Kwaheri mbowe, kwaheri chadema

TheMaster

Member
Joined
Aug 10, 2023
Posts
61
Reaction score
131
Huko miaka ya 2000s baba aliwahi kunambia kuwa Mbowe na ZZK ni vijana wa mfumo, wanaeongoza vyama vya upinzani lakini kwa kulinda na kusimamia miongozo waliyopewa na mfumo.

Kitendo cha Mbowe kukabidhi madaraka kwa mtu mwengine rasmi inaonesha hatokuwa na mamlaka tena ya kutaka na kuamua namna gani chama kitajiendesha.

Nimetafakari mambo mawili unprecedented yalojitokeza baada ya Mbowe kuaga uenyeketi.

1. Kiongozi wa Chama cha CHADEMA kutuhumiwa hatia ya Uhaini, kitu ambacho hakikuwahi kutokea kwa kiongozi yeyote wa chama kabla.
2. CHADEMA kutokushiriki uchaguzi mwaka 2025-2030; hii huwenda ikaiondoa kabisa CHADEMA kwenye ramani ya kisiasa Tanzania kwasababu ni hatari kujiita chama kikuu cha upinzani bila uwakilishi wowote kwenye dimba za kisiasa hususani Bungeni na baraza la uwakilishi kadhalika nafasi za udiwani.
Hadi mwaka 2020, CHADEMA itakuwa imeshapoteza umaarufu na mvuto kwa kiasi kikubwa saana.

Kuondoka kwa mbowe, kumefunga milango ya hikima na busara CHADEMA

Kuondoka kwa Mbowe kumezima Nuru ya Chama, mwanga wa kibatari unaoelekea kuzima unategemea zaidi busara za Utawala na sio uongozi wa Chama husika.

KWAHERI MBOWE, KWAHERI CHADEMA
 
Mbowe alikaa Gereza Kwa Kesi ipi??.

Wewe ni mwanaCCM au G 55, nmekumis kufuatia CDM kutosain takataka za Jaña.



CDM HAIFI ng'ooooo
 
 

Attachments

  • 6028918-c90487a0a3c9f670172c401e803cbac6.mp4
    3.5 MB
Duh!!👿
 
2019-2024 tulitoka wabunge zaidi ya 70 hadi mbunge 1 ila chama hakikufa kipi kipya ambacho hatujapitia hii miaka 5 kisuggest tutakufa? Chadema ni imani kimeshavuka kuitwa chama, hiki chama kina hard-core followers ndio maana kilivuka miaka hii 5 bila ruzuku wala wabunge na madiwani.

Chama sio wabunge, chama ni WANACHAMA.
 
Kama mpaka Leo hii Kuna wapenzi na mashabiki wa pan African sports club ya enzi hizo wakati
Kama mpaka Leo Kuna wapenzi na mashabiki wa pan African sports club ya enzi hizo ilihali club hiyo haishiriki ligi yoyote basi cdm haitokufa bali mtakufa ninyi mahasimu!
 
Kuondoka kwa Mbowe kumezima Nuru ya Chama, mwanga wa kibatari unaoelekea kuzima unategemea zaidi busara za Utawala na sio uongozi wa Chama husika.
Mbowe ndio aliasisi no reform no election pia Mbowe na busara zake tumekosa mbunge wala diwanii miaka 5 kwahiyo kama busara zake hazikusaidia je zingesaidia nini kwa sasa?
 
Chama kinaongozwa na wanaharakati kutoka nje ya nchi
 
7
 

Attachments

  • cf0ea736521de32f5d65e1a6b7fd56a4_1743187151179.mp4
    579.6 KB

Tofautisha Gaidi na Mhaini
Lissu kukaa mahabusu siku mbili analialia
 
Lakni bado mnateseka na chdema kisa hakutia saini ya ukuwadi isiyokuwa sheria bali matakwa ya ccm kisa kudai no reform no election.
 
Kwakukusaidia tu sasa cdm iko kwenye mikono ya wananchi na sio zaidi ya hapo. Na kwahiki kinachoendelea cdm imepoteza pambano na sio vita.
 
Mkuu, mbona hausomeki? Unasema "hadi 2020, CHADEMA itakuwa imepoteza umaarufu" hayo ni ya kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…