Nobunaga
JF-Expert Member
- Mar 22, 2019
- 1,169
- 4,987
Kwa wale watumiaji wa mtandao wa Vodacom ambao bado hamjasanuka basi nawasanua unaweza kupunguza spidi ya intaneti yako ili kuzuia bado kuisha haraka.
Kwa kawaida usipo-limit matumizi ya spidi basi Vodacom wanakuwezesha kuperuzi kwa spidi ya hadi 100Mbps. Hii ni spidi ya hatari kwa bando lako, kama una matumizi ya kawaida tuu hii ni spidi kubwa sana ambayo kwa hakika itafanya bando likatike ndani ya muda mfupi na kuishia kuwaona Vodacom wezi. Spidi hii ni sawa na kutumia 12.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu (1Mbps = 0.125MBps).
Lakini ukipunguza spidi ya intaneti, utaweza kupewa kasi ya juu isiyozidi 5Mbps. Kutoka 100Mbps mpaka 5Mbps ni tofauti kubwa sana. Spidi hii ni sawa na kutumia 625KB hadi 1.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu. Hii ni reasonable spidi ambayo haitakula bando lako sana.
Kujua tofauti ya Mbps na MBps soma hapa kuna member alielezea vizuri sana tofauti zake.
Kwa kawaida usipo-limit matumizi ya spidi basi Vodacom wanakuwezesha kuperuzi kwa spidi ya hadi 100Mbps. Hii ni spidi ya hatari kwa bando lako, kama una matumizi ya kawaida tuu hii ni spidi kubwa sana ambayo kwa hakika itafanya bando likatike ndani ya muda mfupi na kuishia kuwaona Vodacom wezi. Spidi hii ni sawa na kutumia 12.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu (1Mbps = 0.125MBps).
Lakini ukipunguza spidi ya intaneti, utaweza kupewa kasi ya juu isiyozidi 5Mbps. Kutoka 100Mbps mpaka 5Mbps ni tofauti kubwa sana. Spidi hii ni sawa na kutumia 625KB hadi 1.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu. Hii ni reasonable spidi ambayo haitakula bando lako sana.
Kujua tofauti ya Mbps na MBps soma hapa kuna member alielezea vizuri sana tofauti zake.
Sasa ili kupunguza au kuongeza spidi ya intaneti fuata hatua hizi:
1. Ingia kwenye menu ya *149*01#
2. Kisha nenda namba 3 (Nunua Bando)
3. Kisha nenda namba 2 (Intaneti)
4. Kisha namba 4 (Spidi ya Intaneti)
5. Kisha utachua kati ya 1 (Ongeza Spidi) au 2 (Punguza Spidi) kulingana na unavyoona wewe.[/]
1. Ingia kwenye menu ya *149*01#
2. Kisha nenda namba 3 (Nunua Bando)
3. Kisha nenda namba 2 (Intaneti)
4. Kisha namba 4 (Spidi ya Intaneti)
5. Kisha utachua kati ya 1 (Ongeza Spidi) au 2 (Punguza Spidi) kulingana na unavyoona wewe.[/]