nipate nakala ya kitambulisho lakini website yenu aidha ina matatizo au imesitishwa kutoa nakala hizi.

Ninaomba msaaada au taarifa itolewe kwa wananchi kwa wale ambao hawana vitambulisho vya Kitaifa ila wanazo namba ni utaratibu gani wafuate ili wapate nakala ya vitambulisho vya Kitaifa ili hatimaye waweze kukidhi sharti hili la kupata pasi ya kusafiria. Kwa kweli tunateseka sana.
 
Mimi ni Mtanzania na ninatakiwa kupata pasi mpya ya kusafiri. Moja ya sharti ya kupata pasi hii ni kuwa na kitambulisho cha Taifa au kuwa na nakala ya kitambulisho baada ya kuwa na namba ya kitambulisho cha Taifa.

Tumeelezwa kuwa nakala ya kitambulisho (kama huna kitambulisho) unaweza kuprint kutoka kwenye website yenu.

Nimefuata taratibu zote ili nipate nakala ya kitambulisho lakini website yenu aidha ina matatizo au imesitishwa kutoa nakala hizi.

Ninaomba msaaada au taarifa itolewe kwa wananchi kwa wale ambao hawana vitambulisho vya Kitaifa ila wanazo namba ni utaratibu gani wafuate ili wapate nakala ya vitambulisho vya Kitaifa ili hatimaye waweze kukidhi sharti hili la kupata pasi ya kusafiria. Kwa kweli tunateseka sana.
Kwahiyo huyo mkurugenzi wa NIDA yupo humu ....... kwanini usipeleke malalamiko yako kama barua ofisini kwao na siyo hapa..... au Kwenye hiyo website yao au contacts zao .....
 
Kwahiyo huyo mkurugenzi wa NIDA yupo humu ....... kwanini usipeleke malalamiko yako kama barua ofisini kwao na siyo hapa..... au Kwenye hiyo website yao au contacts zao .....
Usidharau JF Mkuu,
Kuna jamaa aitwa Mk54 alikua na dukuduku lake kuhusu Bodi ya Mikopo akaleta humu na baada ya siku chache Bodi wakajibu. Hii ni platform kubwa mkuu.
 
Kutuma ujumbe kwenye website yao ingetosha nasiyo kuanza na huku ......vitu vingine ni uvivu kidogo tuu tayari thread si ndo uvivu wenyewe huo ...... http://nida.go.tz/swahili/index.php/contact-us-2/
Kuweka barua ya wazi kama hivi kuna impact kubwa kuliko kuwatumia kwenye website yao. Mfano kama kuna jambo baya umelifanya mtaani basi ukifuatwa faragha na uliemfanyia huo ubaya akakueleza hutochukulia kwa uzito mkubwa kuliko tuhuma zako zikiwekwa hadharani watu wakajua ubaya uliofanya.
 
Kwahiyo huyo mkurugenzi wa NIDA yupo humu ....... kwanini usipeleke malalamiko yako kama barua ofisini kwao na siyo hapa..... au Kwenye hiyo website yao au contacts zao .....
Mkuu jf n zaid ya uijuavyo humu tunatumia id fake ndio maana unaona Kama sio sehemu sahh lakn amini hapa n sehemu shh atapatiwa ufumbuzi
 
Hahaha wote wamo humu, kwani wanaposema wanatukanwa mitandaoni unadhani wanaambiwa?! Wanayasoma humu, na wengine wanaomshangilia huko, humu wanamrukana sanaaa. Wanatukanana humu huko nje wanalinda vibarua vyao.
 
Hii ndiyo platform sahihi ya kutoa malamiko/maoni. Sasa kama website haifunguki na tunataka huduma kwa nini asielezwe. jf ni zaidi ya ujumbe wa simu au email. Natumaini wengi watakuwa wamesoma ujumbe huu pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NIDA au watumishi walio chini yake. Kwa maana nyingine message sent na kama hataifanyia kazi basi ana tatizo.
 
Na hii NIDA nyamagana Mwanza Ni full corruption huyu meneja was nyamagana naona kazi imemshinda kupata namba tu ya kitambulisho Ni hatua ya miezi 3 jamani bado ID ukimwambia kulikoni utazungushwa Kama unaomba kazi, hii siyo fair Mambo yetu yanakwama
 
Nadhani hawa watu wa NIDA kuna kitu kinawasumbua na hawako tayari kuwaeleza Watanzania ukweli,na kwa ukimya huo tutawazidi kuwasuta sana.
Yaani suala la mtu kupata namba ya kitambulisho tu limekuwa gumu sana,utadhania haya mambo tunayafanyia nchi nyingine. Lkn wanapofanya hivyo,wajue kuna taasisi hasa za binafsi km vyuo vya udereva vinaathirika sana. Inaeleweka mtu haruhusiwi kuanza practical ya mafunzo ya udereva unless amepata leaner licence. Na ili apate hiyo leaner licence ni "lazima" awe na aidha kitambulisho chenyewe au namba yake. Hapo akifika NIDA iwe ni danadana....sasa hivi vyuo vitaendeshaje kazi zake km si kuumizana taratibu??
Binafs pia naomba tamko la Mkurugenzi wa NIDA
 
Hawa NIDA ni janga la taifa, kwasababu kila unapoenda unadaiwa kitambulisho cha taifa au nakala yake au namba yake, lakini NIDA wanashindwa kutoa hata namba za vitambulisho tuu, na ukweli hawasemi wanasema tuu njoo wiki ijayo kila siku
 
Back
Top Bottom