Kwako dr.slaa:tafadhali cdm isijibu hoja za prof.lipumba

Lu-ma-ga

JF-Expert Member
Sep 21, 2010
4,780
3,227
Mhesimiwa Dr.Slaa pamoja na uongozi mzima wa CDM,
Sisi watanzania tunajua fika kuwa chama chenu kwa sasa kimebeba majukumu ambayo yalipaswa kutimizwa na chama tawala(CCM), lakini chama hicho tawala kinaelekea kusambalatika muda si mrefu.Sisi watanzania tunahitaji kupata updates za utekelezaji wa serikali yetu kama inakwenda sawa au la, kwa bahati mbaya serikali ya JK imeparaganyika kiasi kwamba haina tena uwezo wa kuwashirikisha watanzania katika kupata habari.

Tegemeo letu kwa sasa ni CDM ndicho chombo huru ambacho kinatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kupata habari muhimu ambazo serikali ya CCM inajitahidi sana kuzificha.
Chama chenu(CDM) kwa sasa ni sawa na mti wa matunda ambao kila anayehitaji kupata tunda lazima arushe jiwe, leo hata Prof.Lipumba anahitaji kula tunda la mti unaoitwa CDM.
Dr.Slaa na timu yako tunawaomba msipoteze muda kujibu hoja za Prof. Lipumba huyo mwacheni, anatafuta publicity ambayo kuipata kirahisi lazima ataje CHADEMA VEMA.
Msipoteze muda tutaibiwa na haya majambazi, hakikisheni mnayakurupusha kila saa,tafadhali msiyape muda, yana lengo la kuchukua chao mapema kwani tayari yamegundua chama kinakufa.

Ni hayo tu.
PEOPLESSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS POWER
 
Back
Top Bottom