FredKavishe
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,090
- 322
Habari zenu wandugu baada ya kutafakari sana jinsi ya mbinu za CCM nikamua kuja na wazo hili.vijana wa CCM na wajumbe sasa wanapita kila nyumba kuvutia vijana wajiunge na chama chao kwamba watapata mikopo bank ya vijana ikianza na ni lazima uwe mwana ccm kujiunga na chama chao.
Sasa tujikite kwenye hoja yangu lengo ni kuvutia wanawake kujiunga kwa njia ya pekee na chadema bado mpaka sasa hatujavutia kina mama wengi kujiunga ya chama chetu ratio ni ndogo sana unaweza kusema katika kila watu 10 mikutanoni kwa chadema ni mwanamke mmoja tu 9 wote ni wanaume hii hali inatisha.
Lakini pia tukitumia matokeo ya sensa iliyopita kuna idadi kubwa ya wanawake na hata ya sasa haitakuwa tofauti idadi yao itazidi maradufu hata katika daftari la kupiga kura idadi nyingi ya wapiga kura ni wanawake lakini bado utokezi wa wanawake kwenye siasa umekua mdogo sana haswa kwa chadema hilo jambo liko wazi kabisa.
Mpango wangu huu napenda kusema nishauanza sasa nimetengeneza katimu cha wanawake wa chadema 30 idadi itakuwa wengi ni wanachuo lengo ni kupata wanachuo wanawake 1000 kabla ya mwezi wa tano 2015.wawe tayari kukitumikia chama chao na kufanya mengine kwa ajili ya uchaguzi.
Lengo langu ni kuvutia kina mama na wasichana kujiunga na CHADEMA kwa wingi na mimi nimejiwekea kuvutia wanawake wasomi wa vyuo vikuu 1000 mpaka itakapofika 2015,baadhi wako ndani ya Tanzania nishawapatia kadi zao za uanachama baada ya kukidhi vigezo nivyotaka.
VIGEZO:
1:Kwanza Uielewe CHADEMA ni nini
Hapa ninawapatia elimu ndogo hawa wanawake wa vyuoni kuilewa CHADEMA historia yake toka kuanzishwa na je inasimama kwenye siasa za mkondo gani,nini malengo ya CHADEMA, je mwanamke akiingia na CHADEMA atanufaika na nini tofauti na akiwa CCM kupewa na khanga
2:Nawapatia Katiba Ya chama Wakaisome Ndani ya Wiki Mbili
Nawapatia katiba ya chama waisome waielewe kabla sijawapa kadi zao za kuwa wanachama wa CHADEMA sasa kuna tatizo wanachama wengi wanajiunga kwenye vyama bila kujua katiba za vyama husika mtu anakua hajui mipaka yake kikatiba.Wakishakubaliana na malengo ya katiba ndo wanapata kadi ya uanachama.
3:Kuelewa Sera,mlengo,Ilani zilizopita za CHADEMA
4:Kuchukizwa kweli na ufisadi,rushwa
Hapa kidogo inakua ngumu kwasababu huwezi kujua malengo na mawazo ya mtu kutoka moyoni lakini tunaweza mbadili mtu tukiona hafai.
Nini haswa lengo la kuanzisha hii:
1:kupata nguvu ya wanawake ambao kimsingi ni wengi na ndo wapiga kura
2:Ukikubalika na wanawake basi jamii itakukubali wakinamama wako tayari kwa ujenzi wa chama kujitolea kwa chochote kile
3:Kuvutia wanawake wengi kujiunga na mapambano ya kukijenga chama na kuhakikisha kinashika hatamu ya nchi 2015.
Nini faida ya kuwa kwenye hii kwa wanawake wa vyuoni
1:Kutakua na elimu ya uraia
2:Elimu ya ujasilia mali itatolewa kwa wanawake wote jinsi wanavyoweza kutumia akili zao kujiajiri.
3:kuhamasisha wanawake wengi kujiunga na CHADEMA
Lengo la hii hoja ni kuwa nikitimiza lengo langu la kupata wasomi 1000 kujiunga na CHADEMA hawa wasomi 1000 watapaswa watuletee wanachama 100 kila mmoja kwa wanawake nitakuwa nimefanikiwa kupata kina mama 100000 mpaka mwezi wa 5 2015 ambao watakua wapiga kura kwenye majimbo mbalimbali na kulinda kura.
Pili ni kuwapa Elimu kuwa unaweza kuwa mpambanaji lakini usiwe kiongozi ndani ya chama ukatoa mawazo ukasidia kwenye ujenzi wa chama.lakini pia unaweza ukawa muajiriwa hata serikali lakini ukausika kuwa mwanachama wa chadema.
Shime kina mama mjiunge na chama kitakacho wakomboa
1:kuwaboreshea huduma za maji kuwa karibu
Mfano karatu,arumeru visima vinachimbwa na bado hatuna serikali
2:kuwaletea mbinu mbadala za kuweza kujiajiri kwa mitaji midogo
3:kuwafanya wanawake muthaminiwe muheshimiwe mupate msaada wa kisheria pale mnaponyanyaswa kuvunjiwa mabanda yenu na mgambo.
4:kuwapa watoto wenu elimu bure
N.B:Nimekuwa nikuuliza na baadhi ya watu kuhusu yale matembezi kutunisha mfuko wa M4C ni kwamba wazo liko ndani ya chama sasa linaandaliwa mchakato vizuri kama wataona linafaa watalileta tena kwenu msife moyo mapambano yanaendelea.
F.K
Sasa tujikite kwenye hoja yangu lengo ni kuvutia wanawake kujiunga kwa njia ya pekee na chadema bado mpaka sasa hatujavutia kina mama wengi kujiunga ya chama chetu ratio ni ndogo sana unaweza kusema katika kila watu 10 mikutanoni kwa chadema ni mwanamke mmoja tu 9 wote ni wanaume hii hali inatisha.
Lakini pia tukitumia matokeo ya sensa iliyopita kuna idadi kubwa ya wanawake na hata ya sasa haitakuwa tofauti idadi yao itazidi maradufu hata katika daftari la kupiga kura idadi nyingi ya wapiga kura ni wanawake lakini bado utokezi wa wanawake kwenye siasa umekua mdogo sana haswa kwa chadema hilo jambo liko wazi kabisa.
Mpango wangu huu napenda kusema nishauanza sasa nimetengeneza katimu cha wanawake wa chadema 30 idadi itakuwa wengi ni wanachuo lengo ni kupata wanachuo wanawake 1000 kabla ya mwezi wa tano 2015.wawe tayari kukitumikia chama chao na kufanya mengine kwa ajili ya uchaguzi.
Lengo langu ni kuvutia kina mama na wasichana kujiunga na CHADEMA kwa wingi na mimi nimejiwekea kuvutia wanawake wasomi wa vyuo vikuu 1000 mpaka itakapofika 2015,baadhi wako ndani ya Tanzania nishawapatia kadi zao za uanachama baada ya kukidhi vigezo nivyotaka.
VIGEZO:
1:Kwanza Uielewe CHADEMA ni nini
Hapa ninawapatia elimu ndogo hawa wanawake wa vyuoni kuilewa CHADEMA historia yake toka kuanzishwa na je inasimama kwenye siasa za mkondo gani,nini malengo ya CHADEMA, je mwanamke akiingia na CHADEMA atanufaika na nini tofauti na akiwa CCM kupewa na khanga
2:Nawapatia Katiba Ya chama Wakaisome Ndani ya Wiki Mbili
Nawapatia katiba ya chama waisome waielewe kabla sijawapa kadi zao za kuwa wanachama wa CHADEMA sasa kuna tatizo wanachama wengi wanajiunga kwenye vyama bila kujua katiba za vyama husika mtu anakua hajui mipaka yake kikatiba.Wakishakubaliana na malengo ya katiba ndo wanapata kadi ya uanachama.
3:Kuelewa Sera,mlengo,Ilani zilizopita za CHADEMA
4:Kuchukizwa kweli na ufisadi,rushwa
Hapa kidogo inakua ngumu kwasababu huwezi kujua malengo na mawazo ya mtu kutoka moyoni lakini tunaweza mbadili mtu tukiona hafai.
Nini haswa lengo la kuanzisha hii:
1:kupata nguvu ya wanawake ambao kimsingi ni wengi na ndo wapiga kura
2:Ukikubalika na wanawake basi jamii itakukubali wakinamama wako tayari kwa ujenzi wa chama kujitolea kwa chochote kile
3:Kuvutia wanawake wengi kujiunga na mapambano ya kukijenga chama na kuhakikisha kinashika hatamu ya nchi 2015.
Nini faida ya kuwa kwenye hii kwa wanawake wa vyuoni
1:Kutakua na elimu ya uraia
2:Elimu ya ujasilia mali itatolewa kwa wanawake wote jinsi wanavyoweza kutumia akili zao kujiajiri.
3:kuhamasisha wanawake wengi kujiunga na CHADEMA
Lengo la hii hoja ni kuwa nikitimiza lengo langu la kupata wasomi 1000 kujiunga na CHADEMA hawa wasomi 1000 watapaswa watuletee wanachama 100 kila mmoja kwa wanawake nitakuwa nimefanikiwa kupata kina mama 100000 mpaka mwezi wa 5 2015 ambao watakua wapiga kura kwenye majimbo mbalimbali na kulinda kura.
Pili ni kuwapa Elimu kuwa unaweza kuwa mpambanaji lakini usiwe kiongozi ndani ya chama ukatoa mawazo ukasidia kwenye ujenzi wa chama.lakini pia unaweza ukawa muajiriwa hata serikali lakini ukausika kuwa mwanachama wa chadema.
Shime kina mama mjiunge na chama kitakacho wakomboa
1:kuwaboreshea huduma za maji kuwa karibu
Mfano karatu,arumeru visima vinachimbwa na bado hatuna serikali
2:kuwaletea mbinu mbadala za kuweza kujiajiri kwa mitaji midogo
3:kuwafanya wanawake muthaminiwe muheshimiwe mupate msaada wa kisheria pale mnaponyanyaswa kuvunjiwa mabanda yenu na mgambo.
4:kuwapa watoto wenu elimu bure
N.B:Nimekuwa nikuuliza na baadhi ya watu kuhusu yale matembezi kutunisha mfuko wa M4C ni kwamba wazo liko ndani ya chama sasa linaandaliwa mchakato vizuri kama wataona linafaa watalileta tena kwenu msife moyo mapambano yanaendelea.
F.K