Kwako Kaka yangu ,Albert Msando

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,875
Kwanza napenda kukupongeza sana,kwa jitihada na moyo wako wa kusaidia jamii yetu.Umekuwa mfano bora kabisa katika jamii yetu na kwetu vijana.

Tuliona ulijitoa kuchangisha milioni 5 ,kumsaidia Mh.Rais kulipa deni la yule mama yetu aliyefiwa na mama yake Muhimbili .Na hakika leo tumeona umekabidhi fedha hizo hospital ya Muhimbili ,hongera sana kaka yetu.

Ila ,Mimi napata kukufananisha na kijana mmoja mwenye huruma sana anaitwa *Kalukalanga* , Siku moja Kalukalanga alipita msituni akakuta nyumba moja ikiwa imejitenga, alivyopita njiani karibu na nyumba ile akasikia sauti ya wamama wakilia kwa uchungu waokolewe kutoka katika chumba kimoja ,chenye giza kidogo.

Kalukalanga akachungulia dirishani ukamuona mmoja wa mama akilia kwa sauti akihitaji maji ya kunywa, huku mama wengine wakiwa wamelegea sauti hazitoki kwa unyonge .

Kalukalanga alivyojaliwa huruma ,akakimbia haraka kutafuta maji , akiomba huku na kule kwa rafiki zake na majirani zake ili chupa lijae akampe maji mama yule .

Alijaliwa kuyapata akampelekea mama yule dirishani ,yule mama akanywa .Kalukalanga akaondoka huku akisema moyoni nimemsaidia mama yule.


Kalukalanga hakujali kuwa mama yule hayupo pekeake katika kile chumba, bali wapo wengi katika chumba kile ,ila sababu walikuwa wamedhoofu hawakuweza kutoa sauti zao ila sauti ya mama yule mmoja ilipaswa kubebwa na Kalukalanga kwa uzito zaidi kama sauti wakilishi ya wamama wote mule ndani.


Pia Kalukalanga alijua amempa msaada mama yule ,ila Kalukalanga hakuwaza nani atakaye mpa tena mama yule maji au chakula hapo baadaye ikiwa sehemu ile hakuna wapitanjia wengi.

Msaada mkubwa Kalukalanga angeufanya kupitia sauti ya mama yule mmoja,angetafuta namna ya kuwaokoa wale wa mama kutoka katika chumba chenye giza ,mateso na unyong'onyefu kuliko kumpa maji tuu na kuondoka kwa kufikiri ametoa msaada wa kutosha.Ndio ni msaada ila sio msaada wa kutatua tena kiu chake hapo baadaye ,ikiwa maji yenyewe alikunywa yote sababu ya uchache.

Watanzania ni maskini , mikakati imara ya kusaidia upatikanaji rahisi wa huduma ya afya kwa mfumo wa pamoja ili kusaidia wengi zaidi.Kuliko mmoja mmoja ! Yes ni vyema mama alipaswa kusaidiwa ila tunapaswa kwenda mbali zaidi ,msaada alioupata ,anaweza uomba tena kama akipata shida kama hiyo siku zijazo .

Kipato cha mtanzania kwa mwaka ni Mil.2.4

Pia ndicho kipato cha yule mama hospital ,ambapo kama hana ajira rasmi anapaswa awe na mil,1.5 kwa mwaka kulipia bima ya afya .

Ripoti ya Sikika inasema asilimia 80 ya watanzania hawana Bima ya afya. Sababu ya bei ghali ya Bima, tunawezaje kufikia Universal health Coverage (UHC) ifikapo 2030 kwa namna hii?

Lazima tuangalia namna ya kusaidia jamii yetu kupata huduma bora, rahisi na nafuu.

Mnaepuka majukumu msiulizwe maswali mengi kwa kujificha nyuma ya mgongo wa Bima ya afya ya jamii (improved community health fund) iCHF .

Mnajua changamoto ya mfuko huu ? ,Kwanza sio mpya , Sheria ya kuanzisha mfuko huu imetungwa tangu 2001 ,kwa sheria ya Bunge No.1 ya 2001 ,mnaweza kutuambia kiasi gani mfuko huu umeimarika ndani ya miaka 18 tangu 2001 ,Mfuko huu unachangamoto nyingi,ndio maana hata wananchi hawaujui .

Nitaziandika siku moja changamoto zake.

Ila tunapaswa kufikiria kwa mapana kusaidia jamii yetu , katika suala la afya na sio kuchangia mmoja mmoja , watanzania ni wengi wenye matatizo hayo.

Shukrani Kaka yangu ,Msando .

Abdul Nondo.
 
Kwanza napenda kukupongeza sana,kwa jitihada na moyo wako wa kusaidia jamii yetu.Umekuwa mfano bora kabisa katika jamii yetu na kwetu vijana.

Tuliona ulijitoa kuchangisha milioni 5 ,kumsaidia Mh.Rais kulipa deni la yule mama yetu aliyefiwa na mama yake Muhimbili .Na hakika leo tumeona umekabidhi fedha hizo hospital ya Muhimbili ,hongera sana kaka yetu.

Ila ,Mimi napata kukufananisha na kijana mmoja mwenye huruma sana anaitwa *Kalukalanga* , Siku moja Kalukalanga alipita msituni akakuta nyumba moja ikiwa imejitenga, alivyopita njiani karibu na nyumba ile akasikia sauti ya wamama wakilia kwa uchungu waokolewe kutoka katika chumba kimoja ,chenye giza kidogo.

Kalukalanga akachungulia dirishani ukamuona mmoja wa mama akilia kwa sauti akihitaji maji ya kunywa, huku mama wengine wakiwa wamelegea sauti hazitoki kwa unyonge .

Kalukalanga alivyojaliwa huruma ,akakimbia haraka kutafuta maji , akiomba huku na kule kwa rafiki zake na majirani zake ili chupa lijae akampe maji mama yule .

Alijaliwa kuyapata akampelekea mama yule dirishani ,yule mama akanywa .Kalukalanga akaondoka huku akisema moyoni nimemsaidia mama yule.


Kalukalanga hakujali kuwa mama yule hayupo pekeake katika kile chumba, bali wapo wengi katika chumba kile ,ila sababu walikuwa wamedhoofu hawakuweza kutoa sauti zao ila sauti ya mama yule mmoja ilipaswa kubebwa na Kalukalanga kwa uzito zaidi kama sauti wakilishi ya wamama wote mule ndani.


Pia Kalukalanga alijua amempa msaada mama yule ,ila Kalukalanga hakuwaza nani atakaye mpa tena mama yule maji au chakula hapo baadaye ikiwa sehemu ile hakuna wapitanjia wengi.

Msaada mkubwa Kalukalanga angeufanya kupitia sauti ya mama yule mmoja,angetafuta namna ya kuwaokoa wale wa mama kutoka katika chumba chenye giza ,mateso na unyong'onyefu kuliko kumpa maji tuu na kuondoka kwa kufikiri ametoa msaada wa kutosha.Ndio ni msaada ila sio msaada wa kutatua tena kiu chake hapo baadaye ,ikiwa maji yenyewe alikunywa yote sababu ya uchache.

Watanzania ni maskini , mikakati imara ya kusaidia upatikanaji rahisi wa huduma ya afya kwa mfumo wa pamoja ili kusaidia wengi zaidi.Kuliko mmoja mmoja ! Yes ni vyema mama alipaswa kusaidiwa ila tunapaswa kwenda mbali zaidi ,msaada alioupata ,anaweza uomba tena kama akipata shida kama hiyo siku zijazo .

Kipato cha mtanzania kwa mwaka ni Mil.2.4

Pia ndicho kipato cha yule mama hospital ,ambapo kama hana ajira rasmi anapaswa awe na mil,1.5 kwa mwaka kulipia bima ya afya .

Ripoti ya Sikika inasema asilimia 80 ya watanzania hawana Bima ya afya. Sababu ya bei ghali ya Bima, tunawezaje kufikia Universal health Coverage (UHC) ifikapo 2030 kwa namna hii?

Lazima tuangalia namna ya kusaidia jamii yetu kupata huduma bora, rahisi na nafuu.

Mnaepuka majukumu msiulizwe maswali mengi kwa kujificha nyuma ya mgongo wa Bima ya afya ya jamii (improved community health fund) iCHF .

Mnajua changamoto ya mfuko huu ? ,Kwanza sio mpya , Sheria ya kuanzisha mfuko huu imetungwa tangu 2001 ,kwa sheria ya Bunge No.1 ya 2001 ,mnaweza kutuambia kiasi gani mfuko huu umeimarika ndani ya miaka 18 tangu 2001 ,Mfuko huu unachangamoto nyingi,ndio maana hata wananchi hawaujui .

Nitaziandika siku moja changamoto zake.

Ila tunapaswa kufikiria kwa mapana kusaidia jamii yetu , katika suala la afya na sio kuchangia mmoja mmoja , watanzania ni wengi wenye matatizo hayo.

Shukrani Kaka yangu ,Msando .

Abdul Nondo.
🤣🤣🙌🏾
 
Na wewe unaweza ukawa Kalukalanga kusaidia pale alipoishia Kalukalanga.., mimi sina tatizo la watu binafsi kutoa kitu.., ila kutumia utoaji wa kitu kama promo.., kama kweli ingekuwa msaada hakuna sababu ya jamii kujua

Pili vyombo kama serikali na taasisi nyingine zinazoongozwa na watu tunaowalipa na kutumia kodi zetu hazipaswi kusema zinatoa misaada.., bali zifanye kazi zao na zingefanya kazi zake hao watu wasingekuwa kwenye hayo matatizo...

Haiwezekani watu wanakunywa wine huku wananchi hawana hata maji na wakilalamika wanawapa umande walambe lambe alafu wanategemea tuwasifu kwa kuwapa watu umande ?...,
 
Yawezekana alberto msando amefanya kama huyu kalukalanga uliyemtolea mfano..lakini swali la kujiuliza ni leo tu msando amejitokeza kuisaidia jamii?vipi kuhusu wale watoto wa chuo kikuu cha Dar ambao walikosa ada na yeye akachangisha na mpaka sasa wanaendelea na masomo na wengine wamemaliza degree zao?lakini kingine wewe ambaye sio kalukalanga umefanyanini ili kusaidia jamii inayokuzunguka?
 
Na wewe unaweza ukawa Kalukalanga kusaidia pale alipoishia Kalukalanga.., mimi sina tatizo la watu binafsi kutoa kitu.., ila kutumia utoaji wa kitu kama promo.., kama kweli ingekuwa msaada hakuna sababu ya jamii kujua

Pili vyombo kama serikali na taasisi nyingine zinazoongozwa na watu tunaowalipa na kutumia kodi zetu hazipaswi kusema zinatoa misaada.., bali zifanye kazi zao na zingefanya kazi zake hao watu wasingekuwa kwenye hayo matatizo...

Haiwezekani watu wanakunywa wine huku wananchi hawana hata maji na wakilalamika wanawapa umande walambe lambe alafu wanategemea tuwasifu kwa kuwapa watu umande ?...,
pesa zimechangwa na umma hivyo kukabidhiwa kwake kwa walengwa ni busara pia umma ujue kama ilivyofanyika.
 
Kwanza napenda kukupongeza sana,kwa jitihada na moyo wako wa kusaidia jamii yetu.Umekuwa mfano bora kabisa katika jamii yetu na kwetu vijana.

Tuliona ulijitoa kuchangisha milioni 5 ,kumsaidia Mh.Rais kulipa deni la yule mama yetu aliyefiwa na mama yake Muhimbili .Na hakika leo tumeona umekabidhi fedha hizo hospital ya Muhimbili ,hongera sana kaka yetu.

Ila ,Mimi napata kukufananisha na kijana mmoja mwenye huruma sana anaitwa *Kalukalanga* , Siku moja Kalukalanga alipita msituni akakuta nyumba moja ikiwa imejitenga, alivyopita njiani karibu na nyumba ile akasikia sauti ya wamama wakilia kwa uchungu waokolewe kutoka katika chumba kimoja ,chenye giza kidogo.

Kalukalanga akachungulia dirishani ukamuona mmoja wa mama akilia kwa sauti akihitaji maji ya kunywa, huku mama wengine wakiwa wamelegea sauti hazitoki kwa unyonge .

Kalukalanga alivyojaliwa huruma ,akakimbia haraka kutafuta maji , akiomba huku na kule kwa rafiki zake na majirani zake ili chupa lijae akampe maji mama yule .

Alijaliwa kuyapata akampelekea mama yule dirishani ,yule mama akanywa .Kalukalanga akaondoka huku akisema moyoni nimemsaidia mama yule.


Kalukalanga hakujali kuwa mama yule hayupo pekeake katika kile chumba, bali wapo wengi katika chumba kile ,ila sababu walikuwa wamedhoofu hawakuweza kutoa sauti zao ila sauti ya mama yule mmoja ilipaswa kubebwa na Kalukalanga kwa uzito zaidi kama sauti wakilishi ya wamama wote mule ndani.


Pia Kalukalanga alijua amempa msaada mama yule ,ila Kalukalanga hakuwaza nani atakaye mpa tena mama yule maji au chakula hapo baadaye ikiwa sehemu ile hakuna wapitanjia wengi.

Msaada mkubwa Kalukalanga angeufanya kupitia sauti ya mama yule mmoja,angetafuta namna ya kuwaokoa wale wa mama kutoka katika chumba chenye giza ,mateso na unyong'onyefu kuliko kumpa maji tuu na kuondoka kwa kufikiri ametoa msaada wa kutosha.Ndio ni msaada ila sio msaada wa kutatua tena kiu chake hapo baadaye ,ikiwa maji yenyewe alikunywa yote sababu ya uchache.

Watanzania ni maskini , mikakati imara ya kusaidia upatikanaji rahisi wa huduma ya afya kwa mfumo wa pamoja ili kusaidia wengi zaidi.Kuliko mmoja mmoja ! Yes ni vyema mama alipaswa kusaidiwa ila tunapaswa kwenda mbali zaidi ,msaada alioupata ,anaweza uomba tena kama akipata shida kama hiyo siku zijazo .

Kipato cha mtanzania kwa mwaka ni Mil.2.4

Pia ndicho kipato cha yule mama hospital ,ambapo kama hana ajira rasmi anapaswa awe na mil,1.5 kwa mwaka kulipia bima ya afya .

Ripoti ya Sikika inasema asilimia 80 ya watanzania hawana Bima ya afya. Sababu ya bei ghali ya Bima, tunawezaje kufikia Universal health Coverage (UHC) ifikapo 2030 kwa namna hii?

Lazima tuangalia namna ya kusaidia jamii yetu kupata huduma bora, rahisi na nafuu.

Mnaepuka majukumu msiulizwe maswali mengi kwa kujificha nyuma ya mgongo wa Bima ya afya ya jamii (improved community health fund) iCHF .

Mnajua changamoto ya mfuko huu ? ,Kwanza sio mpya , Sheria ya kuanzisha mfuko huu imetungwa tangu 2001 ,kwa sheria ya Bunge No.1 ya 2001 ,mnaweza kutuambia kiasi gani mfuko huu umeimarika ndani ya miaka 18 tangu 2001 ,Mfuko huu unachangamoto nyingi,ndio maana hata wananchi hawaujui .

Nitaziandika siku moja changamoto zake.

Ila tunapaswa kufikiria kwa mapana kusaidia jamii yetu , katika suala la afya na sio kuchangia mmoja mmoja , watanzania ni wengi wenye matatizo hayo.

Shukrani Kaka yangu ,Msando .

Abdul Nondo.
Unajua haya mambo bana, sisi wengine tuliotoka mbali na haya mambo ya siasa tunawachora tu. Yaani wewe Nondo sasa unampiga shule Msando! Anyway labda ndio maana hatufanani, endeleeni na porojo zenu!

Hivi Msando yule enzi zile(tuachane na sasa) na huyu dogo ungeweza kuwaweka kapu moja? Dogo ushauri wangu wa bure kwako, achana na watu, focus kwenye issues! Nimemaliza.
 
Unajua haya mambo bana, sisi wengine tuliotoka mbali na haya mambo ya siasa tunawachora tu. Yaani wewe Nondo sasa unampiga shule Msando! Anyway labda ndio maana hatufanani, endeleeni na porojo zenu!

Hivi Msando yule enzi zile(tuachane na sasa) na huyu dogo ungeweza kuwaweka kapu moja? Dogo ushauri wangu wa bure kwako, achana na watu, focus kwenye issues! Nimemaliza.

Ishu hazitoki hewani, Ishu zinatokana na watu!
Hujamaliza, umekimbia hoja!

Hili andiko la Abdu Nondo ni zuri na ni fikirishi sana!
Msando eti anamsaidia raisi kumchangia mwenye uhitaji wa pesa ya kukomboa mwili wa marehemu wake: Difficult to comprehend!.
Raisi ambaye ana mamlaka ya kumwagiza waziri na waziri akamwagiza mkurugenzi wa Muhimbili aachie miili yote ya wanaokufa pale bila kuwatoza hata senti Moja , Kama akitaka!

Hapa nchini kuna wenye uhitaji wangapi?, kumsaidia mmoja kuna msaada gani kwa Taifa?, Tulitegemea Msando akiendesha juhudi tuone Coverage ya health care kwa watu wengi zaidi siyo kutafuta kiki!.

Kama kusaidia anaweza kwenda kumtafuta huyo mama peke yake kimyakimya na kusaidia kuliko kuanzisha mass movement kwa jina la Rais eti kutoa msaada!. Absurd!!!
 
pesa zimechangwa na umma hivyo kukabidhiwa kwake kwa walengwa ni busara pia umma ujue kama ilivyofanyika.
Kuchangisha pesa UMMA na Harambee zisizoisha ni kuwa na taifa la ombaomba bila watu kufanya wajibu wao.. yule mama anayechangiwa hakupaswa kuwepo katika hali ile kama watu katika nafasi zao wangewajibika.., na tutaendelea kuchangishana mpaka lini badala ya kuchangishana pesa za kupumzisha tatizo tuchangishane mawazo ya kuondoa tatizo.. (na kama sikosei kuna watu tunawalipa na wanakula kodi zetu ili walete mawazo mbadala ila wanchofanya ni business worse than usual)
 
Haya masuala ya mwili wa marehemu kuwa Collateral ili bili ilipwe tulikuwa tunayasikia Kenya. Awamu hii kuna ndugu wa marehemu wanaoweka hati za nyumba kama Collateral ili wakomboe maiti.

Tunatakiwa tuwe na mfumo wa huduma za Afya ambao utawahusu Watanzania wote.Najiuliza akitokea ndugu mwingine ambaye ameshindwa kumkomboa ndugu yake ili akamzike,Msando atajitokeza tena kumchangia?
 
Dogo wa pafyumu utakufa na kihoro!

Yaani wewe kijambanani wa juzi kati unataka umpe Shule Msando!?Wendawazimu!

Sura yako inaakisi pafyumu zile.
 
Unajua haya mambo bana, sisi wengine tuliotoka mbali na haya mambo ya siasa tunawachora tu. Yaani wewe Nondo sasa unampiga shule Msando! Anyway labda ndio maana hatufanani, endeleeni na porojo zenu!
Siwajui wote hao hapo juu..., ila ninachokijua hakuna mwenye hati miliki ya kutoa mawazo au fikra vilevile even the broken clock is right once a day
 
Dogo ni bora ungetulia kwanza ujifunze mambo kwa uelewa mpana. ..
Msando hana mpango na hayo maelezo marefu ulioweka hapo. . Anatafuta long term benefit na political lift....
Mambo sijui ya CHF sijui nini ni hisia zako tu...
Kwani unadhani mjomba hazijui?
Be smart, learn, research then talk
 
Back
Top Bottom