Kwaheri Lowassa, kwaheri CHADEMA...

Kwaheri Lowassa, kwaheri CHADEMA...

Linamo

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2011
Posts
9,976
Reaction score
24,498
Nianze kwa kukupa pole Lowassa,halafu nikuage.

Ulichokifanya Jana pale jangwani kimedhihirisha kabisa wewe ni msanii wa hali ya juu na bila shaka unaitendea haki taaluma yako ipasavyo, kwa hili nikupe hongera nadhani baada ya October 25 utajiunga na kina Ray na utasaidia tasnia ya filamu kufika mbali.

Lowassa umekosa sera umekuwa ukirudia yale yale kila kukicha.

Umati mkubwa uliookuwepo pale jangwani kwa siku ya jana ulikuja kusikiliza ilani ya UKAWA na walitaka kusikia kutoka mdomoni kwako ukahaidi utawafanyia nini, unasema unaleta mabadiliko,hicho ndicho walichotaka kusikia na si habari za babu seya, bilali na masheikh wa uhamsho.

Kuwaambia wananchi wakasome ilani kwenye website ni kuwakosea heshima na kutothamini muda wao. Ni wananchi wangapi wenye access ya internet?

Ndiyo wananchi tunataka mabadiliko lakini siyo mabadiliko ya kiini macho kama yako lowassa.

Hotuba yako imeshindwa kukidhi kabisa kiu ya wananchi, umekosa mipango umekuwa mtu wa kusemewa na wapambe wako,wewe ndiyo mtendaji tunataka useme wewe.

Chadema huu ndiyo mwisho wenu,baada ya uchaguzi tunawasahau kabisa kwenye ulingo wa siasa. Mmeamua kulamba matapishi yenu na kutaka kuwalazimisha watanzania walambe pamoja na nyie ila wengi tumejitambua tumevunja uaminifu wetu kwenu.

Kama Mbowe aliamua kuchenji gia hewani sisi tutachenji ardhini ifikapo October 25.

Siioni nafasi ya Lowassa na UKAWA baada ya uchaguzi.

Kwaheri Lowassa, kwa heri UKAWA.
 
Subiri sindano ikuingie wewe. Wasomi maprofesa wameona cha maana kutoka kwa Lowasa jana. Hotuba yake imelenga kila sekta na inatekelezeka. Sasa wewe aliekutuma kamwambie watanzania hawataki propaganda wanataka mabadiliko na mabafiliko ni kupitia kwa Lowasa.
Mnajisumbua tu ndugu zangu wana ccm...
 
Subiri sindano ikuingie wewe. Wasomi maprofesa wameona cha maana kutoka kwa Lowasa jana. Hotuba yake imelenga kila sekta na inatekelezeka. Sasa wewe aliekutuma kamwambie watanzania hawataki propaganda wanataka mabadiliko na mabafiliko ni kupitia kwa Lowasa.
Mnajisumbua tu ndugu zangu wana ccm...

Watanzania tunataka mabadiliko siyo kiini macho. Mfikishie salamu zangu.
 
kumwelewa mtu lazima uwe makini, ilani ya chadema imetulia sema tu kuwa mmezoea maneno mengi.
 
siku zote ma jiniasi (watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri) hawanaga maneno mengi ila vitendo hilo lisikupe shaka, watu jana jagwani tulienda kumuona lowasa na majembe wengine hata wasingeongea chochote still hatupo tayari kuichagua CCM.
unajua story ya mtaani mida hii ni kuwa hata kama UKAWA WANGESIMAMISHA JIWE TUTACHAGUA HILO ILA SIYO HAWA MIUNGU WATU WA CCM
 
siku zote ma jiniasi (watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri) hawanaga maneno mengi ila vitendo hilo lisikupe shaka, watu jana jagwani tulienda kumuona lowasa na majembe wengine hata wasingeongea chochote still hatupo tayari kuichagua CCM.
unajua story ya mtaani mida hii ni kuwa hata kama UKAWA WANGESIMAMISHA JIWE TUTACHAGUA HILO ILA SIYO HAWA MIUNGU WATU WA CCM

Una tatizo siyo bure. Napata shida na uwezo wako wa kufikiri.
 
Una tatizo siyo bure. Napata shida na uwezo wako wa kufikiri.
ni vigumu sana akiri ndogo kuielewa kubwa... hivi unakumbuka uzinduzi wa kampeni CCM mwaka 2005 JK2 alivoongea vizuri na maneno mengi na yenye mvuto? kipi kafanya sasa. I REPEAT CCM nahisi ishalaaniwa so hata ashuke malaika agombee uraisi simpi kura yangu ng'oooo. LOWASA JANA TULIMUELEWA SANA WANA UKAWA.... ILA WANA CCM ndo mnapata shida kuelewa.
 
ni vigumu sana akiri ndogo kuielewa kubwa... hivi unakumbuka uzinduzi wa kampeni CCM mwaka 2005 JK2 alivoongea vizuri na maneno mengi na yenye mvuto? kipi kafanya sasa. I REPEAT CCM nahisi ishalaaniwa so hata ashuke malaika agombee uraisi simpi kura yangu ng'oooo. LOWASA JANA TULIMUELEWA SANA WANA UKAWA.... ILA WANA CCM ndo mnapata shida kuelewa.

Nachelea kusema jambo maana sijui umri wako laiti ningejua ningekueleza.una matatizo mkubwa ya ubongo.
 
Nachelea kusema jambo maana sijui umri wako laiti ningejua ningekueleza.una matatizo mkubwa ya ubongo.
dah kumbe mpo wengi eeh!! laiti ningekuwa mods ningewadelete kitambo sana JF, maana mnakera.... kama hamuwaelewi UKAWA si muwe bize kumfuatilia yule ngosha wenu bhana
 
Linamo sisiem ingelikuwa inatekeleza sera zake sidhani kama leo tungeongelea maadui 3 tulioambiwa na Nyerere toka uhuru mpaka magufuli anawanadi leo

Kajipange uje tena.
 
Last edited by a moderator:
heee kipaji kimegeuka na kuwa taaluma!!! anawatesa huyu mtu hatari. Nasikia hata hamlali siku hizi kazi ni kuumiza akili kupambana naye. tatizo siyo yeye tatizo ni watanzania kuwashtukia na kuamua kudai mabadiliko ya kweli
 
siku zote ma jiniasi (watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri) hawanaga maneno mengi ila vitendo hilo lisikupe shaka, watu jana jagwani tulienda kumuona lowasa na majembe wengine hata wasingeongea chochote still hatupo tayari kuichagua CCM.
unajua story ya mtaani mida hii ni kuwa hata kama UKAWA WANGESIMAMISHA JIWE TUTACHAGUA HILO ILA SIYO HAWA MIUNGU WATU WA CCM

wewe naye ni mtanzania kweli?
 
Back
Top Bottom