Kwako Kibwana Dachi wa Magic FM

Kwako Kibwana Dachi wa Magic FM

Hivi ni sahihi kwa rais wa nchi kuongoza wanaotokana na chama chake tu katika nchi yenye vyama vingi vya siasa? Wale wasiokuwa wanachama wa chama chake huongozwa na nani? Najaribu kuwaza kwa sauti tu, povu lolote litanisaidia kuitakatisha akili!
Wasio kuwa wa chama chake anawatawala. Ni ukoloni kama ukoloni mwingine, kwani anatumia kodi zao kinyume na matakwa yao na ni kwafaida yake yeye na kundi lake.
 
Kama fomu tu ya mgombea inapokonywa vipi hizo camera zitaachwa salama?
 
Tufike mahali tuwe tunatumia akili zetu si zawawekezaji.
1. Awali tulisema hatutasimamisha mgombea kutokana na rafu zao natukaamini ndio msimamo wetu tukihitaji mabadiliko tume ila hayakufanyika zaidi ya Kailima kwenda jikoni tena na aliyekuja ndio Master wa rafu.

2. Ni bora kuwaacha wajipitishe hta bila ya kupingwa nafikiri wabane matumizi
 
Kwanza kabisa, inabidi kujiuliza, hivi ni kwa nini tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, matukio ya aina hii yalikuwa nadra sana kutokea? maana tungetarajia miaka ile kwamba vyama vilikuwa havina uelewa wa taratibu za uchaguzi. lakini kinyume chake, miaka 26 baadaye ndiyo tunaanza kushuhudia matukio ya namna hii. ni wazi kwamba kuna tatizo kubwa hapa.
unaonesha kura ulianza kupiga 2015
Mapingamizi,mihuri sahihi na kuchelewa kurudisha fomu na kutoa vizingizo ni ugonjwa wa wapinzani
mwaka 2000,mgombea wa chadema alichelewa kurudisha fomu akasingizia kawekewa trekta!
Njelu kasaka,aliwekewa pingamizi kwa kuwa ana muhuri wa katibu wa jimbo chadema,badala wa wilaya,fasta siku hiyo hiyo ya mwisho akajiunga na cuf huko Lupa,akaishia kuchelewa kurudisha fomu
2018,chadema wanamleta Salum mwalimu kinondoni,kaulizwa unaishi mtaa gani anajiuma uma tu,ni busara ya tume tu,lilimrudisha kwenye kinyang'anyiro,akini hakujipigia kura
2018 chadema wanatuma wagombea udiwani wawili wawili huko mbeya,matokeo yake wote wamepoteza
2015,iliwachukua chadema dakika tisini kumsimamisha mgombea ambae hajui hata ubeti mmoja wa katiba,na walimtukana sana mpaka siku ya uteuzi wake
Mifano ni mingi,lakini kwa hiyo michache utagundua Tanzania hatuna wapinzani,tuna wapiga kelele tu
Wakati ccm wanateua mgombea na kurudisha fomu,kina mashinji walikua bize mitandaoni kuishambulia dreamliner kuwa imekufa mwanza
 
Watangazaji sio wachambuzi... Wanajivika majukumu ya siyo yao....ndio maana uchambuzi wao ni mashudu....Kibwana na wenzake kazi zao ni kuripoti matukio l.... Uchambuzi ni Akili kubwa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tufike mahali tuwe tunatumia akili zetu si zawawekezaji.
1. Awali tulisema hatutasimamisha mgombea kutokana na rafu zao natukaamini ndio msimamo wetu tukihitaji mabadiliko tume ila hayakufanyika zaidi ya Kailima kwenda jikoni tena na aliyekuja ndio Master wa rafu.

2. Ni bora kuwaacha wajipitishe hta bila ya kupingwa nafikiri wabane matumizi
Kususia jambo ni kiwango cha chini sana cha kukata tamaa,hivi ukimsusia fisi zizi itakuaje nani atakaeumia,pale wamepima uwezekano wa kushinda haupo,fanya utafiti sehemu zote zenye ngome zao zenye uhakika wa kushinda hawafanyi figisu figisu.Figisu utazikia Arusha,Kilimanjaro, Kigoma,Mbeya,Mara,Mwanza,nk mambo hayo uyasikii Dodoma, Tabora,nk.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja yako haindoi hoja ya Kibwana.
Naafiki. nadhani tuanzishe Maktaba maalum, Collection maalum ya matendo maovu na figisu za Serikali ya Awamu ya Tano, ambayo itajumuisha"
1) Maagizo ya Rais ambayo ni kinyume cha katiba, mfano amri ya kuwataka vyama vya upinzani waache mikutano na maandamano wasubiri 2020. Video alizoongea hayo zihifadhiwe
2) Maagizo ya watendaji wake ambayo yanakiuka katiba. Kuna agizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, kwamba wanaCCM wawafanyie fujo wabunge wa upinzani. hili siyo tu ni kinyume cha sheria na katiba, bali pia linaudhi na lina ukakasi
3) Matendo ya wagombea wa upinzani kunyang'anywa fomu, fomu feki kupokelewa na wasimamizi, kupigwa, kuteswa, kupotezwa, nk.
 
At least Mindi umekwishaona nini kinaendelea nchini please tumia ushawishi wako kuelimisha wengi...kwani uimara unaoneshwa na upinzani kwasasa ni upendo wa hali ya juu haijawahi kutokea...simply they have shown us that they are devoting and dedicating their lives just for us all we poor cowards of the country.
Umeona eeh? ila mkuu wala sina ushawishi kihivyo, ila cha msingi tusiache kuyajadili haya mambo kwa njia hii na nyinginezo. maana wengine huwa yanawapita mambo kama haya
 
Back
Top Bottom