PapoKwaPapo
JF-Expert Member
- Jun 5, 2008
- 380
- 45
Heshima kwako mheshimiwa.
Kwanza kabisa natanguliza shukrani zangu za dhati kwako, kwa hamasa kubwa uliyoileta kwenye siasa za Tanzania hasa kwa vijana. Wewe ni kiongozi shupavu, ninaposema shupavu namaanisha shupavu kweli kweli. Huogopi kusema kile unachokimini popote pale na ndio viongozi wa namna hii tunaowahitaji hapa kwetu Tanzania.
Lengo hasa la waraka huu ni kukusifu na kukutia moyo kama mbunge mteule wa Arusha mjini na waziri kivuli wa mabo ya ndani. Kilicho nisukuma mpaka nikakuandikia waraka huu leo ni baada ya kusikia ulikuwa Tarime. Kuna watanzania wenzetu wameuwa huko kama waziri kivuli wa mambo ya ndani ukafanya lile linalotaki yaani kwenda kujua nini hasa kilicho tokea.
Kilichonishangaza mimi ni kwamba hata waziri mwenye dhamana ya mabo ya ndani hakujitokeza kutaka kujua ni nini kilichotokea huko. Hili kwako na Chadema ni goli la ushindi.
Nakuomba sana sana uwakumbushe mawaziri wengine vivuli wa Chadema watende kama ulivyo tenda, tunata kuona kwa mfano waziri kivuli wa afya anatembelea hospitali zetu za rufaa na kujionea jinsi zinavyofanya kazi na kuwa changamoto. Pia waziri kivuli wa ajira na vijana akitupa changamoto zake jinsi gani vijana watawezeshwa. Kila siku ninapoulizwa swahi hili huwa najibiwa nikasome ilani ya Chadema, ukweli ni kwamba si wote tuliopata hiyo bahati ya kusoma ilani yenu.
Huu ni muda wa kuonyesha chama chenu kipo tayari kushika madaraka. Godbless Lema waziri kivuli wa mambo ya ndani ameanza na wewe anza sasa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema.
Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Kwanza kabisa natanguliza shukrani zangu za dhati kwako, kwa hamasa kubwa uliyoileta kwenye siasa za Tanzania hasa kwa vijana. Wewe ni kiongozi shupavu, ninaposema shupavu namaanisha shupavu kweli kweli. Huogopi kusema kile unachokimini popote pale na ndio viongozi wa namna hii tunaowahitaji hapa kwetu Tanzania.
Lengo hasa la waraka huu ni kukusifu na kukutia moyo kama mbunge mteule wa Arusha mjini na waziri kivuli wa mabo ya ndani. Kilicho nisukuma mpaka nikakuandikia waraka huu leo ni baada ya kusikia ulikuwa Tarime. Kuna watanzania wenzetu wameuwa huko kama waziri kivuli wa mambo ya ndani ukafanya lile linalotaki yaani kwenda kujua nini hasa kilicho tokea.
Kilichonishangaza mimi ni kwamba hata waziri mwenye dhamana ya mabo ya ndani hakujitokeza kutaka kujua ni nini kilichotokea huko. Hili kwako na Chadema ni goli la ushindi.
Nakuomba sana sana uwakumbushe mawaziri wengine vivuli wa Chadema watende kama ulivyo tenda, tunata kuona kwa mfano waziri kivuli wa afya anatembelea hospitali zetu za rufaa na kujionea jinsi zinavyofanya kazi na kuwa changamoto. Pia waziri kivuli wa ajira na vijana akitupa changamoto zake jinsi gani vijana watawezeshwa. Kila siku ninapoulizwa swahi hili huwa najibiwa nikasome ilani ya Chadema, ukweli ni kwamba si wote tuliopata hiyo bahati ya kusoma ilani yenu.
Huu ni muda wa kuonyesha chama chenu kipo tayari kushika madaraka. Godbless Lema waziri kivuli wa mambo ya ndani ameanza na wewe anza sasa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema.
Natanguliza shukrani zangu za dhati.