Kwa wanaotaka kujiunga vyuo vikuu 2018/19 tu

Kwa wanaotaka kujiunga vyuo vikuu 2018/19 tu

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,252
Reaction score
16,171
Nafahamu vyuo vikuu ni vichache nchini na kila mtu anapenda kusoma chuo kikuu. Lakini kama wewe au familia yako hamna uwezo wa kulipa kwa wakati tafadhali sana usichague kwenda kusoma Vyuo vikuu vya binafsi binafsi (private private) hutaweza au utanyanyasika mnooooooo.

Asilimia 99% ya vyuo hivi huwa vinategemea 99% ada ya wanafunzi kujiendesha, hivyo hawana mzaha na wasiolipita ada hata kidogo.

Hivi ni vile vyuo ambavyo hata ukipewa 3,100,000 na bodi ya mikopo lazima pia uongeze hadi 4,000,000 kutoka mfukoni kwako kuongezea kwenye fee.

Jiulize mara tatu tatu kama familia yako itamudu kulipa kwa wakati 7,000,000 kwa mwaka bila mkopo au 4,000,000 kwa kuchanganya na mkopo vinginevyo tafuta chuo cha kusoma Diploma tu yaishe.

Baadhi ya karaha utazozipata kama huna hela hizo ni pamoja na:
1. Kukataliwa kujiandikisha kuwa mwanafunzi hata kama umechaguliwa chuo hicho.
2. Kuzuiwa kuingia darasani kama hujawalipa
3. Kutolewa darasani kila wakati
4. Jina lako kusomwa na kubandikwa kwenye mbao za matangazo kama mtu anayeidaiwa
5. Kuzuiwa kupata chumba kwenye hostel za chuo hicho
6. Kuzuiwa kufanya mitihani
7. Kukosa muda wa kujisomea wakati unahangaikia deni la chuo
8. Kudhalilika mbele ya wanachuo wenzako na watu wengine
9. Ni rahisi mno kujiingiza kwenye vitendo usivyovipenda
10.Uhusiano wako na uongozi/walimu wa taasisi unakuwa mbaya. Hutatamani kurudi tena hapo baada ya kumaliza.
11.
12.
 
Tatizo kubwa hapa n kukosekana kwa taarfa sahih tangu ukiwa advance kwa maana wengi wanafikiri ukifka Chuo mambo mteremko tuu kama enzi za akna JK

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo kubwa hapa n kukosekana kwa taarfa sahih tangu ukiwa advance kwa maana wengi wanafikiri ukifka Chuo mambo mteremko tuu kama enzi za akna JK

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana kama hujalipa ada mambo hayatakuwa mteremko hata kidogo. Wanafunzi wanaopata shida sana wengi wao ama wanalelewa na mzazi mmoja tu, hawana wazazi, wazazi wao ni wazee sana, wanategemea kulima mahindi ambayo hayana bei au wazazi wao wanakwaruzana mara kwa mara kwa mambo yao ya kifamilia.
 
Hivi ni vile vyuo ambavyo hata ukipewa 3,100,000 na bodi ya mikopo lazima pia uongeze hadi 4,000,000 kutoka mfukoni kwako kuongezea kwenye fee.

Jiulize mara tatu tatu kama familia yako itamudu kulipa kwa wakati 7,000,000 kwa mwaka bila mkopo au 4,000,000 kwa kuchanganya na mkopo vinginevyo tafuta chuo cha kusoma Diploma tu yaishe.
Mkuu naona taarifa yako haielezi ukweli wote na kwa kiasi fulani inatishia waombaji. Siyo wote watakao isoma kwa umakini unaotakiwa. Ada za vyuo hivi zina range kubwa kutegemea unakwenda kusoma nini. Kuna koozi ambazo ada ni sawa na vyuo vya serikali na zipo ambazo ada iko juu kupita vyuo vya serikali. Cha kusisitiza waombaji wahakikishe wanauwezo wa kulipa ada husika. Na hata wale wanaokwenda vyuo vya serikali sio wote wanapata mkopo-na ni wengi wanaokosa siku hizi hivyo angalizo lako huko pia linatakiwa upande huo.
Hayo 10 uliyo orodhesha hutokea pia vyuo vya umma kama muda wa kulipa ada ukipita nawe hujalipa. Nakumbuka vijana wa SUA ambao walichelewa kulipa ada na walipo banwa wakati wa mitihani, malipo yao yalidunda ikabidi warudie mwaka.


WENGI HAWAELEWI
Hata mimi sikuelewa LoL
 
Mkuu naona taarifa yako haielezi ukweli wote na kwa kiasi fulani inatishia waombaji. Siyo wote watakao isoma kwa umakini unaotakiwa. Ada za vyuo hivi zina range kubwa kutegemea unakwenda kusoma nini. Kuna koozi ambazo ada ni sawa na vyuo vya serikali na zipo ambazo ada iko juu kupita vyuo vya serikali. Cha kusisitiza waombaji wahakikishe wanauwezo wa kulipa ada husika. Na hata wale wanaokwenda vyuo vya serikali sio wote wanapata mkopo-na ni wengi wanaokosa siku hizi hivyo angalizo lako huko pia linatakiwa upande huo.
Hayo 10 uliyo orodhesha hutokea pia vyuo vya umma kama muda wa kulipa ada ukipita nawe hujalipa. Nakumbuka vijana wa SUA ambao walichelewa kulipa ada na walipo banwa wakati wa mitihani, malipo yao yalidunda ikabidi warudie mwaka.


Hata mimi sikuelewa LoL
soma vizuri taarifa yangu, niliposema ......hadi 4,000,000 nilimaanisha "range" kutoka 0-4,000,000. kaka vyuo vya private vingi havisemi ukweli au waombaji wenyewe hawaufahamu ukweli wa mambo. Wako waombaji ambao wanadhani wakipata mkopo kwa 100% basi unatosha kusoma kwenye chuo husika. Na hapo ndiyo shida inapoanzia, mwanafunzi kapewa mkopo kwa 100% lakini anaambiwa alipe tena hadi sh. 4,000,000 au zaidi nyingine kutoka kwa wazazi wake. Pamoja kwamba chuo kimeupokea mkopo wake na wameutumia kuendeshea chuo lakini huyu mwanafunzi bado chamoto kama nilivyosema anakiona, yaana ni kama hajalipa kitu chochote kile pale shuleni.

Kwasababu hiyo huku kwetu A town viko vyuo sasa ambavyo kama huna hela hawakuchagui kabisa hata kama sifa unazo lukuki, wanakwambia waziwazi kuwa usikanyage kabisa chuoni kwao.
 
soma vizuri taarifa yangu, niliposema ......hadi 4,000,000 nilimaanisha "range" kutoka 0-4,000,000. kaka vyuo vya private vingi havisemi ukweli au waombaji wenyewe hawaufahamu ukweli wa mambo. Wako waombaji ambao wanadhani wakipata mkopo kwa 100% basi unatosha kusoma kwenye chuo husika. Na hapo ndiyo shida inapoanzia, mwanafunzi kapewa mkopo kwa 100% lakini anaambiwa alipe tena hadi sh. 4,000,000 au zaidi nyingine kutoka kwa wazazi wake. Pamoja kwamba chuo kimeupokea mkopo wake na wameutumia kuendeshea chuo lakini huyu mwanafunzi bado chamoto kama nilivyosema anakiona, yaana ni kama hajalipa kitu chochote kile pale shuleni.
Nimekusoma vizuri sana na ndiyo maana nimesema "Siyo wote watakao isoma kwa umakini unaotakiwa". Ni muhimu kupitia fee structure ya chuo unachochagua.
 
Nimekusoma vizuri sana na ndiyo maana nimesema "Siyo wote watakao isoma kwa umakini unaotakiwa". Ni muhimu kupitia fee structure ya chuo unachochagua.
Kweli kabisa, hapo ndipo chimbuko la tatizo linapoanzia. Vyuo vingi vinapotoa matangazo yao kwenye magazeti, redio na luninga ambazo hata wazazi wa kawaida wanaweza kuyasikiliza na kuyaelewa kwa ufasaha huwa hawaweki taarifa juu ya ada za vyuo vyao na namna ya kuilipa na hatua zitakazochukuliwa kwa asiyelipa.

Mara nyingi taarifa kuhusu ada za vyuo ziko kwenye internet (TCU website, tovuti za vyuo, facebook, nk) ambako wazazi wengi hawana uwezo wa kuzi access. Hivyo, vijana ndio wanaoweza kuzipata la Kwa nakusudia au kwakuwa huwa hawawambii ukweli wazazi wao kuhusu ada hizo kwa kuogopa kuwashitua wazazi wao na kukosa kupata chuo. Na baadhi ya vijana huko wilayani hawaelewi kabisa na wala kwenye maonyesho ya vyuo vikuu hawaendi.
 
Kweli kabisa, hapo ndipo chimbuko la tatizo linapoanzia. Vyuo vingingi vinapotoa matangazo yao kwenye magazeti, redio na luninga ambazo hata wazazi wa kawaida wanaweza kuyasikiliza na kuyaelewa kwa ufasaha huwa hawaweki taarifa juu ya ada za vyuo vyao na namna ya kuilipa na hatua zitakazochukuliwa kwa asiyelipa.

Mara nyingi taarifa kuhusu ada za vyuo ziko kwenye internet (TCU website, tovuti za vyuo, facebook, nk) ambako wazazi wengi hawana uwezo wa kuzi access. Hivyo, vijana hawawambii ukweli wazazi wao kuhusu ada hizo kwa kuogopa kuwashitua wazazi wao na kukosa kupata chuo. Na baadhi ya vijana huko wilayani hawaelewi kabisa na wala kwenye maonyesho ya vyuo vikuu hawaendi.
Mwanzo TCU kwenye guide book zao walikua wanaweka ada ya kila course na cut off point za mwaka uliyopita vitu ambavyo ni vya msaada lakini takribani miaka 2-3 iliyopita wameacha hilo. Lakini kama msimamizi wa udahili wangefanya hima kutoa taarifa hizo .
Maonyesho ya vyuo vikuu ni mazuri lakini yako Dar huko sehemu nyingine ni kudra ya Mwenyezi Mungu.
 
Back
Top Bottom