Kwako Mh. Ndalichako, Joyce.

Kwako Mh. Ndalichako, Joyce.

wahanga tuko wengi ..nami nipo hapa udom mambo si mambo ...eeh Mungu tunusuru mafukara ...imefika time najutia kusoma kabisa bt nmeappeal uku nikisubiri hayo yaliyobaki ...Mungu ni mwema hakika atatenda ndugu tusikate tamaa.
 
Naitwa Shafir Zubail, mhitimu wa kidato cha nne 2010. Shule nimesoma ya serikali ya Kaigara Shule ya Sekondari, ila kulingana na hali ngumu ya kimaisha ya hapa nyumbani sikuweza kufaulu kuwndelea na ngazi ya juu. Nimeteseka sana mtaani huku nikichanja na kuuza kuni mtaani, ile biashara haikunilipa kulingana na uduni wa familia yangu kwani licha ya kuwa mdogo, nilipaswa kutafuta chakula kwa ajili ya familia yangu kwani Baba yangu aliumwa sana kipindi hiko, kuanzia 2009 mpaka mwaka 2014, Mei ndipo alitoka hospitalini. Baada ya kusota mtaani kwa muda mrefu bila ya maganikio kimaisha, February 2014 niliamua kuanza kusoma mtaani ili niweze kurudia mtihani wa kidato cha nne kwani nisingeweza kurudi shule maana tayari muda ushaniacha. Nimesoma kwa shida sana huku nikitafuta ada ya twisheni niliyokuwa nasoma. Mwezi Oktoba, 4, 2014 kaka zangu watatu walipata ajali na kupoteza maisha. Hapohapo Baba yangu akapata stroke na kurudi upya kwenye maradhi. Sikuwa na uhakika na mwaka ule kulingana na matatizo ya nyumbani na ilhali tarehe 03/11 ndo tarehe iliyokuwa ya kuanza kufanya mtihani huo. Mwaka 2015 14, February matokeo yalitoka na nikafanikiwa kupata alama za kuniwezesha kufanya mtihani wa kidato cha sita. Katika hali ya matatizo mengi huku nikitafuta ada ya twisheni, mwezi wa tano mwaka huu nikafanya mtihani sikubahatika kupata alama za juu ila nikabahatika kupata pointi zinazohitajika kwenda chuo kikuu. Nilijaza fomu za kuomba mkopo bila kukosea lolote kwani kwenye list ya watu waliokosea 10,027 jina langu halikuwepo(nilijihakikishia). Wakati wa kuomba vyuo, nakumbuka niliomba tarehe 27/07. Nilibahatika kupata chuo cha Archbishop James University College (AJUCO), first batch jina langu ni la 877, na kwenye list ya TCU iliyotoka yenye majina 63,773 ya wanafunzi waliofahiliwa mwaka 2016/17 jina langu ni la 181.

Ada ya kulipa Archbishop James University College (AJUCO) ni kubwa sana kwangu (Ada Tsh 1,260,000/=, Administration fees Tsh 285,000/=, Hostel Tsh 400,000/=) kwani kulingana na maradhi aliyoyapata Baba, eneo kubwa la shamba ameshaliuza. Hivyo ameuza sehemu aliyokuwa amenipa ili nilipe mahitaji ya kwanza. Lakini pesa haitoshi hivyo ikanibidi niombe transfer UDOM.

Lakini cha kushangaza ni kwamba sijapata mkopo na maisha yangu ni magumu sana huku mtaani maana tayari nilikuwa nimeona nuru mbele yangu lakini nasikitika kwa masikitiko makubwa. Tafadhali, nisaidie mimi maana bila mkopo uwezo wa kujisomesha sitaupata kwani sitapata ada kwa ajili ya semester ya pili ya mwaka wa kwanza.

Samahani, Kiswahili na maelezo niliyotoa yamejikita kwenye lugha mama.

Nashukuru sana kwa kunielewa.


Binafsi kuna vitu vinanitatiza kwenye hii taarifa yako. Umedai kuwa ukufanya mtihani wa kidato cha nne 2014 kwa kuwa mzazi alikuwa mgonjwa na hali ngumu ya maisha na wewe ndio ulikuwa unategemea. In between unao kaka watatu wamefariki kwa ajali. Hao kaka hawakuwa na mchango?

Secondly, uliamua kurudia mtihani 2014 February, ina maana ulifanya mtihani mwaka huo 2014 (CSEE) matokeo yalitoka January 2015, hayo ni matokeo ya form four siyo?

Hiyo form six ulisoma lini????, uliwezaje kufanya mtihani bila kusoma F6? huwezi kuona hii ndio sababu ya wewe kutopata mkopo? Hivyo vyuo vingi vinafanya biashara pia Zaidi ya kutoa elimu, yawezekanaje kuwa admitted chuo kikuu na history za shule hii, maana wakiangalia cheti cha form four 2010 (Hauna alama kwa maelezo yako) ukitumia hiki cha 2015, inaonesha wewe sasa unatakiwa uwepo form six yaani ufanye mtihani 2017, sasa mwenzetu unaenda chuo??
 
Mama Ndalichako, Watanzania wengi wanahitaji msaada. Huu ni mfano wa mmoja wa waliojitolea kukueleza yanayowasibu. Hii dhana ya ukopeshaji na vigezo vinavyotumika kupata mikopo bado haijaeleweka miongoni mwa Watanzania. Tafadhali wasaidie hawa vijana ili waweze kujikomboa kielimu. Tusije tengeneza Taifa la mambumbu.

KWanza kuna mkanganyiko kwenye hiyo elimu, unategemea akikimbilia chuo kikuu kabla ya kupata msingi nyuma atasaidika? au ndio akimaliza tena tuanze kusema hapati kazi, nadhani yafaa tumshahuri asome kwanza katika mtiririko sahihi awe na msingi wa kutosha. walioweza elimu ya miaka 2 walikuwa na maana. kwa maelezo yake huyo kasoma lini F6???
 
Binafsi kuna vitu vinanitatiza kwenye hii taarifa yako. Umedai kuwa ukufanya mtihani wa kidato cha nne 2014 kwa kuwa mzazi alikuwa mgonjwa na hali ngumu ya maisha na wewe ndio ulikuwa unategemea. In between unao kaka watatu wamefariki kwa ajali. Hao kaka hawakuwa na mchango?

Secondly, uliamua kurudia mtihani 2014 February, ina maana ulifanya mtihani mwaka huo 2014 (CSEE) matokeo yalitoka January 2015, hayo ni matokeo ya form four siyo?

Hiyo form six ulisoma lini????, uliwezaje kufanya mtihani bila kusoma F6? huwezi kuona hii ndio sababu ya wewe kutopata mkopo? Hivyo vyuo vingi vinafanya biashara pia Zaidi ya kutoa elimu, yawezekanaje kuwa admitted chuo kikuu na history za shule hii, maana wakiangalia cheti cha form four 2010 (Hauna alama kwa maelezo yako) ukitumia hiki cha 2015, inaonesha wewe sasa unatakiwa uwepo form six yaani ufanye mtihani 2017, sasa mwenzetu unaenda chuo??

Ndugu huenda hujanielewa, nimesema February 2014 nilisajili kurisit mtihani wa kidato cha nne, kabla ya necta mwaka huo huo kaka zangu watatu walipata ajali na kufariki. Wakati huo ni oktoba, novemba nilipaswa kufanya mtihani kulingana na nilikuwa nimeshasajiliwa, nilifanya mtihani huo na February 14, 2015 matokeo kidato cha nne yalitoka. Nimesoma mwaka mmoja form 5 na 6. Ni kipi hakijaeleweka? Kupata ajali kwa kaka zangu au mzee kupata strock?
 
KWanza kuna mkanganyiko kwenye hiyo elimu, unategemea akikimbilia chuo kikuu kabla ya kupata msingi nyuma atasaidika? au ndio akimaliza tena tuanze kusema hapati kazi, nadhani yafaa tumshahuri asome kwanza katika mtiririko sahihi awe na msingi wa kutosha. walioweza elimu ya miaka 2 walikuwa na maana. kwa maelezo yake huyo kasoma lini F6???

Ahsante
 
S0880/0176/2010
P0880/0083/2014
P0360/0517/2016
Sidhani kama utakuwa hujaelewa hapo ndugu.

Au, tafuta majina ya first selection ya Archbishop James University College (AJUCO), list ya waliodahiliwa na TCU mwaka huu. Au tafuta namba ya S0880/0176/2010 kwenye cas ya TCU utajua
ulisoma form six lini na muda gani. Hii ndio sababu ya wewe kutopata mkopo
 
Ndugu huenda hujanielewa, nimesema February 2014 nilisajili kurisit mtihani wa kidato cha nne, kabla ya necta mwaka huo huo kaka zangu watatu walipata ajali na kufariki. Wakati huo ni oktoba, novemba nilipaswa kufanya mtihani kulingana na nilikuwa nimeshasajiliwa, nilifanya mtihani huo na February 14, 2015 matokeo kidato cha nne yalitoka. Nimesoma mwaka mmoja form 5 na 6. Ni kipi hakijaeleweka? Kupata ajali kwa kaka zangu au mzee kupata strock?

Matokeo yametoka mwaka 2015 January ya form four uliyofanya October 2014 sio?
Haya baada ya matokeo yanakuqualify ulisoma lini form six na ukafanya mtihani na kupata matokeo, maana kama ulifanya mtihani ulifanya wa form six ni 2016, ni mwaka mmoja. Hizi elimu hizi zinatiliwa mashaka, na kuchanguliwa vyuo wanavyofanya biashara ni ngumu, ndio maana vyuo kama UDSM hawawezi kukupa nafasi
 
Matokeo yametoka mwaka 2015 January ya form four uliyofanya October 2014 sio?
Haya baada ya matokeo yanakuqualify ulisoma lini form six na ukafanya mtihani na kupata matokeo, maana kama ulifanya mtihani ulifanya wa form six ni 2016, ni mwaka mmoja. Hizi elimu hizi zinatiliwa mashaka, na kuchanguliwa vyuo wanavyofanya biashara ni ngumu, ndio maana vyuo kama UDSM hawawezi kukupa nafasi

Sawa, unajua kilichonifanya nisome mwaka mmoja?
 
Nimesoma mwaka mmoja. Mbona wengine wamepata na the same qualifications?
Hii haipo, waliopata ni wale waliopo mtiririko wa kawaida 4+2 years of secondary school. Kaa ukijua pia first exams performance in Nguvu sana, husije tegemea kamwe mtu aliye na alama nzuri kwa first performance watakujudge nawe. Ndio maana matokeo yanatengwa kuwatofautisha. Hao wanaweza kupata kwa kuwa wamesoma miaka 2 form six na mtiririko wa elimu unajulikana
 
Hii haipo, waliopata ni wale waliopo mtiririko wa kawaida 4+2 years of secondary school. Kaa ukijua pia first exams performance in Nguvu sana, husije tegemea kamwe mtu aliye na alama nzuri kwa first performance watakujudge nawe. Ndio maana matokeo yanatengwa kuwatofautisha. Hao wanaweza kupata kwa kuwa wamesoma miaka 2 form six na mtiririko wa elimu unajulikana

Ooh! Ahsante kwa maelezo yako.
 
Ooh! Ahsante kwa maelezo yako.
Nakushauri hii itakusaidia hata baadae, unatakiwa uingie katika mfumo wa school candidates, uonekane umefanya mtihani na umesoma kama school candidate, na sio unapeleka vyeti vya private seating form four 2015, f6 2016, nakuhakikishia hata kazi ya maana ni ngumu kupata,
yaonesha unao Uwezo ingia mfumo huo uwe na performance zinazoeleka.

Hii wengi wanafanya hawajui inawagarimu vipi
 
Pole waone bodi ukiwa supporting documents zote. Nadhani bado wako masasani.
 
Cc FaizaFoxy njoo msaidie nduguyo katika imani ili apate kile ambacho umekua ukikitetea kwa Watoto wa Kiislamu. Mtafutie hata transfer to Muslim University ili apate ufadhili huko.

Ahsante.
 
Binafsi kuna vitu vinanitatiza kwenye hii taarifa yako. Umedai kuwa ukufanya mtihani wa kidato cha nne 2014 kwa kuwa mzazi alikuwa mgonjwa na hali ngumu ya maisha na wewe ndio ulikuwa unategemea. In between unao kaka watatu wamefariki kwa ajali. Hao kaka hawakuwa na mchango?

Secondly, uliamua kurudia mtihani 2014 February, ina maana ulifanya mtihani mwaka huo 2014 (CSEE) matokeo yalitoka January 2015, hayo ni matokeo ya form four siyo?

Hiyo form six ulisoma lini????, uliwezaje kufanya mtihani bila kusoma F6? huwezi kuona hii ndio sababu ya wewe kutopata mkopo? Hivyo vyuo vingi vinafanya biashara pia Zaidi ya kutoa elimu, yawezekanaje kuwa admitted chuo kikuu na history za shule hii, maana wakiangalia cheti cha form four 2010 (Hauna alama kwa maelezo yako) ukitumia hiki cha 2015, inaonesha wewe sasa unatakiwa uwepo form six yaani ufanye mtihani 2017, sasa mwenzetu unaenda chuo??
Kwa hyo ww braza hujawah kuona watu wanapiga form 5 na 6 kwa mwaka mmoja na mwisho wanapiga pepa kama PC? Watu kibao wanafanya hvyo kusave muda na pesa,,,, em pitia majina ya Udsm ya mwaka huu usipokutana na watu waliomaliza mwaka 2014
 
Back
Top Bottom