Kwako Boss/ Mwajiri nadhani ukifanya hivi itapendeza sana

CONTROLA

JF-Expert Member
Sep 15, 2019
6,939
22,989
  • Acha mazoea yaliyozidi na kuvuka mipaka na Watumishi/wafanyakazi wako
Hapa naongelea yale mazoea Too much ya boss na mfanyakazi, kama unajijua unataka kazi ziende epuka mazoea ya namna hiyo.

Mfano unaweza kukuta mfanyakazi anamtania boss wake "boss demu wako anakuita" na anajua fika boss wake ana mke na watoto.

Huu utani wa namna hii sio mzuri na haufai,yapo mazoea ya aina nyingi ila cha kuzingatia awe na mipaka.
  • Kukaa ofisini/dukani na Mfanyakazi
Unapoamua kuajiri kwanza ajiri mtu unaemuamini na umejiridhisha na tabia yake,unapomleta dukani/ofisini baada ya kujiridhisha kua kasha master biashara inendaje ni wakati wako sasa wa kumuacha na kumpa uhuru afanye kazi kwa bidii.

Yawezekana una duka moja na huna mahali pa kwenda basi nashauri dukani toka kaa hata huko nnje ya duka muache dukani akae yeye wateja wakija aongee nao yeye.

Kukaa na boss mbele yake kunampotezea ujasiri wa kuongea na mteja.

Mfano: Mfanyakazi wa kike then mteja kaja wakiume Moja ya mbinu ya mfanyakazi wako ili yule mteja anunue kitu ni kuji bebisha kwake na kum bembeleza.

Sasa boss unapokuwa eneo la tukio unamfanya mfanyakazi ashkndwe tumia tekniki za kazi kwa kukuogopa utamchukuliaje nk nk.
  • Zawadi
Wewe ni boss/mwajiri yawezekana huonekani kazini mara kwa mara na hata ukija onekana ni mtu serious serious jambo linalopelekea wafanyakazi kukuogopa na kukuheshimu kupitiliza.

Heshima ya kupitiliza ni ile unaingia kazini mfanyakazi anakusalimia shikamoo, unatoka nje ukirudi ndani anahisi kama hajakusalimia anakusalimia tena.

Hapo fahamu tu kuwa unaogopwa.

ili kutengeneza/kuimarisha mahusiano mazuri kati yako na team yako si mbaya kama mara moja moja ukawa unawapa zawadi staff wako.

Zawadi inaweza kuwa chochote ambacho kipo ndani ya uwezo wako. Hata kama wewe ni mama ntilie uwezo unao wakuwapa wafanyakazi wako zawadi.

Unaonaje siku 1 ukajitoa fahamu ukawmbia wafanyakazi wako wajipikie Chakula wanachotaka wa kula kuku ale, paka ale,mbwa ale wape pesa wakanunue mahitaji yote wayatakayo sio kila siku unawalisha ugali wali ugali wali.

Kama una duka la nguo unaweza jitoa ufahamu tu siku ukamwambia mfanyakazi achague nguo anayotaka avae.

Mfanye ajisikie raha na bahati kupata boss kama wewe, unaweza mlipa mtu mshahara mdogo ila kutokana na jinsi unavyoishi naye ukajikuta anadumu kwako hadi unashangaa.
  • Mapumziko
Asee hamna mtu asie choka hata huyo mfanyakazi wako bora ambae hujui anaumwaga lini, anafua saa ngapi,analala saa ngapi usifikiri hachoki, anachoka sana tu ila anafanya yote hayo ili tu "kulinda kibarua" ila laiti ungekua na camera umuone akirudi nyumbani usiku anavyokuaga kalegea kwa uchovu ungemuonea huruma.

Wape/mpe wafanyakazi wako mapumziko hata kama yeye atakwambia sijachoka "usimsikilize" ni muongo hawezi kukwambia kachoka hata siku 1 maana anajua utamuona lege lege hivyo basi Mapumziko ni lazima na sio ombi, wape nafasi wapumzike,wape nafasi yakufanya mambo yao,mfanye ajione kuwa nae yupo huru na si kwamba ni MTUMWA mpe uhuru kabisa.

Mueleze faida za kupumzika maana kusema ukweli kuna wafanyakazi hawataki Off wapo kama vile marobot ni vizuri saawa mtu afanye kazi ila hapana isizidi bwana hata yeye ni binadamu anahitaji kusaidiwa kupumzishwa.
  • Mavazi
Katika kitu kitaongeza thamani kuanzia kwako/ofisi/wafanyakazi wako ni ule utambulisho wenu kwa wateja SARE (hasa tshirt) ni muhimu kupita jambo lolote,bkwanza kunafanya mteja awe na amani na ujasiri wa kumuita mfanyakazi bila wasi wasi wowote kuhofia "labda si mfanyakazi".

Yawezekana una duka hata la kawaida una kijana wako m1 mtafutie tshirt 1 ya form six rangi flani iwe ndio sare yake ya kazini.

Chini avae suruali/skirt,nl vyvyte ila juu hakikisha mtu yeyote anaefanya kazi kwenye ofisi yako ana utambulisho wa sare, kuna faida sana eneo hili.

Tumeshazoea kuona wahudumu wa bar tu ndio wana sare lakini nani kasem sare ivaliwe na wahudumu tu?

Sare ya kazi inatakiwa iwe kila mahali hvyo na wewe kama unapenda kuwa Boss/mwajiri unaejillewa usikubali wafanyakzi wafae watakavyo wanapokua eneo la kazi.
  • Kuajiri Ndugu
Point hiii nisiisemee maneno mengi ila naomba tu nikushauri jambo kama unawapenda ndugu zako sana sana kuliko uwape ajira kwenye ofisi zako ni mara 1000 upambane kufa na kupona umtafutie ajira sehemu fulani najua una connection huwezi kosa,mtafutie aende huko ila ukitaka kubugi muajiri ofisi yako na mshahara mlipe wewe, huwezi elewa ila kama ni mbishi we ajiri tu.
  • Mahusiano ya kimapenzi ofisini
Hii nayo haina maelezo mengi maana inaeleweka ni marufuku mfanyakazi kwa mfanyakazi kudate, Boss na mfanyakazi, Mfanyakazi na Mteja kote huko ni marufuku tena kubwa,bila kama utaona hili halina umuhimu wewe lipuuzie wape uhuru wajitawale eneo hilo wakishatendana huko stress wazilete kazini ndio utaelewa nilikuwa namaanisha nini.
 
Sioni tatizo la kuajiri ndugu, ili mradi kila mmoja atapewa Mkataba Wa Kazi Na Job Description.
 
Bonge la thread..But litapata wachangiaji wachache.. Wadau wapo kule kwenye ule Uzi wa kueleza Namna ulivyokula tunda kimasihara uzi umetembea page ya 5.. Back to the topic umesahau kale katabia Cha kichawi kwa waajiri wengi kuwa na wasiwasi wa kuibiwa na wafanyakazi wake Yaani asimuone mfanyakazi kanunua kitu kipya tayari anaanza kumletea nongwa, Yaani wanatamani mfanyakazi aendelee kupauka na kuonekana katika hali mbaya. Mimi nimebarikiwa roho ya kitajiri Kama mtu anafanya kazi zangu vizuri Sina noma kumuona akifanya maendeleo... Waajiri wengi Awana hiyo.
 
Nasikia haka ka tabia ka kusalimiana mara kwa mara wanako wasukuma, mtasalimiana hapa lakini baada ya dakika mbili utasikia tena 'ulimola bhagosha' na usipoangalia hadi kuku na bata watapewa salamu
 
I think waajiri na waajiriwa likija kwenye hili suala la kazi wengi wao huajiriwa kiholela bila mikataba wala policy hii hali hupelekea muajiriwa kushindwa kudai haki yake pale muajiri wake anapomletea manyanyaso au kutomlipa mshahara kwa wakati hasa wale wamajumbani nazungumzia dada wakazi/housegirl na shambaboi/house boy/Gardner nafikiri waajiri woote wakiwapa nmikataba wafanyakazi wao watasaidia kuondoa au kupunguza mitafaruko ndani ya sehemu zakazi.



Bila kusahau child labor is a crime Ukiona jirani yako anamtumikisha mtoto au kijana chini ya miaka 17 unatakiwa kumripoti kwa vyombo husika maana hao ni wahanga wakuu wa manyanyaso hupewa mshahara mdogo na wengine kunyanyaswa kijisia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo point ya kuajiri ndugu naielewa kiundani kabisa...sitasahau mdogo wangu mtoto wa mama yangu mdogo alichonifanyia kwenye duka langu la jumla pale Tip Top mwaka 2012 aiseeee...ndugu waache wabaki kua ndugu tu la sivyo mtaishia kwenye uhasama mkubwa saaaana na migogoro isiyoisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sioni tatizo la kuajiri ndugu, ili mradi kila mmoja atapewa Mkataba Wa Kazi Na Job Description.
Huoni tatizo ila lipo tatizo

assume umemuajiri mkeo,wiki ya kwanza mtoto wako nyumbani kaumwa (wewe shahidi unamuona mtoto home) hata kama mkataba umeweka wa vipi,lazima utamruhus abaki home amuuguze mtoto.

Akibaki home kumbuka kazini nafasi yake inabaki wazi, ile mtoto amepona tu Unapokea simu kuwa mama mkwe wako kaumwa kalazwa anatakiwa mkeo aende kumuuguza (sijui kama una ubavu wa kumnyima ruhusa)

Ametoka kumuuguza mama mkeo karudi nyumbani kachoka umemuona kbsa hali yake na bahati mbaya tumbo lianza kumuuma usiku,kesho ni J3 ntaona kama una ubavu wa kumwambia a report kazini saa mbili kamili.

Piga muda aliokaa mkeo huyo nnje ya ofisi kuanzia mtoto kaumwa,mama mkwe aumwe,yeye aumwe piga hesabu za muda ambao hajaingia kazini halafu urudi uniambie "mkataba utakua na kazi gani kwa watu wa namna hiyo Ndugu"
 
Nasikia haka ka tabia ka kusalimiana mara kwa mara wanako wasukuma, mtasalimiana hapa lakini baada ya dakika mbili utasikia tena 'ulimola bhagosha' na usipoangalia hadi kuku na bata watapewa salamu
wasikusikie mkuu,punguza sauti
 
Back
Top Bottom