Kwa wateja wa Vodacom: Jinsi ya Kupunguza Spidi ya Intaneti ili Bando lisiishe haraka

Nobunaga

JF-Expert Member
Mar 22, 2019
1,169
4,987
Kwa wale watumiaji wa mtandao wa Vodacom ambao bado hamjasanuka basi nawasanua unaweza kupunguza spidi ya intaneti yako ili kuzuia bado kuisha haraka.

Kwa kawaida usipo-limit matumizi ya spidi basi Vodacom wanakuwezesha kuperuzi kwa spidi ya hadi 100Mbps. Hii ni spidi ya hatari kwa bando lako, kama una matumizi ya kawaida tuu hii ni spidi kubwa sana ambayo kwa hakika itafanya bando likatike ndani ya muda mfupi na kuishia kuwaona Vodacom wezi. Spidi hii ni sawa na kutumia 12.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu (1Mbps = 0.125MBps).

Lakini ukipunguza spidi ya intaneti, utaweza kupewa kasi ya juu isiyozidi 5Mbps. Kutoka 100Mbps mpaka 5Mbps ni tofauti kubwa sana. Spidi hii ni sawa na kutumia 625KB hadi 1.5MB kwa sekunde endapo unadownload kitu. Hii ni reasonable spidi ambayo haitakula bando lako sana.

Kujua tofauti ya Mbps na MBps soma hapa kuna member alielezea vizuri sana tofauti zake.​

IMG_20220801_213941.jpg



Sasa ili kupunguza au kuongeza spidi ya intaneti fuata hatua hizi:

1. Ingia kwenye menu ya *149*01#
2. Kisha nenda namba 3 (Nunua Bando)
3. Kisha nenda namba 2 (Intaneti)
4. Kisha namba 4 (Spidi ya Intaneti)
5. Kisha utachua kati ya 1 (Ongeza Spidi) au 2 (Punguza Spidi) kulingana na unavyoona wewe.[/]


IMG_20220812_125117.jpg


IMG_20220812_125206.jpg
IMG_20220801_213941.jpg
IMG_20220812_125206.jpg
IMG_20220812_125117.jpg
IMG_20220812_125206.jpg


 
Hii ni sawa na nihitaji kupakua kitu cha MBs 500, ila nikaamua nisikipate ndani ya dakika moja, nishinde siku nzima nakipakua, huku najidanganya kwamba MBs zimekaa sana kumbe niliyekaa sana ni mimi.

Nadhani dawa ni moja kati ya machaguo mawili, kwanza ni MBs kuongezeka kwa pesa ile ile, au mbili ni kupunguza matumizi ili kutumia pesa ile ile.
 
Mazeee hi ni Uwongo ni nimeona haina haja ya kulimt speed speed ya vodacom haizuilik kwa namna hiyo labda uwende settings ukaweke 2G maana hata 3G ya vodacom ni hatari weka pesa enjoy speed

nimejarb kuweka kamaulvo seme lakin wap 5Mbps nilitarajia isivuke 700kb/s lakin inaenda had 5MB/s ambayo ni sawa na 40Mbps

nkaona haitosh nikaenda kwenye app yangu ya kupima na speed lakn inafka had 6MB/s ambayo sawaya 48Mbps

nimeona bora niweke full speed hakuna kinacho zuilika labda uwende settings ukaweke 2G

IMG_4660.jpg

IMG_4661.jpg

IMG_4662.jpg

IMG_4663.jpg

IMG_4664.jpg

IMG_4665.jpg

IMG_4666.jpg

IMG_4667.jpg

IMG_4669.jpg
 
Back
Top Bottom